< Deuteronomy 10 >

1 At that time Yahweh said to me, 'Carve two tablets of stone like the first, and come up to me on the mountain, and make an ark of wood.
Wakati ule Bwana aliniambia, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza uje kwangu juu mlimani. Pia utengeneze Sanduku la mbao.
2 I will write on the tablets the words that were on the first tablets that you broke, and you will put them in the ark.'
Nitaandika juu ya vibao maneno yaliyokuwa katika vile vibao vya kwanza, ambavyo ulivivunja. Kisha utaviweka ndani ya Sanduku.”
3 So I made an ark of acacia wood, and I carved two tablets of stone like the first, and I went up the mountain, having the two tablets in my hand.
Hivyo nikatengeneza Sanduku kwa mti wa mshita, nikachonga pia vibao vya mawe kama vile vya kwanza, kisha nikakwea mlimani nikiwa na vibao viwili mikononi mwangu.
4 He wrote on the tablets, like the first writing, the Ten Commandments which Yahweh had spoken to you on the mountain out of the middle of the fire on the day of the assembly; then Yahweh gave them to me.
Bwana akaandika juu ya hivi vibao kile alichokuwa amekiandika kabla, Amri Kumi alizokuwa amewatangazia juu mlimani, kutoka kwenye moto siku ile ya kusanyiko. Bwana akanikabidhi.
5 I turned and came down from the mountain, and put the tablets in the ark that I had made; there they are, as Yahweh commanded me.”
Kisha nikashuka kutoka mlimani na kuweka vibao ndani ya Sanduku nililokuwa nimelitengeneza, kama Bwana alivyoniagiza, navyo viko huko sasa.
6 (The people of Israel journeyed from Beeroth Bene Jaakan to Moserah. There Aaron died, and there he was buried; Eleazar, his son, served in the priest's office in his place.
(Waisraeli walisafiri kutoka visima vya Yaakani hadi Mosera. Huko Aroni alifariki na kuzikwa, naye Eleazari mwanawe akachukua nafasi yake kama kuhani.
7 From there they journeyed to Gudgodah, and from Gudgodah to Jotbathah, a land of streams of water.
Kutoka pale, walisafiri hadi Gudgoda wakaendelea mpaka Yotbatha, nchi yenye vijito vya maji.
8 At that time Yahweh chose the tribe of Levi to carry the ark of the covenant of Yahweh, to stand before Yahweh to serve him, and to bless people in his name, as today.
Wakati huo Bwana aliteua kabila la Lawi kulibeba Sanduku la Agano la Bwana, kusimama mbele za Bwana ili kutoa huduma, na kutangaza baraka kwa Jina lake, kama wanavyofanya mpaka leo.
9 Therefore Levi has no portion nor inheritance of land with his brothers; Yahweh is his inheritance, as Yahweh your God spoke to him.)
Hiyo ndiyo sababu ya Walawi kutokuwa na sehemu wala urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama Bwana Mungu wao alivyowaambia.)
10 “I stayed on the mountain as at the first time, forty days and forty nights. Yahweh listened to me that time also; Yahweh did not wish to destroy you.
Basi nilikaa mlimani kwa siku arobaini usiku na mchana, kama nilivyofanya mara ya kwanza, pia Bwana alinisikiliza hata wakati huu. Haikuwa nia yake kuwaangamiza.
11 Yahweh said to me, 'Arise, go before the people to lead them on their journey; they will go in and possess the land that I swore to their ancestors to give to them.'
Bwana akaniambia, “Nenda, ukawaongoze watu katika njia yao ili kwamba waweze kuingia na kuimiliki nchi ile niliyowaapia baba zao kuwapa.”
12 Now, Israel, what does Yahweh your God require of you, except to fear Yahweh your God, to walk in all his ways, to love him, and to worship Yahweh your God with all your heart and with all your soul,
Na sasa, ee Israeli, Bwana Mungu wako anataka nini kwako ila kumcha Bwana Mungu wako, kwenda katika njia zake, kumpenda na kumtumikia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote,
13 to keep the commandments of Yahweh, and his statutes, which I am commanding you today for your own good?
na kuyashika maagizo ya Bwana na amri zake ninazokupa leo kwa mafanikio yako mwenyewe?
14 Behold, to Yahweh your God belongs heaven and the heaven of heavens, the earth, with all that is in them.
Mbingu, hata mbingu za juu sana, dunia na kila kitu kilichomo ndani yake, ni mali ya Bwana Mungu wako.
15 Only Yahweh took pleasure in your fathers so as to love them, and he chose you, their descendants, after them, more than any of the other peoples, as he does today.
Hata hivyo Bwana alikuwa na shauku na baba zako, akawapenda na akawachagua ninyi, wazao wao, kuliko mataifa yote, kama ilivyo leo.
16 Therefore circumcise the foreskin of your heart, and be stubborn no longer.
Kwa hiyo tahirini mioyo yenu, na msiwe na shingo ngumu tena.
17 For Yahweh your God, he is God of gods and Lord of masters, the great God, the mighty one and the fearsome one, who favors no one and takes no bribes.
Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni Mungu wa miungu na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye uweza na wa kutisha, ambaye hana upendeleo na hapokei rushwa.
18 He executes justice for the fatherless and widow, and he shows love for the foreigner by giving him food and clothing.
Huwapigania yatima na wajane, humpenda mgeni, akimpa chakula na mavazi.
19 Therefore love the foreigner; for you were foreigners in the land of Egypt.
Nanyi wapendeni wageni, kwa kuwa ninyi wenyewe mlikuwa wageni huko Misri.
20 You will fear Yahweh your God; him will you worship. To him you must cling, and by his name will you swear.
Mche Bwana Mungu wako na umtumikie yeye. Shikamana naye kwa uthabiti na kuapa kwa jina lake.
21 He is your praise, and he is your God, who has done for you these great and fearsome things, which your eyes have seen.
Yeye ni sifa yako; yeye ni Mungu wako, ambaye alikutendea yale maajabu makubwa na ya kutisha uliyoyaona kwa macho yako mwenyewe.
22 Your fathers went down into Egypt as seventy persons; now Yahweh your God has made you as many as the stars of the heavens.
Baba zako walioshuka kwenda Misri jumla yao walikuwa sabini, na sasa Bwana Mungu wako amekufanya wengi kama nyota za angani.

< Deuteronomy 10 >