< 1 Samuel 9 >
1 There was a man from Benjamin, a man of influence. His name was Kish son of Abiel son of Zeror son of Bekorath son of Aphiah, the son of a Benjamite.
Basi kulikuwa na mtu mmoja kutoka Benyamini, mtu mashuhuri. Jina lake aliitwa Kishi mwana wa Abieli, mwana wa Zerori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia, mwana wa Mbenyamini.
2 He had a son named Saul, a handsome young man. There was no man among the people of Israel who was a more handsome person than he. From his shoulders upward he was taller than any of the people.
Huyu alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Sauli, kijana mzuri wa uso. Hapakuwapo mwanaume mzuri wa uso kuliko huyu miongoni mwa watu wote wa Israeli. Kutoka mabegani kwenda juu alikuwa mrefu kuliko watu wengine.
3 Now the donkeys of Kish, Saul's father, were lost. So Kish said to Saul his son, “Take one of the servants with you; arise and go look for the donkeys.”
Na punda wa Kishi, baba yake na Sauli walipotea. hivyo Kishi akamwambia Sauli mwanawe, “Mchukue mmoja wa watumishi; uamke uende kuwatafuta punda,”
4 So Saul passed through the hill country of Ephraim and went through the land of Shalishah, but they did not find them. Then they passed through the land of Shaalim, but they were not there. Then he passed through the land of the Benjamites, but they did not find them.
Sauli akapita katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu na akaenda akapita katika nchi ya Shalisha, lakini hawakuwaona. Kisha walipita katika nchi ya Shaalimu, lakini hawakuwa huko. Baadaye alipita katika nchi ya Wabenyamini, lakini hawakuwaona wale punda.
5 When they came to the land of Zuph, Saul said to his servant who was with him, “Come, let us go back, or my father may stop caring for the donkeys and begin to worry about us.”
Na walipofika nchi ya Sufu, Sauli alimwambia mtumishi wake aliyekuwa naye, “Njoo na turudi, pengine baba aweza kuacha kuchunga punda na kuanza kutuhofia sisi.”
6 But the servant said to him, “Listen, there is a man of God in this city. He is a man who is held in honor; everything that he says comes true. Let us go there; maybe he can tell us which way we should go on our journey.”
Lakini mtumishi akamwmbia, “Sikiliza, Yupo mtu wa Mungu katika mji huu. Naye ni mtu wa kuheshimiwa sana; kila asemalo huwa kweli. Hebu twende huko; labda anaweza kutuambia tupitie wapi katika safari yetu.”
7 Then Saul said to his servant, “But if we go, what can we bring the man? For the bread in our sack is gone, and there is no present to bring to the man of God. What do we have?”
Ndipo Sauli akamwambia mtumish iwake, “Lakini kama tukienda kwake, twaweza kumpelekea nini? Maana hata mkate katika mfuko wetu umekwisha, na hakuna zawadi ya kumpelekea mtumishi wa Mungu. Tuna kitu gani?
8 The servant answered Saul and said, “Here, I have with me one-fourth of a shekel of silver that I will give to the man of God, to tell us which way we should go.”
Huyo mtumishi akamjibu Sauli na kusema, “Hapa, ninayo robo ya shekeli ya fedha ambayo nitampa mtumishi wa Mungu, atuambie ni njia ipi yatupasa tuiendee.”
9 (Formerly in Israel, when a man went to seek the knowledge of God's will, he said, “Come, let us go to the seer.” For today's prophet was formerly called a seer.)
(Zamani katika Israeli, mtu alipotaka kujua neno kuhusu mapenzi ya Mungu, alisema, “Njoo, haya twende kwa mwonaji.” Kwa maana nabii wa leo, zamani aliitwa Mwonaji).
10 Then Saul said to his servant, “Well said. Come, let us go.” So they went to the city where the man of God was.
Ndipo Sauli akamwambia mtumishi wake, “Umesema vyema. Haya, njoo twende.” Basi wakaenda katika mji ambao mtu wa Mungu alikuwamo.
11 As they went up the hill to the city, they found young women coming out to draw water; Saul and his servant said to them, “Is the seer here?”
Walipopanda mlima kuelekea mjini, walikutana na wasichana wakienda kuteka maji; Sauli na mtumishi wake wakawauliza, “Mwonaji hupo hapa?”
12 They answered, and said, “He is; see, he is just ahead of you. Hurry up, for he is coming to the city today, because the people are sacrificing today at the high place.
Nao wakawajibu, na kusema, “Yupo; tazameni, yuko mbele yenu. Harakisheni, kwa maana anakuja mjini leo, sababu leo watu wanatoa dhabihu zao mahali pa juu.
13 As soon as you enter the city you will find him, before he goes up to the high place to eat. The people will not eat until he comes, because he will bless the sacrifice; afterwards those who are invited will eat. Now go up, for you will find him immediately.”
Mara tu mtakapoingia mjini mtamuona, kabla hajapanda mahali pa juu kla chakula. Watu hawatakula hata atakapokuja, kwa sababu ndiye ataibariki dhabihu; na baadaye wale ambao wamealikwa hula. Basi pandeni, mtamuona sasa hivi.”
14 So they went up to the city. As they were entering the city, they saw Samuel coming out toward them, to go up to the high place.
Kwa hiyo walikwea kwenda mjini. Walipokuwa wakiingia mjini, walimuona Samweli akija mbele yao, akipanda kwenda mahali pa juu.
15 Now the day before Saul came, Yahweh had revealed to Samuel:
Siku moja kabla Sauli hajafika, BWANA alikuwa amemfunulia Samweli:
16 “Tomorrow about this time I will send you a man from the land of Benjamin, and you will anoint him to be prince over my people Israel. He will save my people from the hand of the Philistines. For I have looked on my people with pity because their call for help has come to me.”
“Kesho wakati kama huu nitakutumia mtu kutoka nchi ya Benyamini, nawe utamtia mafuta awe mfalme juu ya watu wangu Israeli. Atawaokoa watu wangu kutoka mkono wa Wafilisti. Kwa kuwa nimewaonea huruma watu wangu na kilio cha kutaka msaada kimenifikia.”
17 When Samuel saw Saul, Yahweh told him, “Here is the man I told you about! He is the one who will rule over my people.”
Samweli alipomuona Sauli, BWANA akamwambia, “Huyu ndiye mtu niliyekwambia habari zake! Yeye ndiye atakayewatawala watu wangu.”
18 Then Saul came close to Samuel in the gate and said, “Tell me where is the house of the seer?”
Ndipo Sauli akaja karibu na Samweli katika lango na kusema, “Niambie nyumba ya Mwonaji iko wapi?
19 Samuel answered Saul and said, “I am the seer. Go up before me to the high place, for today you will eat with me. In the morning I will let you go, and I will tell you everything that is on your mind.
Samweli akamjibu Sauli akisema, “Mimi ndiye mwonaji. Tangulia mbele hadi mahali pa juu, nami nitakueleza kila kitu kilichomoyoni mwako.
20 As for your donkeys that were lost three days ago, do not worry about them, for they have been found. Then on whom are all the desires of Israel set? Is it not on you and all your father's house?”
Kama punda wenu waliopotea siku tatu zilizopita, msihofu kuhusu hao punda, kwa kuwa wamekwishapatikana. Na yote yaliyotamanika kwa ajili ya Israeli yanamwangukia nani? Siyo kwako na nyumba ya baba yako yote?”
21 Saul answered and said, “Am not I a Benjamite, from the smallest of the tribes of Israel? Is not my clan the least of all the clans of the tribe of Benjamin? Why then have you spoken to me in this manner?”
Sauli akamjibu na kusema, Siyo mimi Mbenyamini, kutoka kabila lililo dogo sana kwa makabila ya Israeli? Siyo ukoo wangu ulio mdogo sana kwa kabila la Benyamini? Kwa nini basi unaniambia kwa namna hii?”
22 So Samuel took Saul and his servant, brought them into the hall, and seated them at the head place of those who had been invited, who were about thirty people.
Hivyo Samweli akamchukua Sauli na mtumishi wake, akawaingiza ukumbini, akawakalisha mahali pa heshima pa wale walioalikwa, idadi yao takribani watu thelathini.
23 Samuel said to the cook, “Bring the portion which I gave to you, of which I said to you, 'Put it aside.'”
Samweli akamwambia mpishi, “Lete sehemu niliyokupatia, sehemu ambayo nilikwambia hivi, “Itenge.”'
24 So the cook took up the thigh and what was on it and set it before Saul. Then Samuel said, “See what has been kept is set before you. Eat it, because it has been kept for you until the appointed time, from the time when I said, 'I have invited the people.'” So Saul ate with Samuel that day.
Basi mpishi alichukua paja lililokuwa limeinuliwa katika dhabihu na kile kilichokuwa pamoja nalo, akaitenga mbele ya Sauli. Kisha Samweli akasema, “Angalia kile kilichokuwa kimetunzwa kwa ajili yako! Kula, kwa sababu kilitunzwa hadi wakati maalum ufike kwa ajili yako. Na kwa sasa waweza kusema, 'Nimewaalika watu.”' Kwa hiyo Sauli alikula pamoja na Samweli siku hiyo.
25 When they had come down from the high place into the city, Samuel spoke with Saul on the rooftop.
Walipokuwa wamekwisha shuka chini kutoka sehemu ya juu na kuingia mjini, Samweli akazungumza na Sauli darini.
26 Then at the break of dawn, Samuel called to Saul on the rooftop and said, “Get up, so I can send you on your way.” So Saul got up, and both he and Samuel went out into the street.
Na kulipopambazuka, Samweli alimwita Sauli darini na kusema, “Amka, kusudi nikusindikize uende zako,” Hivyo Sauli aliamka, na wote wawili, yeye na Samweli walitoka kwenda mtaani.
27 As they were going to the outskirts of the city, Samuel said to Saul, “Tell the servant to go ahead of us”—and he went ahead—”but you must stay here awhile, that I may announce the message of God to you.”
Walipokuwa wakienda nje ya viunga vya mji, Samweli akamwambia Sauli, “Mwambie mtumishi wako atanguliye mbele yetu(na alitangulia mbele), Lakini wewe sharti usubiri kidogo, nipate kukuambia ujumbe wa Mungu.”