< Amos 8 >

1 This is what the Lord Yahweh showed me. Look, a basket of summer fruit!
Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: kikapu cha matunda yaliyoiva.
2 He said, “What do you see, Amos?” I said, “A basket of summer fruit.” Then Yahweh said to me, “The end has come for my people Israel; I will spare them no longer.
Akaniuliza, “Amosi, unaona nini?” Nikajibu, “Kikapu chenye matunda yaliyoiva.” Ndipo Bwana akaniambia, “Wakati umewadia kwa watu wangu Israeli; sitawahurumia zaidi.”
3 The songs of the temple will become wailings in that day —this is the declaration of the Lord Yahweh— many dead bodies, they are thrown everywhere! Silence!”
Bwana Mwenyezi asema, “Katika siku ile, nyimbo katika Hekalu zitageuka kuwa maombolezo. Miili mingi, mingi sana: itatupwa kila mahali! Kimya!”
4 Listen to this, you who trample the needy and remove the poor of the land.
Lisikieni hili, ninyi ambao mnawagandamiza wahitaji, na kuwaonea maskini wa nchi,
5 They say, “When will the new moon be over, so we can sell grain again? When will the Sabbath day be over, so that we can sell wheat? We will make the measure small and increase the price, as we cheat with false scales.
mkisema, “Ni lini Mwezi Mwandamo utakapopita ili tupate kuuza nafaka, na Sabato itakwisha lini ili tuweze kuuza ngano?” Mkipunguza vipimo, na kuongeza bei, na kudanganya kwa mizani zisizo sawa,
6 This is so we can sell bad wheat, buy the poor with silver, and the needy for a pair of sandals.”
mkiwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu, na mkiuza hata takataka za ngano pamoja na ngano.
7 Yahweh has sworn by the pride of Jacob, “Surely I will never forget any of their actions.”
Bwana ameapa kwake mwenyewe, aliye Kiburi cha Yakobo: “Kamwe sitasahau chochote ambacho wamefanya.
8 Will not the land quake for this, and every one who lives in it mourn? All of it will rise up like the Nile River, and it will be tossed about and sink again, like the river of Egypt.
“Je, nchi haitatetemeka kwa ajili ya hili, nao wote waishio ndani mwake hawataomboleza? Nchi yote itainuka kama Naili; itapanda na kushuka kama mto wa Misri.
9 “It will come in that day —this is the declaration of the Lord Yahweh— that I will make the sun set at noon, and I will darken the earth at daylight.
“Katika siku ile,” asema Bwana Mwenyezi, “Nitalifanya jua litue alasiri na kuifanya dunia iwe giza wakati wa mchana mwangavu.
10 I will turn your festivals into mourning and all your songs into lamentation. I will make all of you wear sackcloth and have baldness on every head. I will make it like mourning for an only son, and a bitter day to its end.
Nitageuza sikukuu zenu za kidini kuwa maombolezo, na kuimba kwenu kote kuwe kilio. Nitawafanya ninyi nyote mvae nguo ya gunia na kunyoa nywele zenu. Nitaufanya wakati ule uwe kama wa kuombolezea mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.
11 Look, the days are coming —this is the declaration of the Lord Yahweh— when I will send a famine in the land, not a famine for bread, nor of thirst for water, but for hearing the words of Yahweh.
“Siku zinakuja,” asema Bwana Mwenyezi, “wakati nitakapotuma njaa katika nchi yote: si njaa ya chakula wala kiu ya maji, lakini njaa ya kusikia maneno ya Bwana.
12 They will stagger from sea to sea; they will run from the north to the east to seek the word of Yahweh, but they will not find it.
Wanaume watayumbayumba kutoka bahari hadi bahari na kutangatanga kutoka kaskazini mpaka mashariki, wakitafuta neno la Bwana, lakini hawatalipata.
13 In that day the beautiful virgins and the young men will faint from thirst.
“Katika siku ile “wasichana wazuri na vijana wanaume wenye nguvu watazimia kwa sababu ya kiu.
14 Those who swear by the sin of Samaria and say, 'As your god lives, Dan,' and, 'As the way to Beersheba exists'— they will fall and never rise again.”
Wale waapao kwa aibu ya Samaria, au kusema, ‘Hakika kama miungu yenu iishivyo, ee Dani,’ au ‘Hakika kama mungu wa Beer-Sheba aishivyo’: wataanguka, wala hawatasimama tena.”

< Amos 8 >