< 2 Samuel 1 >
1 After the death of Saul, David returned from attacking the Amalekites and remained in Ziklag for two days.
Baada ya kifo cha Sauli, Daud alirudi kutoka kuwashambulia Waamaleki na akakaa Siklagi kwa siku mbili.
2 On the third day, a man came from Saul's camp with his clothes torn and with dirt on his head. When he came to David he lay facedown on the ground and prostrated himself.
Siku ya tatu, mtu mmoja alikuja kutoka kambi ya Sauli nguo zake zikiwa zimeraruliwa na akiwa na vumbi juu ya kichwa chake. Alipofika kwa Daudi alinamisha uso wake chini akajifanya yeye mwenyewe kuwa si kitu.
3 David said to him, “Where did you come from?” He answered, “I escaped from the camp of Israel.”
Daudi akamuliza, “Unatoka wapi?” Yeye akajibu, “Nimeponyoka kutoka kambi ya Israeli.”
4 David said to him, “Please tell me how things went.” He answered, “The people fled from the battle. Many have fallen and many are dead. Saul and Jonathan his son are also dead.”
Daudi akamwambia, “Tafadhari nieleze jinsi mambo yalivyokuwa.” Akajibu, “Watu walikimbia kutoka vitani. Wengi wameanguka, na wengi wao wameuawa. Sauli na Yonathani mwanawe pia wameuawa.”
5 David said to the young man, “How do you know that Saul and Jonathan his son are dead?”
Daudi akamwuliza kijana, “unajuaje kuwa Sauli na Yonathani mwanawe wameuawa?”
6 The young man replied, “By chance I happened to be on Mount Gilboa, and there Saul was leaning on his spear, and chariots and riders were about to catch up with him.
Yule kijana akajibu, “Kwa bahati nilikuwa juu ya Mlima Gilboa, na pale alikuwepo Sauli ameegemea mkuki wake, na magari ya farasi na waongozaji walikuwa karibu kumkamata.
7 Saul turned around and saw me and called out to me. I answered, 'Here I am.'
Sauli alipogeuka aliniona na akaniita. Nikajibu, 'Mimi hapa.'
8 He said to me, 'Who are you?' I answered him, 'I am an Amalekite.'
Akaniuliza, 'Wewe ni nani?' Nikamjibu, 'Mimi ni Mwamaleki,'
9 He said to me, 'Please stand over me and kill me, for great suffering has taken hold of me, but life is still in me.'
Akaniambia, Tafadhari simama juu yangu uniuwe, kwa kuwa shida kubwa imenipata, lakini uhai ungalimo ndani yangu.'
10 So I stood over him and killed him, because I knew that he would not live after he had fallen. Then I took the crown that was on his head and the band that was on his arm, and brought them here to you, my master.”
Hivyo nilisimama juu yake nikamuuwa, kwa maana nilijua kwamba asingeweza kuishi baada ya kuwa ameanguka. Ndipo nikachukuwa taji iliyokuwa juu ya kichwa chake na kikuku kilichokuwa mkononi mwake, na nimevileta hapa kwako, bwana wangu.”
11 Then David tore his clothes, and all the men with him did the same.
Kisha Daudi akararua mavazi yake, na watu wote waliokuwa pamoja naye wakafanya vilevile.
12 They mourned, wept, and fasted until evening for Saul, for Jonathan his son, for the people of Yahweh, and for the house of Israel because they had fallen by the sword.
Walilia, wakaomboleza na kufunga mpaka jioni kwa ajili ya Sauli, Yonathani mwanawe, watu wa Yahwe, na kwa ajili ya nyumba ya Israeli kwa maana wameanguka kwa upanga.
13 David said to the young man, “Where are you from?” He answered, “I am the son of a foreigner in the land, an Amalekite.”
Daudi akamwambia yule kijana, “Unatokea wapi?” Akajibu, mimi ni kijana wa mgeni Mwamaleki.”
14 David said to him, “Why were you not afraid to kill Yahweh's anointed king with your own hand?”
Daudi akamwambia, “Kwa nini haukuogopa kumwua mfalme, mtiwa mafuta wa Yahwe kwa mkono wako?”
15 David called one of the young men and said, “Go and kill him.” So that man went and struck him down, and the Amalekite died.
Daudi akamwita mmojawapo wa vijana na akamwambia, “Nenda ukamuue.” Hivyo kijana huyo akaenda na kumpiga hata ata chini, Mwamaleki akafa.
16 Then David said to the dead Amalekite, “Your blood is on your head because your own mouth has testified against you and said, 'I have killed Yahweh's anointed king.'”
Ndipo Daudi akamwambia Mwamaleke aliyekufa, “Damu yako iwe juu ya kichwa chako kwa kuwa kinywa chako kimeshuhudia dhidi yako kusema, Nimemuua mfalme mtiwa mafuta wa Yahwe.
17 Then David sung this funeral song about Saul and Jonathan his son.
Ndipo Daudi akaimba wimbo wa maombolezo juu ya Sauli na Yonathani mwanawe.
18 He commanded the people to teach this Song of the Bow to the sons of Judah, which has been written in the Book of Jashar.
Akawaamuru watu kuufundisha wimbo wa Bow kwa wana wa Yuda, ambao umeandikwa katika Kitabu cha Yashari.
19 “Your glory, Israel, is dead, killed on your high places! How the mighty have fallen!
“Utukufu wako, Israel, umeondolewa, umeondolewa juu ya mahali pako pa juu! Jinsi mwenye nguvu alivyoanguka!
20 Do not tell it in Gath, do not proclaim it in the streets of Ashkelon, so that the daughters of the Philistines may not rejoice, so that the daughters of the uncircumcised may not celebrate.
Msiiseme katika Gathi, msiitangaze katika mitaa ya Ashikeloni, ili binti za wafilisti wasifurahi, ili binti za wasiotailiwa wasisherehekee.
21 Mountains of Gilboa, let there not be dew or rain on you, nor fields giving grain for offerings, for there the shield of the mighty was defiled. The shield of Saul is no longer anointed with oil.
Milima ya Gilboa, kusiwe na umande au mvua juu yenu. wala mashamba yasitoe nafaka kwa ajili ya sadaka, kwa maana hapo ngao ya mwenye nguvu imeharibiwa. Ngao ya Sauli haiwezi tena kutiwa mafuta.
22 From the blood of those who have been killed, from the bodies of the mighty, the bow of Jonathan did not turn back, and the sword of Saul did not return empty.
Kutoka katika damu ya waliouawa, kutoka katika miili ya wenye nguvu, upinde wa Yonathani haukurudi nyuma, na upanga wa Sauli haukurudi patupu.
23 Saul and Jonathan were loved and gracious in life, and in their death they were not separated. They were swifter than eagles, they were stronger than lions.
Sauli na Yonathani walikuwa wakipendwa na walikuwa wenye neema maishani, hata wakati wa mauti yao walikuwa pamoja. Walikuwa na kasi kuliko tai, walikuwa na nguvu kuliko simba.
24 You daughters of Israel, weep over Saul, who clothed you in scarlet as well as jewels, and who put ornaments of gold on your clothing.
Enyi binti wa Israeli lieni juu ya Sauli, aliyewavika mavazi ya thamani pamoja na vito vya thamani, na aliyetia mapambo ya dhahabu katika mavazi yenu.
25 How the mighty have fallen in the midst of the battle! Jonathan is killed on your high places.
Jinsi wenye nguvu walivyoanguka vitani! Yonathani ameuawa juu ya mahali pako pa juu.
26 I am distressed for you, my brother Jonathan. You were very dear to me. Your love to me was wonderful, exceeding the love of women.
Nimesikitishwa sana kwa ajili yako, Yonathani ndugu yangu. Ulikuwa mpendwa wangu sana. Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, ukipita upendo wa wanawake.
27 How the mighty have fallen, and the weapons of war perished!”
Jinsi wenye nguvu walivyoanguka na silaha za vita zimeteketea!”