< 1 Samuel 21 >

1 Then David came to Nob to see Ahimelech the priest. Ahimelech came to meet David trembling and said to him, “Why are you alone and have no one with you?”
Daudi akaenda Nobu, kwa Ahimeleki kuhani. Ahimeleki akatetemeka alipokutana naye, akamuuliza, “Kwa nini uko peke yako? Kwa nini hukufuatana na mtu yeyote?”
2 David said to Ahimelech the priest, “The king has sent me on a mission and has said to me, 'Let no one know anything about the business I am sending you, and what I have commanded you.' I have directed the young men to a certain place.
Daudi akamjibu Ahimeleki kuhani, akisema, “Mfalme ameniagiza shughuli fulani na kuniambia, ‘Mtu yeyote asijue chochote kuhusu kazi yako wala maagizo yako!’ Kuhusu watu wangu, nimewaambia tukutane mahali fulani.
3 Now then what do you have on hand? Give me five loaves of bread, or whatever is here.”
Sasa basi, una nini mkononi? Nipatie mikate mitano au chochote unachoweza kupata.”
4 The priest answered David and said, “There is no ordinary bread on hand, but there is holy bread—if the young men have kept themselves from women.”
Lakini kuhani akamjibu Daudi, “Sina mkate wowote wa kawaida kwa sasa. Hata hivyo, ipo hapa mikate iliyowekwa wakfu, iwapo watu wamejitenga na wanawake.”
5 David answered the priest, “Surely women have been kept from us for the past three days, as usual when I set out. The things belonging to the men have been set apart even on ordinary missions. How much more today will what they have be set apart!”
Daudi akajibu, “Hakika tumejitenga na wanawake kwa siku hizi chache kama kawaida ya ninapotoka kwenda kwenye shughuli. Navyo vyombo vya wale vijana huwa ni vitakatifu hata kwenye safari ya kawaida, si zaidi sana leo vyombo vyao vitakuwa ni vitakatifu?”
6 So the priest gave him the bread that was set apart. For there was no bread there except the bread of the presence, which was removed from before Yahweh, in order to put hot bread in its place on the day it was taken away.
Hivyo kuhani akampa ile mikate iliyowekwa wakfu, kwa kuwa hapakuwepo mikate mingine isipokuwa hiyo ya Wonyesho iliyokuwa imeondolewa hapo mbele za Bwana na kubadilishwa na mingine yenye moto siku ile ilipoondolewa.
7 Now one of the servants of Saul was there that day, detained before Yahweh. His name was Doeg the Edomite, the chief of Saul's herdsmen.
Basi siku hiyo palikuwepo na mmoja wa watumishi wa Sauli, aliyezuiliwa mbele za Bwana; alikuwa Doegi Mwedomu, kiongozi wa wachunga wanyama wa Sauli.
8 David said to Ahimelech, “Now is there not here on hand any spear or sword? For I brought neither my sword nor my weapons with me, because the king's business was urgent.”
Daudi akamuuliza Ahimeleki, “Je, unao mkuki au upanga hapa? Sikuleta upanga wala silaha nyingine yoyote, kwa sababu shughuli ya mfalme ilikuwa ya haraka.”
9 The priest said, “The sword of Goliath the Philistine, whom you killed in the Valley of Elah, is here wrapped in a cloth behind the ephod. If you want to take that, take it, for there is no other weapon here.” David said, “There is no other sword like that one; give it to me.”
Kuhani akajibu, “Upanga wa Goliathi Mfilisti, ambaye ulimuua katika Bonde la Ela, upo hapa, umefungiwa katika kitambaa nyuma ya kisibau. Kama unauhitaji, uchukue, hakuna upanga mwingine hapa ila huo tu.” Daudi akasema, “Hakuna upanga mwingine kama huo. Nipatie huo.”
10 David arose and fled that day from Saul and went to Achish, the king of Gath.
Siku ile Daudi akamkimbia Sauli na kwenda kwa Akishi mfalme wa Gathi.
11 Achish's servants said to him, “Is not this David, the king of the land? Did they not sing to one another about him in dances, 'Saul has killed his thousands, and David his ten thousands?'”
Lakini watumishi wa Akishi wakamwambia, “Je, huyu si ndiye Daudi mfalme wa nchi? Je, huyu si ndiye yule ambaye wanaimba katika ngoma zao wakisema: “‘Sauli amewaua elfu zake, naye Daudi makumi elfu yake’?”
12 David took these words to heart and was very afraid of Achish, the king of Gath.
Daudi akayaweka maneno haya moyoni naye akamwogopa sana Akishi mfalme wa Gathi.
13 He changed his behavior before them and pretended to be insane in their hands; he made marks on the doors of the gate and let his saliva run down his beard.
Basi akajifanya mwendawazimu mbele yao; naye alipokuwa mikononi mwao, alitenda kama kichaa, akikwaruza kwa kutia alama juu ya milango ya lango na kuachia udelele kutiririka kwenye ndevu zake.
14 Then Achish said to his servants, “Look, you see the man is mad. Why have you brought him to me?
Akishi akawaambia watumishi wake, “Tazameni mtu huyu! Ana wazimu! Kwa nini mnamleta kwangu?
15 Do I lack madmen, so that you have brought this fellow to behave like one in my presence? Will this fellow really come into my house?”
Je, mimi nimepungukiwa na wenda wazimu kiasi kwamba mmeniletea mtu huyo hapa aendelee kufanya hivi mbele yangu? Je, ilikuwa ni lazima mtu huyo aje nyumbani kwangu?”

< 1 Samuel 21 >