< 2 Chronicles 10 >
1 Rehoboam went to Shechem, for all Israel was coming to Shechem to make him king.
Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
2 When Jeroboam the son of Nebat heard this (for he was in Egypt, where he had fled from King Solomon), he returned from Egypt.
Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri.
3 So they sent and called him, and Jeroboam and all Israel came; they spoke to Rehoboam and said,
Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
4 “Your father made our yoke difficult. Now therefore, make your father's hard work easier, and lighten the heavy yoke that he put on us, and we will serve you.”
“Baba yako aliweka nira nzito, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
5 Rehoboam said to them, “Come again to me after three days.” So the people left.
Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
6 King Rehoboam consulted with the old men who had stood before Solomon his father while he was alive; he said, “How would you advise me to bring an answer to these people?”
Kisha Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee ambao walimtumikia Solomoni baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri nini katika kuwajibu watu hawa?”
7 They spoke to him and said, “If you are good to this people and please them, and say good words to them, then they will always be your servants.”
Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
8 But Rehoboam ignored the advice of the old men that they had given him, and consulted with the young men who had grown up with him, who stood before him.
Lakini Rehoboamu akakataa shauri alilopewa na wazee na akataka ushauri kwa vijana wanaume rika lake waliokuwa wakimtumikia.
9 He said to them, “What advice do you give me, so that we may answer the people who spoke to me and said, 'Lighten the yoke that your father put on us'?”
Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu?’”
10 The young men who had grown up with Rehoboam spoke to him, saying, “This is how you should speak to the people who told you that your father Solomon made their yoke heavy, but that you must make it lighter. This is what you should say to them, 'My little finger is thicker than my father's waist.
Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Waambie watu hawa waliokuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi,’ kuwa, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
11 So now, although my father burdened you with a heavy yoke, I will add to your yoke. My father punished you with whips, but I will punish you with scorpions.'”
Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi; mimi nitawachapa kwa nge.’”
12 So Jeroboam and all the people came to Rehoboam on the third day, as the king said, “Come back to me on the third day.”
Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
13 Rehoboam spoke to them harshly, ignoring the advice of the old men.
Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,
14 He spoke to them following the advice of the young men, saying, “My father made your yoke heavy, but I will add to it. My father punished you with whips, but I will punish you with scorpions.”
akafuata shauri la vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.”
15 So the king did not listen to the people, for it was a turn in events brought about by God, that Yahweh might carry out his word that Ahijah the Shilonite had spoken to Jeroboam son of Nebat.
Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Mungu ili kutimiza neno ambalo Bwana alikuwa amenena kwa Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshiloni.
16 When all Israel saw that the king did not listen to them, the people answered him and said, “What share do we have in David? We have no inheritance in the son of Jesse! Each of you should go back to his tent, Israel. Now see to your own house, David.” So all Israel returned to their tents.
Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli, angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
17 But as for the people of Israel who lived in the cities of Judah, Rehoboam reigned over them.
Lakini kwa habari ya Waisraeli waliokuwa wakiishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
18 Then King Rehoboam sent Adoniram, who was over the forced laborers, but the people of Israel stoned him to death with stones. King Rehoboam fled quickly in his chariot to Jerusalem.
Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoniramu aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake na kutorokea Yerusalemu.
19 So Israel has been in rebellion against the house of David to this day.
Hivyo Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.