< 2 Kings 24 >
1 In Jehoiakim's days, Nebuchadnezzar king of Babylon attacked Judah; Jehoiakim became his servant for three years. Then Jehoiakim turned back and rebelled against Nebuchadnezzar.
Wakati wa utawala wa Yehoyakimu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliishambulia nchi, naye Yehoyakimu akawa mtumwa wake kwa miaka mitatu. Lakini hatimaye akabadili mawazo yake na kuasi dhidi ya Nebukadneza.
2 Yahweh sent against Jehoiakim bands of Chaldeans, Arameans, Moabites, and Ammonites; he sent them against Judah to destroy it. This was in conformity with the word of Yahweh that had been spoken through his servants the prophets.
Bwana akatuma wavamiaji wa Wakaldayo, Waaramu, Wamoabu na Waamoni ili kumshambulia. Aliwatuma kuiangamiza Yuda sawasawa na neno la Bwana lililosemwa na watumishi wake manabii.
3 It was certainly at the mouth of Yahweh that this came on Judah, to remove them out of his sight, because of the sins of Manasseh, all that he did,
Hakika mambo haya yalitokea Yuda kulingana na agizo la Bwana, ili kuwaondoa kutoka machoni pake kwa sababu ya dhambi za Manase na yote aliyoyafanya,
4 and also because of the innocent blood that he shed, for he filled Jerusalem with innocent blood. Yahweh was not willing to pardon that.
ikiwa ni pamoja na kumwaga damu isiyo na hatia. Kwa kuwa aliijaza Yerusalemu kwa damu isiyo na hatia, naye Bwana hakuwa radhi kusamehe.
5 As for the other matters concerning Jehoiakim, and all that he did, are they not written in the book of the events of the kings of Judah?
Matukio mengine ya utawala wa Yehoyakimu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
6 Jehoiakim slept with his ancestors, and Jehoiachin his son became king in his place.
Yehoyakimu akalala pamoja na baba zake. Naye Yehoyakini mwanawe akawa mfalme baada yake.
7 The king of Egypt did not attack any more out of his land, because the king of Babylon had conquered all the lands that had been controlled by the king of Egypt, from the brook of Egypt to the Euphrates River.
Mfalme wa Misri hakutoka tena katika nchi yake, kwa sababu mfalme wa Babeli alikuwa ameitwaa himaya yake yote, kuanzia Kijito cha Misri hadi Mto Frati.
8 Jehoiachin was eighteen years old when he began to reign; he reigned in Jerusalem three months. His mother's name was Nehushta; she was the daughter of Elnathan of Jerusalem.
Yehoyakini alikuwa na miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Nehushta binti Elnathani kutoka Yerusalemu.
9 He did what was evil in the sight of Yahweh; he did all that his father had done.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
10 At that time the army of Nebuchadnezzar king of Babylon attacked Jerusalem and besieged the city.
Wakati huo, maafisa wa Nebukadneza mfalme wa Babeli walikuja ili kuishambulia Yerusalemu, nao wakaizunguka kwa jeshi.
11 Nebuchadnezzar king of Babylon came to the city while his soldiers were besieging it,
Nebukadneza mwenyewe akaupandia mji wakati maafisa wake walipokuwa wameuzunguka kwa jeshi.
12 and Jehoiachin the king of Judah went out to the king of Babylon, he, his mother, his servants, his princes, and his officers. The king of Babylon captured him in the eighth year of his own reign.
Yehoyakini mfalme wa Yuda, mama yake, wahudumu wake, wakuu na maafisa wake wote wakajisalimisha kwa Nebukadneza. Katika mwaka wa nane wa utawala wa mfalme wa Babeli, akamchukua Yehoyakini kuwa mfungwa.
13 Nebuchadnezzar took out from there all the valuable things in the house of Yahweh, and those in the king's palace. He cut into pieces all the golden objects that Solomon king of Israel had made in the temple of Yahweh, as Yahweh had said would happen.
Kama vile Bwana alivyokuwa amesema, Nebukadneza akaondoa hazina yote kutoka Hekalu la Bwana na kutoka jumba la mfalme, akavichukua vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amevitengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana.
14 He took into exile all Jerusalem, all the leaders, and all the fighting men, ten thousand captives, and all the craftsmen and the smiths. No one was left except the poorest people in the land.
Akawachukua watu wa Yerusalemu wote kwenda uhamishoni: yaani maafisa wote na mashujaa, watu wenye ustadi na ufundi, jumla yao watu elfu kumi. Watu maskini sana ndio tu waliobaki katika nchi.
15 Nebuchadnezzar took Jehoiachin into exile at Babylon, as well as the king's mother, wives, officers, and the chief men of the land. He took them into exile from Jerusalem to Babylon.
Nebukadneza akamchukua mateka Yehoyakini hadi Babeli. Pia akawachukua utumwani kutoka Yerusalemu hadi Babeli mama yake mfalme, wake zake, maafisa wake, na viongozi wote wa nchi.
16 All the fighting men, seven thousand in number, and one thousand craftsmen and blacksmiths, all of them fit for fighting—the king of Babylon brought these men into exile at Babylon.
Mfalme wa Babeli pia akawahamishia Babeli mashujaa elfu saba, wenye nguvu na wanaofaa kupigana vita, na watu wenye ustadi na mafundi elfu moja.
17 The king of Babylon made Mattaniah, Jehoiachin's father's brother, king in his place, and changed his name to Zedekiah.
Akamfanya Matania, ndugu wa baba yake Yehoyakini, kuwa mfalme mahali pake, na akalibadilisha jina lake kuwa Sedekia.
18 Zedekiah was twenty-one years old when he began to reign; he reigned eleven years in Jerusalem. His mother's name was Hamutal; she was the daughter of Jeremiah from Libnah.
Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
19 He did what was evil in the sight of Yahweh; he did all that Jehoiakim had done.
Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
20 Through Yahweh's anger, all these events happened in Jerusalem and Judah, until he drove them out of his presence. Then Zedekiah rebelled against the king of Babylon.
Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.