< Deuteronomy 16 >

1 Observe the month of Abib, and keep the Passover to Yahweh your God, for in the month of Aviv Yahweh your God brought you out of Egypt by night.
Shikeni mwezi wa Abibu, na kuiadhimisha Pasaka ya Bwana Mungu wenu, kwa sababu katika mwezi wa Abibu, Mungu aliwatoa Misri usiku.
2 You will sacrifice the Passover to Yahweh your God with some of the flock and the herd in the place that Yahweh will choose as his sanctuary.
Mtatoa dhabihu ya Pasaka ya mnyama kwa Bwana Mungu wenu kutoka kundi lenu la mbuzi na kondoo au la ngʼombe, mahali pale ambapo Bwana atapachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake.
3 You will eat no leavened bread with it; seven days will you eat unleavened bread with it, the bread of affliction; for you came out of the land of Egypt in haste. Do this all the days of your life so that you may call to mind the day when you came out of the land of Egypt.
Msile nyama hiyo pamoja na mikate iliyotiwa chachu, lakini kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, mikate ya kujitesa, kwa sababu mliondoka Misri kwa haraka, ili kwamba siku zote za maisha yenu mpate kukumbuka wakati wenu wa kuondoka Misri.
4 No yeast must be seen among you within all your borders during seven days; nor must any of the meat that you sacrifice in the evening on the first day remain until the morning.
Chachu isionekane katika mali zenu katika nchi yenu yote kwa siku saba. Nyama yoyote ya dhabihu mtakayotoa jioni ya siku ya kwanza isibakizwe mpaka asubuhi.
5 You may not sacrifice the Passover within any of your city gates that Yahweh your God is giving you.
Kamwe msitoe dhabihu ya Pasaka katika mji wowote ambao Bwana Mungu wenu amewapa,
6 Instead, sacrifice at the place that Yahweh your God will choose as his sanctuary. There you will perform the sacrifice of the Passover in the evening at the going down of the sun, at the time of year that you came out of Egypt.
isipokuwa mahali atakapopachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake. Hapo ndipo lazima mtoe dhabihu ya Pasaka jioni, jua litakapotua, iwe kumbukumbu yenu ya kutoka Misri.
7 You must roast it and eat it at the place that Yahweh your God will choose; in the morning you will turn and go to your tents.
Okeni na mle mahali pale ambapo Bwana Mungu wenu atakapopachagua, kisha asubuhi mrudi kwenye mahema yenu.
8 For six days you will eat unleavened bread; on the seventh day there will be a solemn assembly for Yahweh your God; on that day you must do no work.
Kwa siku sita mtakula mikate isiyotiwa chachu na siku ya saba fanyeni kusanyiko kwa ajili ya Bwana Mungu wenu na msifanye kazi.
9 You will count seven weeks for yourselves; from the time you begin to put the sickle to the standing grain you must start counting seven weeks.
Mhesabu majuma saba tangu wakati mnapoanza kuchukua mundu kuvuna nafaka.
10 You must keep the Festival of Weeks for Yahweh your God with the contribution of a freewill offering from your hand that you will give, according as Yahweh your God has blessed you.
Kisha msherehekee Sikukuu ya Majuma kwa Bwana Mungu wenu kwa kutoa sadaka ya hiari kwa kadiri ya baraka ambayo Bwana Mungu wenu amewapa.
11 You will rejoice before Yahweh your God—you, your son, your daughter, your male servant, your female servant, the Levite who is within your city gates, and the foreigner, the fatherless, and the widow who are among you, at the place that Yahweh your God will choose for his sanctuary.
Shangilieni mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua kama makao ya Jina lake, ninyi, wana wenu na binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, Walawi walio katika miji yenu, na wageni, yatima na wajane waishio miongoni mwenu.
12 You will call to mind that you were a slave in Egypt; you must observe and do these statutes.
Kumbukeni kwamba mlikuwa watumwa kule Misri na mfuate amri hizi kwa uangalifu.
13 You must keep the Festival of Shelters for seven days after you have gathered in the harvest from your threshing floor and from your winepress.
Adhimisheni sikukuu ya vibanda kwa siku saba baada ya kukusanya mazao yenu ya nafaka na kukamua zabibu.
14 You will rejoice during your festival—you, your son, your daughter, your male servant, your female servant, the Levite, and the foreigner, and the fatherless and the widow who are within your gates.
Mfurahie sikukuu yenu, ninyi, wana wenu, binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, Walawi, wageni, yatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu.
15 For seven days you must observe the festival for Yahweh your God at the place that Yahweh will choose, because Yahweh your God will bless you in all your harvest and all the work of your hands, and you must be completely joyful.
Kwa siku saba mtaiadhimisha sikukuu ya Bwana Mungu wenu katika mahali atakapopachagua Bwana. Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki katika mavuno yenu na katika kazi zote za mikono yenu na furaha yenu itakamilika.
16 Three times in a year all your males must appear before Yahweh your God at the place that he will choose: at the Festival of Unleavened Bread, at the Festival of Weeks, and at the Festival of Shelters. No one will appear before Yahweh empty-handed;
Wanaume wenu wote lazima wajitokeze mara tatu kwa mwaka mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua: kwa ajili ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma, na Sikukuu ya Vibanda. Hakuna mtu atakayejitokeza mbele za Bwana mikono mitupu:
17 instead, every man will give as he is able, that you might know the blessing that Yahweh your God has given to you.
Kila mmoja wenu ni lazima alete zawadi kulingana na jinsi ambavyo Bwana Mungu wenu alivyowabariki.
18 You must make judges and officers within all your city gates that Yahweh your God is giving you; they will be taken from each of your tribes, and they must judge the people with righteous judgment.
Wateue waamuzi na maafisa kwa kila kabila lenu katika kila mji ambao Bwana Mungu wenu anawapa, nao watawaamua watu kwa usawa.
19 You must not take justice away by force; you must not show partiality nor take a bribe, for a bribe blinds the eyes of the wise and perverts the words of the righteous.
Msipotoshe haki wala msifanye upendeleo. Msikubali rushwa kwa sababu rushwa hupofusha macho ya wenye busara na kugeuza maneno ya wenye haki.
20 You must follow after justice, after justice alone, so that you may live and inherit the land that Yahweh your God is giving you.
Mfuate haki na haki peke yake, ili mweze kuishi na kuimiliki nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa.
21 You must not set up for yourselves an Asherah, any sort of pole, beside the altar of Yahweh your God that you will make for yourself.
Msisimamishe nguzo yoyote ya Ashera kando ya madhabahu mliyomjengea Bwana Mungu wenu,
22 Neither must you set up for yourself any sacred stone pillar, which Yahweh your God hates.
wala msisimamishe jiwe la kuabudu, kwa maana Bwana Mungu wenu anavichukia vitu hivi.

< Deuteronomy 16 >