< 1 Samuel 27 >

1 David said in his heart, “I will now perish one day by Saul's hand; there is nothing better for me than to escape into the land of the Philistines; Saul will give up looking for me any more within all the borders of Israel; in this way I will escape out of his hand.”
Daudi akasema moyoni mwake, “Katika mojawapo ya siku hizi nitaangamizwa kwa mkono wa Sauli. Jambo lililo bora ni kutorokea kwenye nchi ya Wafilisti. Hivyo Sauli atakata tamaa ya kunisaka popote katika Israeli, nami nitakuwa nimeponyoka mkononi mwake.”
2 David arose and passed over, he and the six hundred men who were with him, to Achish son of Maok, the king of Gath.
Hivyo Daudi akaondoka na hao watu mia sita waliokuwa pamoja naye na kwenda kwa Akishi mwana wa Maoki mfalme wa Gathi.
3 David lived with Achish at Gath, he and his men, each man with his own household, and David with his two wives, Ahinoam the Jezreelite woman, and Abigail the Carmelite woman, Nabal's wife.
Daudi na watu wake wakakaa huko Gathi pamoja na Akishi. Kila mtu alikuwa pamoja na jamaa yake, naye Daudi pamoja na wakeze wawili: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, mjane wa Nabali.
4 Saul was told that David had fled to Gath, so he looked for him no longer.
Sauli alipokuwa ameambiwa kwamba Daudi alikuwa amekimbilia Gathi, hakuendelea kumsaka tena.
5 David said to Achish, “If I have found favor in your eyes, let them give me a place in one of the cities in the country, that I may live there. Why should your servant live in the royal city with you?”
Ndipo Daudi akamwambia Akishi, “Kama nimepata kibali machoni pako, unipe sehemu katika mojawapo ya miji katika nchi nikae huko. Kwa nini mtumwa wako akae pamoja nawe katika mji huu wa kifalme?”
6 So that day Achish gave him Ziklag; that is why Ziklag belongs to the kings of Judah to this very day.
Hivyo siku hiyo Akishi akampa Daudi mji wa Siklagi, nao Siklagi umekuwa mali ya wafalme wa Yuda tangu wakati huo.
7 The number of days that David lived in the land of the Philistines was a full year and four months.
Daudi akaishi katika nchi ya Wafilisti muda wa mwaka mmoja na miezi minne.
8 David and his men attacked various places, making raids on the Geshurites, the Girzites, and the Amalekites; for those nations were the inhabitants of the land, as you go to Shur, as far as the land of Egypt. They had been living there in the land from ancient times.
Basi Daudi na watu wake wakapanda na kuwashambulia Wageshuri, Wagirizi na Waamaleki. (Tangu zamani haya mataifa yalikuwa yameishi kwenye eneo lililotanda kuanzia Telemu katika njia iteremkayo Shuri hadi kufikia nchi ya Misri.)
9 David attacked the land and saved neither man nor woman alive; he took away the sheep, the oxen, the donkeys, the camels, and the clothing; he would return and come again to Achish.
Kila mara Daudi aliposhambulia eneo, hakubakiza hai mwanaume wala mwanamke, lakini alichukua kondoo na ngʼombe, punda na ngamia, na nguo. Kisha akarudi kwa Akishi.
10 Achish would say, “Against whom have you made a raid today?” David would answer, “Against the south of Judah,” or “Against the south of the Jerahmeelites,” or “Against the south of the Kenites.”
Akishi alipomuuliza, “Je leo umeshambulia wapi?” Daudi humjibu, “Dhidi ya Negebu ya Yuda,” au wakati mwingine husema, “Dhidi ya Negebu ya Yerameeli,” au “Dhidi ya Negebu ya Wakeni.”
11 David would keep neither man nor woman alive to bring them to Gath, saying, “So that they cannot say about us, 'David did such and such.'” This was what he did all the while he was living in the country of the Philistines.
Daudi hakumwacha hai mwanaume au mwanamke ili apate kuletwa Gathi, kwa maana Daudi aliwaza, “Wanaweza kujulisha habari zetu na kusema, ‘Hivi ndivyo alivyofanya Daudi.’” Hii ndiyo ilikuwa desturi yake wakati wote aliishi katika nchi ya Wafilisti.
12 Achish believed David, saying, “He has made his people Israel utterly abhor him; he will therefore be my servant forever.”
Akishi akamsadiki Daudi na kuwaza moyoni mwake, akasema, “Daudi amekuwa kitu cha kuchukiza kabisa kwa watu wake, Waisraeli, hivi kwamba atakuwa mtumishi wangu milele.”

< 1 Samuel 27 >