< Deuteronomy 21 >

1 If someone is found killed in the land that Yahweh your God is giving you to possess, lying in the field, and it is not known who has attacked him;
Kama mtu akikutwa ameuawa, naye amelala kwenye shamba katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kuimiliki, wala haijulikani ni nani aliyemuua,
2 then your elders and your judges must go out, and they must measure to the cities that are around him who has been killed.
wazee wenu na waamuzi watatoka na kupima umbali kutoka maiti alipolala mpaka kwenye miji ya jirani.
3 Then the elders of the town nearest to the dead man's body must take a heifer from the herd, one that has never been put to work, and that has not borne the yoke.
Kisha wazee wa ule mji ulio karibu zaidi na yule maiti watamchukua mtamba ambaye hajapata kufanyishwa kazi na ambaye hajafungwa nira,
4 Then they must lead the heifer down to a valley with running water, a valley that has been neither plowed nor sown, and there in the valley they must break the heifer's neck.
na kumpeleka kwenye bonde ambalo halijapata kulimwa au kupandwa mazao na ambapo kuna chemchemi itiririkayo. Huko kwenye hilo bonde, wazee watamvunja yule mtamba shingo.
5 The priests, descendants of Levi, must come forward, for Yahweh your God has chosen them to serve him and give blessing in the name of Yahweh and to decide every case of dispute and assault by their word.
Makuhani, hao wana wa Lawi, watasogea mbele, kwa kuwa Bwana Mungu wenu, amewachagua kuhudumu na kutoa baraka katika jina la Bwana, na kuamua mashauri yote ya mabishano na mashambulio.
6 All the elders of the city that is the nearest to the killed man must wash their hands over the heifer whose neck was broken in the valley;
Ndipo wazee wote wa mji ulio karibu zaidi na huyo maiti watanawa mikono yao juu ya huyo mtamba ambaye shingo yake imevunjwa huko kwenye bonde,
7 and they must answer to the case and say, 'Our hands have not shed this blood, neither have our eyes seen it.
nao watatangaza: “Mikono yetu haikumwaga damu hii, wala macho yetu hayakuona likifanyika.
8 Forgive, Yahweh, your people Israel, whom you have redeemed, and do not put guilt for innocent bloodshed in the midst of your people Israel.' Then the bloodshed will be forgiven them.
Ee Bwana, ukubali upatanisho kwa watu wako Israeli, ambao umewakomboa, wala usiwahesabie watu wako hatia ya damu ya mtu asiyekuwa na hatia.” Nayo damu iliyomwagika itakuwa imefanyiwa upatanisho.
9 In this way you will put away the innocent blood from your midst, when you do what is right in the eyes of Yahweh.
Hivyo mtakuwa mmejitakasa wenyewe kutoka hatia ya kumwaga damu isiyokuwa na hatia, kwa kuwa mmefanya lile lililo sawa mbele za macho ya Bwana.
10 When you go out to do battle against your enemies and Yahweh your God gives you victory and puts them under your control, and you take them away as captives,
Mkienda vitani kupigana na adui zenu naye Bwana Mungu wenu akawatia adui mikononi mwenu, nanyi mkachukua mateka,
11 if you see among the captives a beautiful woman, and you have a desire for her and wish to take her for yourself as a wife,
kama ukiona miongoni mwa mateka mwanamke mzuri wa sura nawe wavutwa naye, waweza kumwoa akawa mke wako.
12 then you will bring her home to your house; she will shave her head and cut her nails.
Mlete nyumbani mwako, anyoe nywele na kukata kucha zake,
13 Then she will take off the clothes she was wearing when she was taken captive and she will remain in your house and mourn for her father and her mother a full month. After that you may sleep with her and be her husband, and she will be your wife.
avue nguo alizokuwa amevaa alipotekwa. Baada ya kuishi nyumbani mwako na kumwombolezea baba yake na mama yake kwa mwezi mzima, ndipo utakapoweza kumwendea na kuwa mume wake naye atakuwa mke wako.
14 But if you take no delight in her, then you may let her go where she wishes. But you must not sell her at all for money, and you must not treat her like a slave, because you have humiliated her.
Lakini kama hutaendelea kupendezwa naye, mwache aende popote anapotaka. Kamwe huwezi kumuuza au kumtendea kama mtumwa, kwa sababu utakuwa umemvunjia heshima.
15 If a man has two wives and one is loved and the other is hated, and they have both borne him children—both the beloved wife and the hated wife—if the firstborn son is of her that is hated,
Kama mwanaume ana wake wawili, naye anampenda mmoja na mwingine hampendi na wote wawili wamemzalia wana wa kiume, lakini mwana mzaliwa wa kwanza ni wa yule mke asiyempenda,
16 then on the day that the man causes his sons to inherit what he possesses, he may not make the son of the beloved wife the firstborn before the son of the hated wife, the son who is actually the firstborn.
wakati anapotoa wosia wa mali yake kwa wanawe, kamwe asitoe haki za mzaliwa wa kwanza kwa mwana wa mke ampendaye kwa upendeleo, badala ya mzaliwa hasa wa kwanza, ambaye ni mwana wa mke ambaye hampendi.
17 Instead, he must acknowledge the firstborn, the son of the hated wife, by giving him a double portion of all that he possesses; for that son is the beginning of his strength; the right of the firstborn belongs to him.
Ni lazima amkubali mwana wa mke asiyempenda kama mzaliwa wa kwanza kwa kumpa sehemu ya vile vyote alivyo navyo maradufu. Mwana huyo ni ishara ya kwanza ya nguvu za baba yake. Haki ya mzaliwa wa kwanza ni yake yeye.
18 If a man has a stubborn and rebellious son who will not obey the voice of his father or the voice of his mother, and who, even though they correct him, will not listen to them;
Kama mtu ana mwana mkaidi na mwasi ambaye hamtii baba yake na mama yake, na hasikii wazazi wanapomrudi,
19 then his father and his mother must lay hold on him and bring him out to the elders of his city and to the gate of his city.
baba yake na mama yake watamleta kwa wazee kwenye lango la mji wake.
20 They must say to the elders of his city, 'This son of ours is stubborn and rebellious; he will not obey our voice; he is a glutton and a drunkard.'
Watawaambia wazee, “Huyu mwanetu ni mkaidi na mwasi. Hatutii sisi, yeye ni mpotovu na mlevi.”
21 Then all the men of his city must stone him to death with stones; and you will remove the evil from among you. All Israel will hear of it and fear.
Kisha wanaume wote wa mjini mwake watampiga kwa mawe mpaka afe. Ndivyo imewapasa kuondoa maovu kati yenu. Israeli yote itasikia hili na kuogopa.
22 If a man has committed a sin worthy of death and he is put to death, and you hang him on a tree,
Kama mtu ana hatia ya kosa linalompasa kuuawa naye akauawa, mwili wake utaangikwa mtini,
23 then his body must not remain all night on the tree. Instead, you must surely bury him the same day; for whoever is hanged is cursed by God. Obey this commandment so that you do not defile the land that Yahweh your God is giving you as an inheritance.
kamwe msiuache mwili wake mtini usiku kucha. Hakikisheni mnauzika mwili wake siku ile ile, kwa sababu kila mtu anayeangikwa mtini yupo chini ya laana ya Mungu. Msiinajisi nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi wenu.

< Deuteronomy 21 >