< Deuteronomy 26 >

1 When you have come into the land that Yahweh your God is giving you as an inheritance, and when you possess it and live in it,
Mtakapokuwa mmeingia nchi ile ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi na mtakapokuwa mmeimiliki na kukaa ndani yake,
2 then you must take some of the first of all the harvest of the land that you have brought in from the land that Yahweh your God is giving you. You must put it in a basket and go to the place that Yahweh your God will choose as his sanctuary.
chukueni baadhi ya mavuno ya kwanza ya yale yote mtakayozalisha kutoka udongo wa nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa na mweke kwenye kapu. Kisha uende mahali ambapo Bwana Mungu wako atapachagua kuwa makao kwa ajili ya Jina lake
3 You must go to the priest who will be serving in those days and say to him, 'I acknowledge today to Yahweh your God that I have come to the land that Yahweh swore to our ancestors to give us.'
na umwambie kuhani atakayekuwepo kwa wakati huo, “Ninatangaza leo kwa Bwana Mungu wako kwamba nimekuja katika nchi ambayo Bwana aliwaapia baba zetu kwamba atatupa.”
4 The priest must take the basket out of your hand and set it down before the altar of Yahweh your God.
Kuhani atapokea lile kapu mikononi mwako na kuliweka chini mbele ya madhabahu ya Bwana Mungu wako.
5 You must say before Yahweh your God, 'My ancestor was a wandering Aramean. He went down into Egypt and stayed there, and his people were few in number. There he became a great, mighty, and populous nation.
Kisha utatangaza mbele za Bwana Mungu wako: “Baba yangu alikuwa Mwaramu aliyekuwa anatangatanga, akaenda Misri pamoja na watu wachache, akaishi huko hadi akawa taifa kubwa, lenye nguvu na watu wengi.
6 The Egyptians treated us badly and afflicted us. They made us do the work of slaves.
Lakini Wamisri walituonea na kututaabisha, wakitufanyisha kazi ngumu.
7 We cried out to Yahweh, the God of our fathers, and he heard our voice and saw our affliction, our labor, and our oppression.
Kisha tulimlilia Bwana, Mungu wa baba zetu, naye Bwana akasikia sauti yetu na akaona huzuni yetu, taabu yetu na mateso yetu.
8 Yahweh brought us out of Egypt with a mighty hand, with an outstretched arm, with great fearsomeness, with signs, and with wonders;
Kwa hiyo Bwana akatutoa nchi ya Misri kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa, pamoja na utisho mkuu, ishara za miujiza na maajabu.
9 and he has brought us to this place and has given us this land, a land that flows with milk and honey.
Akatuleta mahali hapa akatupa nchi hii, nchi inayotiririka maziwa na asali;
10 Now look, I have brought the first of the harvest of the land that you, Yahweh, have given me.' You must set it down before Yahweh your God and worship before him;
nami sasa ninaleta malimbuko ya ardhi ambayo wewe, Ee Bwana, umenipa.” Weka kapu mbele za Bwana Mungu wako na usujudu mbele zake.
11 and you must rejoice in all the good that Yahweh your God has done for you, for your house—you, and the Levite, and the foreigner who is among you.
Kisha wewe pamoja na Walawi na wageni wote walioko miongoni mwenu mtafurahi katika vitu vyote vizuri ambavyo Bwana Mungu wenu amewapa pamoja na wa nyumbani mwenu.
12 When you have finished giving all the tithe of your harvest in the third year, that is, the year of tithing, then you must give it to the Levite, to the foreigner, to the fatherless, and to the widow, so that they may eat within your city gates and be filled.
Wakati utakapokuwa umeshatoa zaka zote za mazao yako katika mwaka wa tatu, ambao ni mwaka wa zaka, utampa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, ili waweze kula katika miji yenu na kushiba.
13 You must say before Yahweh your God, 'I have brought out of my house the things that belong to Yahweh, and have given them to the Levite, to the foreigner, to the fatherless, and to the widow, according to all your commandments that you have given me. I have not transgressed any of your commandments, neither have I forgotten them.
Kisha umwambie Bwana Mungu wako: “Nimeondoa katika nyumba yangu ile sehemu iliyowekwa wakfu na nimempa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, kulingana na yote uliyoamuru. Sijazihalifu amri zako wala kusahau hata mojawapo.
14 I have not eaten any of it in my mourning, nor have I put it somewhere else when I was impure, nor have I given any of it in honor of the dead. I have listened to the voice of Yahweh my God; I have obeyed everything you have commanded me to do.
Sijala sehemu iliyowekwa wakfu wakati nilipokuwa nikiomboleza, wala sijaondoa mojawapo wakati nilipokuwa najisi, wala sijatoa sehemu yake yoyote kwa wafu. Nimemtii Bwana Mungu wangu; nimefanya kila kitu ulichoniamuru.
15 Look down from the holy place where you live, from heaven, and bless your people Israel, and the land that you have given us, as you had sworn to our fathers, a land flowing with milk and honey.'
Angalia chini kutoka mbinguni, maskani yako matakatifu, uwabariki watu wako Israeli pamoja na nchi uliyotupa kama ulivyoahidi kwa kiapo kwa baba zetu, nchi inayotiririka maziwa na asali.”
16 Today Yahweh your God is commanding you to obey these statutes and decrees; you will therefore keep them and do them with all your heart and with all your soul.
Bwana Mungu wako anakuagiza leo kufuata amri hizi na sheria; zishike kwa bidii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.
17 You have declared today that Yahweh is your God, and that you will walk in his ways and keep his statutes, his commandments, and his decrees, and that you will listen to his voice.
Umetangaza leo kwamba Bwana ndiye Mungu wako na kwamba utafuata njia zake, kwamba utayashika maagizo yake, amri zake na sheria zake nawe utamtii.
18 Today Yahweh has declared that you are a people who are his own possession, as he had promised you, and that you are to keep all his commandments,
Naye Bwana ametangaza leo kwamba ninyi ni taifa lake, hazina yake ya thamani kama alivyoahidi, ili kwamba mpate kuyashika maagizo yake yote.
19 and he will set you high above all the other nations that he has made, and you will receive praise, fame, and honor. You will be a people that is set apart to Yahweh your God, just as he said.”
Ametangaza kwamba atawaweka juu kuliko mataifa mengine aliyoyafanya katika sifa, kuwa fahari na heshima, na kwamba mtakuwa taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu, kama alivyoahidi.

< Deuteronomy 26 >