< 2 Chronicles 24 >
1 Joash was seven years old when he began to reign; he reigned for forty years in Jerusalem. His mother's name was Zibiah, of Beersheba.
Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala; akatawala kwa mika arobaini katika Yerusalemu. Jina la mama yake aliitwa Sibia wa Beer-sheba.
2 Joash did what was right in the eyes of Yahweh all the days of Jehoiada, the priest.
Yoashi alifanya yaliyo mema katika macho ya Yahwe siku zote za Yehoyada, yule kuhani.
3 Jehoiada took for him two wives, and he became the father of sons and daughters.
Yehoyada akajichukulia wake wawili kwa ajili yake, na akawa baba wa wana na mabinti.
4 It came about after this, that Joash decided to restore the house of Yahweh.
Ikawa baada ya haya, kwamba Yoashi aliamua kuitengeneza nyumba ya Yahwe.
5 He gathered together the priests and the Levites, and he said to them, “Go out every year to the cities of Judah and gather from all Israel money to repair the house of your God. Make sure that you start right away.” The Levites did nothing at first.
Akawakusanya pamoja makuhani na Walawi, na kusema kwao, “Nendeni nje kila mwaka kwenye miji ya Yuda na kukusanya fedha kutoka Israeli yote kwa ajili ya kuikarabati nyumba ya Mungu wenu. Hakikisheni kwamba mnaanza haraka.” Walawi hawakufanya kitu kwanza.
6 So the king called for Jehoiada the high priest and said to him, “Why have you not required the Levites to bring in from Judah and Jerusalem the tax levied by Moses the servant of Yahweh and by the assembly of Israel for the tent of the covenant decrees?”
Kwa hiyo mfalme akamuita Yehoyada, yule kuhani, na kumwambia, “Kwa nini hukuwaagiza Walawi kuleta kutoka Yud na Yerusalemu kodo iliyoagizwa na Musa mtumishi wa Yahwe na kusanyiko la Israeli, kwa ajili ya amri za hema ya agano?”
7 For the sons of Athaliah, that wicked woman, had broken up the house of God and had given all the holy things of the house of Yahweh to the Baals.
Kwa maana wana wa Athalia, yule mwanamke muovu, walikuwa wameivunja nyumba ya Mungu na kuwapa Mabaali vitu vyote vitakatifu vya nyumba ya Yahwe.
8 So the king commanded, and they made a chest and placed it outside at the entrance to the house of Yahweh.
Kwa hiyo mfalme aliamuru, na wakatengeneza kasha na kulileta nje kwenye lango kwenye nyumba ya Yahwe.
9 Then they made a proclamation through Judah and Jerusalem, for the people to bring in for Yahweh the tax that Moses the servant of God levied on Israel in the wilderness.
Kisha wakafanya tangazo katika Yuda na Yerusalemu, kwa ajili ya watu kuleta kwa Yahwe kodi aliyoiagiza Musa mtumishi wa Mungu juu ya Israeli jangwani.
10 All the leaders and all the people rejoiced and brought money in and put it into the chest until they finished filling it.
Viongozi wote na watu wote wakafurahia na wakaleta fedha na kuiweka kwenye kasha hadi walipomaliza kulijaza.
11 It happened that whenever the chest was brought to the king's officials by the hand of the Levites, and whenever they saw that there was much money in it, the king's scribe and the high priest's official would come, empty the chest, and take it and carry it back to its place. They did this day after day, gathering large amounts of money.
Ikatokea kwamba kila lilipoletwa kasha kwa mikono ya Walawi kwa wakuu wa mfalme, na kila walipoona kwamba kulikuwa na fedha nyingi sana ndani yake, waandishi wa mfalme na mkuu wa kuhani mkuu walikuja, kulihamishia fedha kasha, na kulirudisha sehemu yake. Walifanya hivyo siku baada siku, wakikusanya kiasi kikubwa cha fedha.
12 The king and Jehoiada gave the money to those who did the work of serving in the house of Yahweh. These men hired stonemasons and carpenters to restore the house of Yahweh, and also those who worked in iron and bronze.
Mfalme na Yehoyada akawapa zile fedha wale waliofanya kazi ya kuhudumu katika nyumba ya Yahwe, Watu hawa waliwaajiri waashi na maseremala ili waijenge nyumba ya Yahwe, na pia wale waliofanya kazi katika chuma na shaba.
13 So the workmen labored, and the work of repairing went forward in their hands; they set up the house of God in its original design and strengthened it.
Kwa hiyo wafanya kazi wakafanya kazi, na kazi ya kukarabati ikasonga mbele mikononi mwao; waakaisimamisha nyumba ya Mungu katika hali yake halisi na kuiimarisha.
14 When they finished, they brought the rest of the money to the king and Jehoiada. This money was used to make furnishings for the house of Yahweh, utensils with which to serve and make offerings—spoons and utensils of gold and silver. They offered burnt offerings in the house of Yahweh continually for all the days of Jehoiada.
Walipomaliza, wakaleta fedha zilizobaki kwa mfalme na Yehoyada. Fedha hizo zilitumika kutengenezea samani kwa ajili ya nyumba ya Yahwe, vyombo vya huduma na kutolea dhabihu—vijiko na vyombo vya dhahabu na fedha. Wakatoa sadaka za kuteketezwa bila kukomaa katika nyumba ya Yahwe kwa siku zote za Yehoyada.
15 Jehoiada grew old and was full of days, and then he died; he was 130 years old when he died.
Yehoyada akazeeka na alaaikuwa amejaa siku, na kisha akafa; alikuwa na umri wa mika 130 alipokufa.
16 They buried him in the city of David among the kings, because he had done good in Israel, toward God, and to God's house.
Wakamzika katika aamji wa Daudi miongoni mwa wafalme, kwa sababu alikuwa amefanya mema katika Israeli, kwa Mungu, na kwa ajili ya nyumba ya Mungu,
17 Now after the death of Jehoiada, the leaders of Judah came and did honor to the king. Then the king listened to them.
Sasa baada ya kifo cha Yehoyada, kiongozi wa Yuda akaja na kutoa heshima kwa mfalme. Kisha mfalme akawasikiliza.
18 They forsook the house of Yahweh, the God of their ancestors, and worshiped the Asherah gods and the idols. God's anger came on Judah and Jerusalem for this wrongdoing of theirs.
Wakaiacha nyumba ya Yahwe, Mungu wa babu zao, na kuwaabudu miungu na maashera na sanamu. Ghadhabu ya Mungu ikaja juu ya Yuda na Yerusalemu kwa sababau ya hili kosa lao.
19 Yet he sent prophets to them to bring them again to himself, Yahweh; the prophets testified against the people, but they refused to listen.
Bado akatuma manabii kwao ili kuwaleta tena kwake, Yahwe, manabii wakatangaza juu ya watu, lakini walipuuza kusikiliza.
20 The Spirit of God came on Zechariah son of Jehoiada, the priest; Zechariah stood above the people and said to them, “God says this: Why do you transgress the commandments of Yahweh, so that you cannot prosper? Since you have forsaken Yahweh, he has also forsaken you.”
Roho wa Mungu akaja juu ya Zekaria mwana wa Yehoyada, yule kuhani; Zekaria akasimama juu ya watu na kusema kwao, “Mungu anasema hivi: Kwa nini mnazivunja amri za Yahwe, ili kwamba msifanikiwe? Kwa kuwa mmemsahau Yahwe, pia amewasahau ninyi.”
21 But they plotted against him; at the king's command, they stoned him with stones in the courtyard of the house of Yahweh.
Lakini wakapanga njama dhidi yake; kwa amri ya mfalme, wakampiga kwa mawe katika uwanja wa nyumba ya Yahwe.
22 In this manner, Joash, the king, ignored the kindness that Jehoiada, Zechariah's father, had done to him. Instead, he killed Jehoiada's son. When Zechariah was dying, he said, “May Yahweh see this and call you to account.”
Katika namna hii hii, Yoashi, yule mfalme, akapuuza ukarimu ambao Yehoyada, baba yake Zekaria, alikuwa amemfanyia.
23 It came about at the end of the year, that the army of Aram came up against Joash. They came to Judah and Jerusalem; they killed all the leaders of the people and sent all the plunder from them to the king of Damascus.
Ikawa karibu mwisho wa mwaka, kwamba jeshi la Aramu wakaja juu yake Yoashi. Wakaja Yuda na Yerusalemu; wakawaua viongozi wote wa watu na kupeleka nyara zote kutoka kwao kwa mfalme wa Dameski.
24 Although the army of the Arameans had come with only a few soldiers, Yahweh gave them victory over a very great army, because Judah had forsaken Yahweh, the God of their ancestors. In this way the Arameans brought judgment on Joash.
Jeshsi la Waaramu walikuwa wamekuja na jeshi dogo, lakini Yahwe akawapa ushindi juu ya jeshi kubwa, kwa sababu Yuda alikuwa amemsahau Yahwe, Mungu wa babu zao. Katika namna hii Waaramu wakaleta hukumu juu ya Yoashi.
25 By the time that the Arameans had gone, Joash had been severely wounded. His own servants plotted against him because of the murder of the sons of Jehoiada, the priest. They killed him in his bed, and he died; they buried him in the city of David, but not in the tombs of the kings.
Katika muda ambao Waaramu walikuwa wameondoka, Yoashi alikuwa amejeruhiwa vikali. Watumishi wake wakapanga njama dhidi yake kwa sababu ya mauaji ya wana wa Yehoyada, yule kuhani. Wakamuua katika kitanda chake, na akafa; wakamzika katika mji wa Daudi, lakini siyo katika makaburi ya wafalme.
26 These were the persons who plotted against him: Zabad son of Shimeath, an Ammonite woman; and Jehozabad son of Shimrith, a Moabite woman.
Hawa walikuwa watu waliopanaga njama dhidi yake: Zabadi mwana wa Shimeathi, Mwamoni; na Yehozabadi mwana wa Shimrithi, Mwanamke Mmoabu.
27 Now the accounts about his sons, the important prophecies that were spoken about him, and the rebuilding of the house of God, see, they are written in the commentary on the book of the kings. Amaziah his son became king in his place.
Sasa matukio kuhusu wanaye, unabii muhimu uliokuwa umesemwa kumhusu yeye, na kujengwa tena kwa nyumba ya Mungu, ona, yameandikwa katika Kamusi ya kitabu cha wafalme. Amazia mwanaye, akawa mfalme katika nafasi yake.