< 2 Kings 14 >

1 In the second year of Jehoash son of Jehoahaz, king of Israel, Amaziah son of Joash, king of Judah, began to reign.
Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 He was twenty-five years old when he began to reign; he reigned twenty-nine years in Jerusalem. His mother's name was Jehoaddan, of Jerusalem.
Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani, kutoka Yerusalemu.
3 He did what was right in the eyes of Yahweh, yet not like David his father. He did everything that Joash, his father, had done.
Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kama Daudi baba yake alivyokuwa amefanya. Katika kila kitu alifuata mfano wa Yoashi baba yake.
4 But the high places were not taken away. The people still sacrificed and burned incense at the high places.
Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
5 It came about that as soon as his rule was well established, he killed the servants who had murdered his father, the king.
Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
6 Yet he did not put the sons of the murderers to death; instead, he acted according to what was written in the Book of the Law Moses, as Yahweh had commanded, saying, “The fathers must not be put to death for their children, neither must the children be put to death for their parents. Instead, every person must be put to death for his own sin.”
Hata hivyo, hakuwaua wana wa wale wauaji, sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose ambako Bwana aliamuru, “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
7 He killed ten thousand soldiers of Edom in the Valley of Salt; he also took Sela in war and called it Joktheel, which is what it is called to this day.
Ndiye aliwashinda Waedomu elfu kumi katika Bonde la Chumvi, na akauteka Sela katika vita, naye akauita Yoktheeli, jina ambalo mji huo unalo hadi leo.
8 Then Amaziah sent messengers to Jehoash son of Jehoahaz son of Jehu king of Israel, saying, “Come, let us meet each other face to face in battle.”
Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi, mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli, akisema, “Njoo, tuonane uso kwa uso.”
9 But Jehoash the king of Israel sent messengers back to Amaziah king of Judah, saying, “A thistle that was in Lebanon sent a message to a cedar in Lebanon, saying, 'Give your daughter to my son for a wife,' but a wild beast in Lebanon walked by and trampled down the thistle.
Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda: “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
10 You have indeed attacked Edom, and your heart has lifted you up. Take pride in your victory, but stay at home, for why should you cause yourself trouble and fall, both you and Judah with you?”
Hakika umeishinda Edomu, na sasa unajivuna. Jisifu katika ushindi wako, lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini unachokoza na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
11 But Amaziah would not listen. So Jehoash king of Israel attacked and he and Amaziah king of Judah met each other face to face at Beth Shemesh, which belongs to Judah.
Hata hivyo, Amazia hakusikia, hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakutana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
12 Judah was defeated by Israel, and every man fled home.
Yuda ikashindwa na Israeli, na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
13 Jehoash king of Israel, captured Amaziah, king of Judah son of Jehoash son of Ahaziah, at Beth Shemesh. He came to Jerusalem and tore down the wall of Jerusalem from the Ephraim Gate to the Corner Gate, four hundred cubits in distance.
Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akaenda Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
14 He took all the gold and silver, all the objects that were found in the house of Yahweh, and the valuable things in the king's palace, with hostages also, and returned to Samaria.
Akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina zote za jumba la mfalme. Akachukua pia mateka na akarudi Samaria.
15 As for the other matters concerning Jehoash, all that he did, his power, and how he fought with Amaziah king of Judah, are they not written in the book of the events of the kings of Israel?
Matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita vyake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
16 Then Jehoash slept with his ancestors and was buried in Samaria with the kings of Israel, and Jeroboam, his son, became king in his place.
Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli, naye Yeroboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
17 Amaziah son of Joash, king of Judah, lived fifteen years after the death of Jehoash son of Jehoahaz, king of Israel.
Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
18 As for the other matters concerning Amaziah, are they not written in the book of the events of the kings of Judah?
Matukio mengine ya utawala wa Amazia, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
19 They made a conspiracy against Amaziah in Jerusalem, and he fled to Lachish. He fled to Lachish, but they sent men after him to Lachish and killed him there.
Wakafanya shauri baya dhidi ya Amazia huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi, nao wakamuulia huko.
20 They brought him back on horses, and he was buried with his ancestors in the city of David.
Akarudishwa kwa farasi na akazikwa huko Yerusalemu pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi.
21 All the people of Judah took Azariah, who was sixteen years old, and made him king in place of his father Amaziah.
Kisha watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, na kumfanya mfalme mahali pa baba yake Amazia.
22 It was Azariah who rebuilt Elath and restored it to Judah, after King Amaziah slept with his ancestors.
Ndiye aliijenga tena Elathi na kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
23 In the fifteenth year of Amaziah son of Joash king of Judah, Jeroboam son of Jehoash king of Israel began to reign in Samaria; he reigned forty-one years.
Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala huko Samaria, naye akatawala kwa miaka arobaini na mmoja.
24 He did what was evil in the sight of Yahweh. He did not depart from any of the sins of Jeroboam son of Nebat, who had caused Israel to sin.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi hata moja ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
25 He restored the border of Israel from Lebo Hamath to the Sea of the Arabah, following the commands of the word of Yahweh, the God of Israel, which he had spoken through his servant Jonah son of Amittai, the prophet, who was from Gath Hepher.
Ndiye alirudishia mipaka ya Israeli kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bahari ya Araba, sawasawa na neno la Bwana, Mungu wa Israeli, lililosemwa kupitia mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gath-Heferi.
26 For Yahweh saw the suffering of Israel, that it was very bitter for everyone, both slave and free, and that there was no rescuer for Israel.
Bwana alikuwa ameona jinsi kila mmoja katika Israeli, awe mtumwa au aliye huru, alivyoteseka kwa uchungu; hapakuwepo na yeyote wa kuwasaidia.
27 So Yahweh said that he would not blot out the name of Israel under heaven; instead, he saved them by the hand of Jeroboam son of Jehoash.
Kwa kuwa Bwana alikuwa hajasema kuwa atafuta jina la Israeli chini ya mbingu, akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.
28 As for the other matters concerning Jeroboam, all that he did, his power, how he waged war and recovered Damascus and Hamath, which had belonged to Judah, for Israel, are they not written in the book of the events of the kings of Israel?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, yote aliyoyafanya na mafanikio yake ya kijeshi, ikiwa ni pamoja na jinsi alivyorudisha Dameski na Hamathi kwa Israeli, ambayo ilikuwa mali ya Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
29 Jeroboam slept with his ancestors, with the kings of Israel, and Zechariah his son became king in his place.
Yeroboamu akalala pamoja na baba zake, wafalme wa Israeli. Naye Zekaria mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Kings 14 >