< 1 Samuel 20 >

1 Then David fled from Naioth in Ramah and came and said to Jonathan, “What have I done? What is my iniquity? What is my sin before your father, that he seeks to take my life?”
Kisha Daudi akakimbia kutoka Nayothi huko Rama akamwendea Yonathani na kumuuliza, “Kwani nimefanya nini? Kosa langu ni nini? Nimemkosea baba yako kwa jinsi gani, hata kwamba anajaribu kuuondoa uhai wangu?”
2 Jonathan said to David, “Far from it; you will not die. My father does nothing either great or small without telling it to me. Why should my father hide this thing from me? It is not so.”
Yonathani akajibu, “La hasha! Hutakufa! Tazama, baba yangu hafanyi kitu chochote, kikubwa au kidogo, bila kuniambia mimi. Kwa nini anifiche hili? Sivyo ilivyo!”
3 Yet David vowed again and said, “Your father knows well that I have found favor in your eyes. He has said, 'Do not let Jonathan know this, or he will be grieved.' But as truly as Yahweh lives, and as you live, there is but a step between me and death.”
Lakini Daudi akaapa na kusema, “Baba yako anajua kabisa kwamba nimepata kibali mbele yako, naye amesema moyoni mwake, ‘Yonathani sharti asilijue hili, la sivyo atahuzunika.’ Lakini kweli kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, kuna hatua moja tu kati yangu na mauti.”
4 Then Jonathan said to David, “Whatever you say, I will do for you.”
Yonathani akamwambia Daudi, “Chochote unachotaka nifanye, nitakufanyia.”
5 David said to Jonathan, “Tomorrow is the new moon, and I ought to sit down to eat with the king. But let me go, so that I may hide myself in the field until the third day at evening.
Basi Daudi akamwambia, “Angalia, kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo, nami inanipasa kula chakula pamoja na mfalme; lakini niache niende kujificha shambani mpaka kesho kutwa.
6 If your father misses me at all, then say, 'David earnestly asked leave of me that he might run to Bethlehem his city; because it is the yearly sacrifice there for all the clan.'
Kama baba yako akiona ya kuwa sipo, mwambie, ‘Daudi aliniomba sana ruhusa kuwahi Bethlehemu, mji wake wa nyumbani, kwa sababu dhabihu ya mwaka inafanywa huko kwa ajili ya ukoo wake wote.’
7 If he says, 'It is well,' your servant will have peace. But if he is very angry, then know that he has decided on evil.
Kama akisema, ‘Ni vyema sana,’ basi mtumishi wako yu salama. Lakini kama akikasirika, unaweza kuwa na hakika kwamba anakusudia kunidhuru.
8 Therefore deal kindly with your servant. For you have brought your servant into a covenant of Yahweh with you. But if there is sin in me, kill me yourself; for why then should you bring me to your father?”
Lakini kwa habari yako wewe, mtende wema mtumishi wako, kwa sababu mmeingia kwenye agano pamoja naye mbele za Bwana. Kama nina hatia, basi niue wewe mwenyewe! Kwa nini unikabidhi kwa baba yako?”
9 Jonathan said, “Far be it from you! If I learned my father decided harm to come upon you, would I not tell you?”
Yonathani akasema, “La hasha! Kama ningekuwa na kidokezo kidogo kwamba baba yangu amekusudia kukudhuru wewe, je, nisingekuambia?”
10 Then David said to Jonathan, “Who will tell me if by chance your father should answer you roughly?”
Daudi akamuuliza, “Je, nani atakayeniambia kama baba yako atakujibu kwa ukali?”
11 Jonathan said to David, “Come, let us go out into the field.” So they both went out into the field.
Yonathani akamwambia, “Njoo, twende shambani.” Basi wakaenda huko pamoja.
12 Jonathan said to David, “May Yahweh, the God of Israel, be witness. When I have questioned my father around this time tomorrow, or the third day, see, if there is good will toward David, will I not then send to you and make it known to you?
Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Ninakuahidi kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, hakika nitamchunguza baba yangu wakati kama huu kesho kutwa! Kama ameweka utaratibu wa kufaa kukuhusu wewe, je, sitakutumia ujumbe na kukufahamisha?
13 If it pleases my father to do you harm, may Yahweh do to Jonathan and more also if I do not make it known to you and send you away, so that you may go in peace. May Yahweh be with you, as he has been with my father.
Lakini ikiwa baba yangu amenuia kukudhuru, Bwana na anishughulikie kwa ukali, iwapo sitakufahamisha na kukuaga uende salama. Bwana na awe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na baba yangu.
14 If I am still alive, will you not show me the covenant faithfulness of Yahweh, that I may not die?
Lakini nitendee wema usiokoma kama ule wa Bwana siku zote za maisha yangu, ili nisije nikauawa,
15 Do not cut off your covenant faithfulness from my house forever—not even when Yahweh cuts off every one of the enemies of David from the face of the earth.”
wala usiuondoe wema wako kwa jamaa yangu, hata kama ni wakati ule Bwana atakapokuwa amekatilia mbali kila adui wa Daudi kutoka kwenye uso wa dunia.”
16 So Jonathan made a covenant with the house of David and said, “May Yahweh require an accounting from the hand of the enemies of David.”
Basi Yonathani akafanya agano na nyumba ya Daudi, akisema: “Bwana na awaangamize adui za Daudi.”
17 Jonathan made David vow again because of the love that he had for him, because he loved him as he loved his own soul.
Naye Yonathani akamtaka Daudi athibitishe tena kiapo chake cha kumpenda, kwa sababu Yonathani alimpenda Daudi kama nafsi yake mwenyewe.
18 Then Jonathan said to him, “Tomorrow is the new moon. You will be missed because your seat will be empty.
Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo. Itajulikana kwamba haupo kwa kuwa kiti chako kitakuwa hakina mtu.
19 When you have stayed three days, go down quickly and come to the place where you hid yourself when the business was in hand, and stay by the stone Ezel.
Kesho kutwa, inapokaribia jioni, nenda mahali pale ulipojificha wakati tatizo hili lilipoanza na usubiri karibu na jiwe la Ezeli.
20 I will shoot three arrows to the side of it, as though I were shooting at a target.
Nitapiga mishale mitatu kando yake, kama kwamba nilikwenda kulenga shabaha.
21 Then I will send my young man and say to him, 'Go find the arrows.' If I say to the young boy, 'Look, the arrows are on this side of you; get them,” then come; for there will be safety for you and not harm, as Yahweh lives.
Kisha nitamtuma mvulana na kumwambia, ‘Nenda ukaitafute mishale.’ Kama nikimwambia, ‘Tazama mishale iko upande huu wako! Uilete hapa,’ basi uje, kwa sababu hakika kama Bwana aishivyo, wewe ni salama, hakuna hatari.
22 “But if I say to the young man, 'Look, the arrows are beyond you,' then go your way, for Yahweh has sent you away.
Lakini kama nikimwambia huyo mvulana, ‘Angalia, mishale iko mbele yako,’ basi inakupasa uondoke, kwa sababu Bwana amekuruhusu uende zako.
23 As for the agreement of which you and I have spoken, see, Yahweh is between you and me forever.'”
Kuhusu yale tuliyozungumza wewe na mimi: kumbuka, Bwana ndiye shahidi kati yako wewe na mimi milele.”
24 So David hid himself in the field. When the new moon came, the king sat down to eat food.
Basi Daudi akajificha shambani, na sikukuu ya Mwezi Mwandamo ilipowadia, mfalme akaketi ili ale.
25 The king sat on his seat, as usual, on the seat by the wall. Jonathan stood up, and Abner sat by Saul's side. But David's place was empty.
Akaketi mahali pake pa kawaida karibu na ukuta, kuelekeana na Yonathani, naye Abneri akaketi karibu na Mfalme Sauli, lakini kiti cha Daudi kilikuwa wazi.
26 Yet Saul did not say anything that day, because he thought, “Something has happened to him. He is not clean; surely he is not clean.”
Sauli hakusema chochote siku ile kwa kuwa alifikiri, “Kuna kitu cha lazima kimetokea kwa Daudi ambacho kimemfanya najisi asihudhurie karamuni, hakika yeye yu najisi.”
27 But on the second day, the day after the new moon, David's place was empty. Saul said to Jonathan his son, “Why has the son of Jesse not come to the meal either yesterday or today?”
Lakini siku iliyofuata, siku ya pili ya mwezi, kiti cha Daudi kilikuwa wazi tena. Kisha Sauli akamwambia mwanawe Yonathani, “Kwa nini mwana wa Yese hajaja chakulani jana wala leo?”
28 Jonathan answered Saul, “David earnestly asked permission from me to go to Bethlehem.
Yonathani akamjibu, “Daudi alinisihi sana nimpe ruhusa aende Bethlehemu.
29 He said, 'Please let me go. For our family has a sacrifice in the city, and my brother has ordered me to be there. Now, if I have found favor in your eyes, please let me go and see my brothers.' For this reason he has not come to the king's table.”
Alisema, ‘Niruhusu niende, kwa sababu jamaa yetu wana dhabihu mjini, na ndugu yangu ameniagiza niwepo huko. Kama nimepata kibali mbele yako, niruhusu niende kuona ndugu zangu.’ Hii ndiyo sababu hakuja mezani pa mfalme.”
30 Then Saul's anger burned against Jonathan, and he said to him, “You son of a perverse, rebellious woman! Do I not know that you have chosen the son of Jesse to your own shame, and to the shame of your mother's nakedness?
Hasira ya Sauli ikawaka dhidi ya Yonathani na kumwambia, “Wewe mwana wa mwanamke mkaidi na mwasi! Je, sijui kuwa umekuwa upande wa mwana wa Yese kwa aibu yako mwenyewe na kwa aibu ya mama yako aliyekuzaa?
31 For as long as the son of Jesse lives on the earth, neither you nor your kingdom will be established. Now then, send and bring him to me, for he must surely die.”
Maadamu mwana wa Yese angali anaishi katika dunia hii wewe wala ufalme wako hautasimama. Sasa tuma aitwe umlete kwangu, kwa kuwa ni lazima afe!”
32 Jonathan answered Saul his father, “For what reason should he be put to death? What has he done?”
Yonathani akamuuliza baba yake, “Kwa nini auawe? Kwani amefanya nini?”
33 Then Saul threw his spear at him to kill him. So Jonathan knew that his father was determined to put David to death.
Lakini Sauli akamtupia Yonathani mkuki wake kwa nguvu ili amuue. Hapo ndipo Yonathani alipotambua kwamba baba yake alikusudia kumuua Daudi.
34 Jonathan got up from the table in fierce anger and ate no food the second day of the month, for he was grieved over David, because his father had dishonored him.
Yonathani akainuka kutoka mezani kwa hasira kali. Siku ile ya pili ya mwezi hakula chakula, kwa kuwa alikuwa amehuzunishwa na vitendo vya aibu ambavyo baba yake alikuwa anamtendea Daudi.
35 In the morning, Jonathan went out into the field to the appointment with David, and a young man was with him.
Kesho yake asubuhi Yonathani alikwenda shambani kukutana na Daudi. Alikuwa amefuatana na mvulana mdogo,
36 He said to his young man, “Run and find the arrows that I shoot.” As the young man ran, he shot an arrow beyond him.
naye Yonathani akamwambia yule mvulana, “Kimbia ukatafute mishale nitakayorusha.” Mvulana alipokuwa akikimbia, akarusha mishale mbele yake.
37 When the young man came to the place where the arrow that Jonathan shot had landed, Jonathan called after the young man, and said, “Is not the arrow beyond you?”
Yule mvulana alipofika mahali pale ambapo mshale wa Yonathani ulipokuwa umeanguka, Yonathani akamwita, “Je, mshale hauko mbele yako?”
38 Then Jonathan called after the young man, “Hurry, be quick, do not stay!” So Jonathan's young man gathered up the arrows and came to his master.
Yonathani akampigia kelele, “Harakisha, nenda haraka! Usisimame!” Mvulana akaokota mshale na kurudi kwa bwana wake.
39 But the young man did not know anything. Only Jonathan and David knew the matter.
(Mvulana hakujua chochote juu ya hayo yote; Yonathani na Daudi tu ndio waliojua.)
40 Jonathan gave his weapons to his young man and said to him, “Go, take them to the city.”
Basi Yonathani akampa yule mvulana silaha zake na kumwambia, “Nenda, zirudishe mjini.”
41 As soon as the young man was gone, David stood up from behind the mound, lay facedown on the ground, and bowed himself three times. They kissed one another and wept together, with David weeping the more.
Baada ya mvulana kwenda, Daudi akainuka kutoka upande wa kusini wa lile jiwe, naye akasujudu uso wake mpaka nchi mara tatu mbele ya Yonathani. Kisha kila mmoja akambusu mwenzake, wakalia pamoja. Lakini Daudi akalia zaidi.
42 Jonathan said to David, “Go in peace, because we have both sworn in the name of Yahweh and said, 'May Yahweh be between you and me, and between my descendants and your descendants, forever.'” Then David stood up and left, and Jonathan returned to the city.
Yonathani akamwambia Daudi, “Nenda kwa amani, kwa kuwa tumeapiana kiapo cha urafiki kati yetu kwa jina la Bwana, tukisema, ‘Bwana ndiye shahidi kati yako na mimi, na kati ya wazao wako na wazao wangu milele.’” Kisha Daudi akaondoka, naye Yonathani akarudi mjini.

< 1 Samuel 20 >