< 2 Samuel 2 >
1 After this David asked Yahweh and said, “Should I go up to one of the cities of Judah?” Yahweh replied to him, “Go up.” David said, “To which city should I go?” Yahweh replied, “To Hebron.”
Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
2 So David went up with his two wives, Ahinoam from Jezreel, and Abigail from Carmel, the widow of Nabal.
Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
3 David brought the men who were with him, who each brought his family, to the cities of Hebron, where they began to live.
Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
4 Then men from Judah came and anointed David king over the house of Judah. They told David, “The men of Jabesh Gilead have buried Saul.”
Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
5 So David sent messengers to the men of Jabesh Gilead and said to them, “You are blessed by Yahweh, since you have showed this loyalty to your master Saul and have buried him.
akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
6 Now may Yahweh show you covenantal loyalty and faithfulness. I also will show you this goodness because you have done this thing.
Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
7 Now then, let your hands be strong; be courageous for Saul your master is dead, and the house of Judah has anointed me king over them.”
Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
8 But Abner son of Ner, commander of Saul's army, took Ishbosheth son of Saul and brought him to Mahanaim.
Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
9 He made Ishbosheth king over Gilead, Asher, Jezreel, Ephraim, Benjamin, and over all Israel.
Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
10 Ishbosheth son of Saul, was forty years old when he began to reign over Israel, and he reigned two years. But the house of Judah followed David.
Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
11 The time that David was king in Hebron over the house of Judah was seven years and six months.
Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
12 Abner son of Ner, and the servants of Ishbosheth son of Saul, went out from Mahanaim to Gibeon.
Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
13 Joab son of Zeruiah and the servants of David went out and met them by the pool of Gibeon. There they sat down, one group on one side of the pool and the other on the other side.
Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
14 Abner said to Joab, “Let the young men arise and compete before us.” Then Joab said, “Let them arise.”
Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
15 Then the young men got up and gathered together, twelve for Benjamin and Ishbosheth son of Saul, and twelve from servants of David.
Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
16 Each man seized his opponent by the head and thrust his sword into the side of his opponent, and they fell down together. Therefore that place was called “Helkath Hazzurim,” or “Field of Swords,” which is in Gibeon.
Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
17 The battle was very severe that day and Abner and the men of Israel were defeated before the servants of David.
Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
18 The three sons of Zeruiah were there: Joab, and Abishai, and Asahel. Asahel was swift in his feet like a wild gazelle.
Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
19 Asahel closely pursued Abner and followed him without turning away in any direction.
Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
20 Abner looked behind him and said, “Is that you Asahel?” He answered, “It is I.”
Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
21 Abner said to him, “Turn aside to your right or to your left, and seize one of the young men and take his armor.” But Asahel would not turn aside.
Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
22 So Abner said again to Asahel, “Stop pursuing me. Why should I strike you to the ground? How then could I hold up my face to Joab, your brother?”
Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
23 But Asahel refused to turn aside, and so Abner stabbed him in the body with the blunt end of his spear, so that the spear came out the other side. Asahel fell down and died there. So it came about that anyone who arrived at the place where Asahel fell down and died, he stopped and stood still.
Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
24 But Joab and Abishai pursued Abner. When the sun was going down, they came to the hill of Ammah, which is near Giah by the road to the wilderness of Gibeon.
Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
25 The men of Benjamin gathered themselves together behind Abner and stood on the top of the hill.
Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
26 Then Abner called to Joab and said, “Must the sword devour forever? Do you not know it will be bitter in the end? How long will it be before you tell your men to stop pursuing their brothers?”
Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
27 Joab replied, “Just as God lives, if you had not said that, my soldiers would have pursued their brothers until the morning!”
Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
28 So Joab blew the trumpet, and all his men stopped and did not pursue Israel anymore, nor did they fight anymore.
Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
29 Abner and his men traveled all that night through the Arabah. They crossed the Jordan, marched all the next morning, and then reached Mahanaim.
Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
30 Joab returned from pursuing Abner. He assembled all his men, from whom were missing Asahel and nineteen of David's soldiers.
Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
31 But the men of David had killed 360 men of Benjamin with Abner.
Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
32 Then they took up Asahel and buried him in the tomb of his father, which was in Bethlehem. Joab and his men traveled all night, and the day dawned on them at Hebron.
Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.