< Daniel 9 >

1 Darius was the son of Ahasuerus, a descendant of the Medes. It was Ahasuerus who had been made king over the realm of the Babylonians.
Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario mwana wa Ahasuero (mzaliwa wa Umedi), ambaye alifanywa mtawala juu ya ufalme wa Babeli,
2 Now in the first year of Darius' reign I, Daniel, was studying the books containing Yahweh's word, the word that had come to Jeremiah the prophet. I observed that there would be seventy years until Jerusalem's abandonment would end.
katika mwaka wa kwanza wa utawala wake, mimi Danieli nilielewa kutokana na Maandiko, kulingana na neno la Bwana alilopewa nabii Yeremia, kwamba ukiwa wa Yerusalemu ungetimizwa kwa miaka sabini.
3 I turned my face to the Lord God, to seek him with prayer and requests, with fasting, wearing sackcloth, and sitting in ashes.
Kwa hiyo nikamgeukia Bwana Mungu na kumsihi katika maombi na dua, katika kufunga, na kuvaa nguo ya gunia na kujipaka majivu.
4 I prayed to Yahweh my God, and I made confession of our sins. I said, “Please, Lord—you are the great and awesome God—you are the one who keeps the covenant and is faithful to love those who love you and keep your commandments.
Nikamwomba Bwana Mungu wangu na kutubu: “Ee Bwana, Mungu mkuu na unayetisha, anayeshika agano lake la upendo kwao wanaompenda na kutii maagizo yake,
5 We have sinned and have done what is wrong. We have acted wickedly and we have rebelled, turning aside from your commands and decrees.
tumetenda dhambi na kufanya mabaya. Tumekuwa waovu na tumeasi; tumegeuka mbali na maagizo yako na sheria zako.
6 We have not listened to your servants the prophets who spoke in your name to our kings, our leaders, our ancestors, and to all the people of the land.
Hatukuwasikiliza watumishi wako manabii, ambao kwa jina lako walisema na wafalme wetu, wakuu wetu, baba zetu, na watu wote wa nchi.
7 To you, Lord, belongs righteousness. To us today, however, belongs shame on our faces—for the people of Judah and those who live in Jerusalem, and to all Israel. This includes those who are near and those who are far away in all the lands where you scattered them. This is because of the great treachery that we committed against you.
“Bwana, wewe ni mwenye haki, lakini siku hii ya leo tumefunikwa na aibu: tukiwa wanaume wa Yuda, na watu wa Yerusalemu, na Israeli yote, wote walio karibu na walio mbali, katika nchi zote ulikotutawanya kwa sababu ya kukosa uaminifu kwako.
8 To us, Yahweh, belongs shame on our faces—to our kings, to our leaders, and to our ancestors—because we have sinned against you.
Ee Bwana, sisi na wafalme wetu, wakuu wetu na baba zetu tumefunikwa na aibu kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako.
9 To the Lord our God belong compassion and forgiveness, for we have rebelled against him.
Bwana Mungu wetu ni mwenye rehema na anayesamehe, hata ingawa tumefanya uasi dhidi yake.
10 We have not obeyed the voice of Yahweh our God by walking in his laws he gave us through his servants the prophets.
Hatukumtii Bwana Mungu wetu wala kuzishika sheria alizotupa kupitia kwa watumishi wake manabii.
11 All Israel has transgressed your law and turned aside, refusing to obey your voice. The curse and oath that are written in the law of Moses, the servant of God, have been poured out on us, for we have sinned against him.
Israeli yote imekosea sheria yako na kugeuka mbali, nao wamekataa kukutii. “Kwa hiyo laana na viapo vya hukumu vilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, mtumishi wa Mungu, vimemiminwa juu yetu, kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako.
12 Yahweh has confirmed the words that he spoke against us and against our rulers over us, by bringing on us a great disaster. For under the whole of heaven there has not been done anything that could compare with what has been done to Jerusalem.
Umetimiza maneno uliyosema dhidi yetu na dhidi ya watawala wetu, kwa kuleta maafa makubwa juu yetu. Chini ya mbingu yote kamwe hapajatendeka kitu kama kile kilichotendeka kwa Yerusalemu.
13 As it is written in the law of Moses, all this disaster has come on us, yet we have not begged for mercy from Yahweh our God by turning away from our iniquities and paying attention to your truth.
Kama vile ilivyoandikwa katika sheria ya Mose, misiba hii yote imekuja juu yetu, lakini hatujaomba fadhili kwa Bwana Mungu wetu kwa kugeuka kutoka dhambi zetu na kuwa wasikivu katika kweli yake.
14 Therefore Yahweh has kept the disaster ready and has brought it on us, for Yahweh our God is righteous in all the deeds he does, yet we have not obeyed his voice.
Bwana hakusita kuleta maafa juu yetu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mwenye haki katika kila afanyalo; lakini hata hivyo hatujamtii.
15 Now, Lord our God, you brought out your people from the land of Egypt with a mighty hand, and you have made a famous name for yourself, as in this present day. But still we sinned; we have done wicked things.
“Sasa, Ee Bwana Mungu wetu, ambaye uliwatoa watu wako Misri kwa mkono wenye nguvu, na ambaye umejifanyia Jina linalodumu mpaka leo, tumetenda dhambi, tumefanya mabaya.
16 Lord, because of all your righteous deeds, let your anger and your wrath turn away from your city Jerusalem, your holy mountain. Because of our sins, and because of the iniquities of our ancestors, Jerusalem and your people have become an object of scorn to all those around us.
Ee Bwana, wewe kwa kadiri ya matendo yako ya haki, ondoa hasira yako na ghadhabu yako juu ya Yerusalemu, mji wako, mlima wako mtakatifu. Dhambi zetu na maovu ya baba zetu yameifanya Yerusalemu na watu wako kitu cha kudharauliwa kwa wale wote wanaotuzunguka.
17 Now, our God, listen to the prayer of your servant and to his pleas for mercy; for your sake, Lord, make your face shine on your sanctuary that is desolate.
“Basi Mungu wetu, sasa sikia maombi na dua ya mtumishi wako. Ee Bwana, kwa ajili yako angalia kwa huruma ukiwa wa mahali pako patakatifu.
18 My God, open your ears and listen; open your eyes and see. We have been devastated; look at the city that is called by your name. We do not beg for your help because of our righteousness, but because of your great mercy.
Ee Mungu, tega sikio na ukasikie; fumbua macho yako ukaone ukiwa wa mji ule wenye Jina lako. Hatukutolei maombi yetu kwa sababu sisi tuna haki, bali kwa sababu ya rehema zako nyingi.
19 Lord, listen! Lord, forgive! Lord, pay attention and take action! For your own sake, do not delay, my God, for your city and your people are called by your name.”
Ee Bwana, sikiliza! Ee Bwana, samehe! Ee Bwana, sikia na ukatende! Kwa ajili yako, Ee Mungu wangu, usikawie, kwa sababu mji wako na watu wako wanaitwa kwa Jina lako.”
20 While I was speaking—praying and confessing my sin and the sin of my people Israel, and presenting my requests before Yahweh my God on behalf of God's holy mountain—
Basi, nilipokuwa bado nikinena na kuomba, nikiungama dhambi yangu na dhambi ya watu wangu Israeli, na nikifanya maombi yangu kwa Bwana Mungu wangu kwa ajili ya mlima wake mtakatifu,
21 while I was praying, the man Gabriel, whom I had seen in the vision at the first, flew down to me in rapid flight, at the time of the evening sacrifice.
wakati nilipokuwa bado katika maombi, Gabrieli, yule mtu niliyekuwa nimemwona katika maono hapo awali, alinijia kwa kasi karibu wakati wa kutoa dhabihu ya jioni.
22 He gave me understanding and said to me, “Daniel, I have now come out to give you insight and understanding.
Akanielimisha na kuniambia, “Danieli, sasa nimekuja kukupa akili na ufahamu.
23 When you began pleading for mercy, the order was given and I have come to tell you the answer, for you are greatly loved. Therefore consider this word and understand the revelation.
Mara ulipoanza kuomba, jibu lilitolewa, ambalo nimekuja kukupasha habari, kwa maana wewe unapendwa sana. Kwa hiyo, tafakari ujumbe huu na uelewe maono haya:
24 Seventy sevens are decreed for your people and your holy city to end the guilt and put an end to sin, to atone for wickedness, to bring everlasting righteousness, to carry out the vision and the prophecy, and to consecrate the most holy place.
“Majuma sabini yameamriwa kwa ajili ya watu wako na kwa ajili ya mji wako mtakatifu, ili kumaliza makosa, kukomesha dhambi, kufanya upatanisho kwa ajili ya uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri maono na unabii, na pia kumtia mafuta yeye aliye mtakatifu sana.
25 Know and understand that from the issuing of the order to restore and rebuild Jerusalem to the coming of the anointed one (who will be a leader), there will be seven sevens and sixty-two sevens. Jerusalem will be rebuilt with streets and a moat, despite the times of distress.
“Ujue na kuelewa hili: Tangu kutolewa kwa amri ya kuutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu mpaka kuja kwa Mpakwa mafuta, aliye mtawala, kutakuwako majuma saba na majuma sitini na mawili. Barabara zitajengwa tena pamoja na mahandaki, lakini katika wakati wa taabu.
26 After the sixty-two sevens, the anointed one will be destroyed and will have nothing. The army of a coming ruler will destroy the city and the holy place. Its end will come with a flood, and there will be war even to the end. Desolations have been decreed.
Baada ya majuma sitini na mawili, Mpakwa Mafuta atakatiliwa mbali, wala hatabaki na kitu. Watu wa mtawala atakayekuja watauharibu mji pamoja na mahali patakatifu. Mwisho utakuja kama mafuriko: Vita vitaendelea mpaka mwisho, nao ukiwa umeamriwa.
27 He will confirm a covenant with many for one seven. In the middle of the seven he will put an end to the sacrifice and the offering. On the wing of abominations will come someone who makes desolate. A full end and destruction are decreed to be poured out on the one who has made the desolation.”
Mtawala huyo atathibitisha agano na watu wengi kwa juma moja. Katikati ya juma hilo atakomesha dhabihu na sadaka. Mahali pa dhabihu katika Hekalu atasimamisha chukizo la uharibifu, hadi mwisho ulioamriwa utakapomiminwa juu yake yeye aletaye uharibifu.”

< Daniel 9 >