< Amos 1 >
1 These are the things concerning Israel that Amos, one of the shepherds in Tekoa, received in revelation. He received these things in the days of Uzziah king of Judah, and also in the days of Jeroboam son of Joash king of Israel, two years before the earthquake.
Maneno ya Amosi, mmoja wa wachunga wanyama wa Tekoa: yale aliyoyaona kuhusu Israeli miaka miwili kabla ya tetemeko la ardhi, wakati Uzia alikuwa mfalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yehoashi alikuwa mfalme wa Israeli.
2 He said, “Yahweh will roar from Zion; he will raise his voice from Jerusalem. The pastures of the shepherds will dry up; the top of Carmel will wither.”
Alisema: “Bwana ananguruma toka Sayuni, pia ananguruma kutoka Yerusalemu; malisho ya wachunga wanyama yanakauka, kilele cha Karmeli kinanyauka.”
3 This is what Yahweh says: “For three sins of Damascus, even for four, I will not turn away punishment, because they threshed Gilead with instruments of iron.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Dameski, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliipura Gileadi kwa vyombo vya chuma vyenye meno.
4 I will send a fire into the house of Hazael, and it will devour the fortresses of Ben Hadad.
Nitatuma moto juu ya nyumba ya Hazaeli ambao utateketeza ngome za Ben-Hadadi.
5 I will break the gate bars of Damascus and cut off the man who rules over the Valley of Aven, and also the man who holds the scepter in Beth Eden. The people of Aram will go in captivity to Kir,” says Yahweh.
Nitalivunja lango la Dameski; nitamwangamiza mfalme aliyeko katika Bonde la Aveni, na yeye ambaye anaishika fimbo ya utawala katika Beth-Edeni. Watu wote wa Aramu watakwenda uhamishoni huko Kiri,” asema Bwana.
6 This is what Yahweh says: “For three sins of Gaza, even for four, I will not turn away punishment, because they carried away captive a whole people, to hand them over to Edom.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu walichukua mateka jumuiya nzima na kuwauza kwa Edomu,
7 I will send fire on the walls of Gaza, and it will devour her fortresses.
nitatuma moto juu ya kuta za Gaza ambao utateketeza ngome zake.
8 I will cut off the man who lives in Ashdod and the man who holds the scepter from Ashkelon. I will turn my hand against Ekron, and the rest of the Philistines will perish,” says the Lord Yahweh.
Nitamwangamiza mfalme wa Ashdodi na yeye aishikaye fimbo ya utawala katika Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, hadi Mfilisti wa mwisho atakapokufa,” asema Bwana Mwenyezi.
9 This is what Yahweh says: “For three sins of Tyre, even for four, I will not turn away punishment, because they had delivered up a whole people to Edom, and they broke their covenant of brotherhood.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu ameuza jumuiya nzima ya mateka kwa Edomu, na kutokujali mapatano ya undugu,
10 I will send fire on the walls of Tyre, and it will devour her fortresses.”
Nitatuma moto kwenye kuta za Tiro ambao utateketeza ngome zake.”
11 This is what Yahweh says, “For three sins of Edom, even for four, I will not turn away punishment, because he pursued his brother with the sword and cast off all pity. His anger raged continually, and his wrath lasted forever.
Hili ndilo Bwana asemalo: “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu alimfuatia ndugu yake kwa upanga, alikataa kuonyesha huruma yoyote, kwa sababu hasira yake kali iliendelea kupanda wakati wote na ghadhabu iliwaka bila kuzuiliwa.
12 I will send fire on Teman, and it will devour the palaces of Bozrah.”
Nitatuma moto juu ya Temani ambao utateketeza ngome za Bosra.”
13 This is what Yahweh says, “For three sins of the people of Ammon, even for four, I will not turn away punishment, because they ripped open the pregnant women of Gilead, that they may enlarge their borders.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Amoni, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliwatumbua wanawake wajawazito wa Gileadi ili kuongeza mipaka yake.
14 I will light a fire in the walls of Rabbah, and it will devour the palaces, with a shout in the day of battle, with a tempest in the day of the whirlwind.
Nitatuma moto kwenye kuta za Raba ambao utateketeza ngome zake katikati ya vilio vya vita katika siku ya mapigano, katikati ya upepo mkali katika siku ya dhoruba.
15 Their king will go into captivity, he and his officials together,” says Yahweh.
Mfalme wake atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na maafisa wake,” asema Bwana.