< 1 Samuel 26 >

1 The Ziphites came to Saul at Gibeah and said, “Is not David hiding in the hill of Hakilah, which is before Jeshimon?”
Hao Wazifu wakamwendea Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hakujificha katika kilima cha Hakila, kinachotazamana na Yeshimoni?”
2 Then Saul arose and went down to the wilderness of Ziph, having three thousand chosen men of Israel with him, to seek David in the wilderness of Ziph.
Hivyo Sauli akashuka kwenda katika Jangwa la Zifu, akiwa na watu wake 3,000 wa Israeli waliochaguliwa, kumsaka Daudi huko.
3 Saul camped on the hill of Hakilah, which is before Jeshimon, by the road. But David was staying in the wilderness, and he saw that Saul was coming after him into the wilderness.
Sauli akapiga kambi yake kando ya barabara juu ya kilima cha Hakila kinachotazamana na Yeshimoni, lakini Daudi alikuwa anaishi huko jangwani. Alipoona kuwa Sauli amemfuata huko,
4 So David sent out spies and learned that Saul had indeed come.
Daudi akatuma wapelelezi na akapata habari kwa hakika kwamba Sauli alikuwa amewasili.
5 David arose and went to the place where Saul had camped; he saw the place where Saul lay, and Abner son of Ner, the general of his army; Saul lay in the camp, and the people were camped around him, all asleep.
Ndipo Daudi akaondoka, akaenda hadi mahali Sauli alikuwa amepiga kambi. Akaona mahali Sauli na Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi, walipokuwa wamelala. Sauli alikuwa amelala ndani ya kambi, jeshi likiwa limemzunguka.
6 Then David said to Ahimelech the Hittite, and to Abishai son of Zeruiah, the brother of Joab, “Who will go down with me to Saul in the camp?” Abishai said, “I! I will go down with you.”
Basi Daudi akamuuliza Ahimeleki Mhiti, na Abishai mwana wa Seruya, nduguye Yoabu, akisema, “Ni nani atakayeshuka pamoja nami kambini kwa Sauli?” Abishai akajibu, “Nitakwenda pamoja nawe.”
7 So David and Abishai went to the army by night. Saul was there sleeping inside the camp with his spear stuck in the ground beside his head. Abner and his soldiers lay around him.
Hivyo Daudi na Abishai wakaenda kwenye jeshi wakati wa usiku, tazama Sauli, alikuwa amelala ndani ya kambi na mkuki wake umekitwa ardhini karibu na kichwa chake. Abneri na askari walikuwa wamelala kumzunguka Sauli.
8 Then Abishai said to David, “Today God has put your enemy into your hand. Now please let me pin him to the ground with the spear with just one blow. I will not strike him a second time.”
Abishai akamwambia Daudi, “Leo Mungu amemtia adui yako mikononi mwako. Sasa niruhusu nimchome mpaka ardhini kwa pigo moja la mkuki wangu; sitamchoma mara mbili.”
9 David said to Abishai, “Do not destroy him; for who can extend his hand against Yahweh's anointed one and be guiltless?”
Lakini Daudi akamwambia Abishai, “Usimwangamize! Ni nani awezaye kutia mkono juu ya mpakwa mafuta wa Bwana na asiwe na hatia?”
10 David said, “As Yahweh lives, Yahweh will kill him, or his day will come to die, or he will go into battle and perish.
Daudi akasema, “Hakika kama vile Bwana aishivyo, Bwana mwenyewe atampiga; au wakati wake utafika, naye atakufa, au atakwenda vitani na kuangamia.
11 May Yahweh forbid that I should extend my hand against his anointed one; but now, I beg you, take the spear that is at his head and the jar of water, and let us go.”
Lakini Mungu na apishie mbali nisije nikainua mkono juu ya mpakwa mafuta wa Bwana. Sasa chukua huo mkuki na hilo gudulia la maji vilivyo karibu na kichwa chake, tuondoke.”
12 So David took the spear and the jar of water from Saul's head, and they got away. No one saw them or knew about it, nor did anyone wake up, for they were all asleep, because a deep sleep from Yahweh had fallen on them.
Hivyo Daudi akachukua huo mkuki na hilo gudulia la maji vilivyokuwa karibu na kichwa cha Sauli, nao wakaondoka. Hakuna yeyote aliyeona au kufahamu habari hii, wala hakuna hata mmoja aliyeamka usingizini. Wote walikuwa wamelala, kwa sababu Bwana alikuwa amewatia kwenye usingizi mzito.
13 Then David went over to the other side and stood on the top of the mountain far off; a great distance was between them.
Kisha Daudi akavuka upande mwingine na kusimama juu ya kilima mahali palipokuwa na nafasi pana kati yao.
14 David shouted out to the people and to Abner son of Ner; he said, “Do you not answer, Abner?” Then Abner answered and said, “Who are you who is shouting to the king?”
Daudi akalipigia kelele jeshi na Abneri mwana wa Neri, akisema, “Je, Abneri, hutanijibu?” Abneri akajibu, “Nani wewe umwitaye mfalme?”
15 David said to Abner, “Are not you a courageous man? Who is like you in Israel? Why then have you not kept watch over your master the king? For someone came in to kill the king your master.
Daudi akasema, “Wewe si ni mtu shujaa? Ni nani aliye kama wewe katika Israeli? Kwa nini basi hukumlinda mfalme bwana wako? Mtu mmoja alikuja kumwangamiza mfalme, bwana wako.
16 This thing you have done is not good. As Yahweh lives, you deserve to die because you have not kept watch over your master, Yahweh's anointed one. Now see where the king's spear is and the jar of water that was near his head!”
Ulichokifanya si kizuri. Kwa hakika kama aishivyo Bwana, wewe na watu wako mnastahili kufa, kwa sababu hamkumlinda bwana wenu, mpakwa mafuta wa Bwana. Tazameni hapo mlipo. Uko wapi mkuki wa mfalme na gudulia la maji ambavyo vilikuwa karibu na kichwa chake?”
17 Saul recognized David's voice and said, “Is that your voice, my son David?” David said, “It is my voice, my master, king.”
Sauli akatambua sauti ya Daudi, na kusema, “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?” Daudi akajibu, “Naam, hiyo ndiyo, bwana wangu mfalme.”
18 He said, “Why does my master pursue his servant? What have I done? What evil is in my hand?
Pia akaongeza, “Kwa nini bwana wangu anamfuatia mtumishi wake? Nimefanya nini, nalo kosa langu ni lipi nililolifanya niwe na hatia?
19 Now therefore, I beg you, let my master the king listen to the words of his servant. If it is Yahweh who has stirred you up against me, let him accept an offering; but if it is human beings, may they be cursed in the sight of Yahweh, for they have today driven me out, that I should not cling to the inheritance of Yahweh; they have said to me, 'Go worship other gods.'
Sasa mfalme bwana wangu na asikilize maneno ya mtumishi wake. Kama Bwana amekuchochea dhidi yangu, basi yeye na aipokee sadaka yangu. Lakini hata hivyo, kama ni wanadamu waliofanya hivyo, walaaniwe mbele za Bwana! Wao sasa wamenifukuza kutoka sehemu yangu katika urithi wa Bwana wangu wakisema, ‘Nenda ukatumikie miungu mingine.’
20 Now therefore, do not let my blood fall to the earth away from Yahweh's presence; for the king of Israel has come out to look for the one flea as when one hunts a partridge in the mountains.”
Basi usiache damu yangu imwagike kwenye ardhi mbali na uso wa Bwana. Mfalme wa Israeli ametoka kutafuta kiroboto, kama vile mtu awindavyo kware katika milima.”
21 Then Saul said, “I have sinned. Return, David, my son; for I will harm you no more, because my life was precious in your eyes today. See, I have played the fool and have made a very bad mistake.”
Ndipo Sauli akasema, “Nimetenda dhambi. Rudi, Daudi mwanangu. Kwa kuwa uliyahesabu maisha yangu kuwa ya thamani leo, sitajaribu kukudhuru tena. Hakika nimetenda kama mpumbavu na nimekosa sana.”
22 David answered and said, “See, your spear is here, king! Let one of the young men come over and get it and bring it to you.
Daudi akajibu, “Mkuki wa mfalme uko hapa. Mmoja wa vijana wako na avuke kuuchukua.
23 May Yahweh pay each man for his righteousness and his faithfulness; because Yahweh put you into my hand today, but I would not strike his anointed.
Bwana humlipa kila mtu kwa ajili ya haki yake na uaminifu wake. Bwana alikutia katika mikono yangu leo, lakini sikuinua mkono wangu juu ya mpakwa mafuta wa Bwana.
24 See, as your life was precious in my eyes today, so may my life be much valued in the eyes of Yahweh, and may he rescue me out of all trouble.”
Kwa hakika kama vile maisha yako yalivyokuwa ya thamani kwangu leo, vivyo hivyo maisha yangu na yawe na thamani kwa Bwana na kuniokoa kutoka taabu zote.”
25 Then Saul said to David, “May you be blessed, David my son! You will certainly do great things and you will succeed in them.” So David went his way, and Saul returned to his place.
Ndipo Sauli akamwambia Daudi, “Mwanangu Daudi na ubarikiwe; utafanya mambo makubwa na hakika utashinda.” Basi Daudi akaenda zake, naye Sauli akarudi nyumbani.

< 1 Samuel 26 >