< 1 Samuel 2 >

1 Hannah prayed and said, “My heart exults in Yahweh. My horn is exalted in Yahweh. My mouth boasts over my enemies, because I rejoice in your salvation.
Hana aliomba akasema, “moyo wangu wamtukuza BWANA. Pembe yangu imejulikana katika BWANA. Kinywa changu kinatamba dhidi ya maadui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
2 There is no one holy like Yahweh, for there is none besides you; there is no rock like our God.
Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA, kwa kuwa hakuna mwingine zaidi yako; hakuna mwamba kama Mungu wetu.
3 Boast no more so very proudly; let no arrogance come out of your mouth. For Yahweh is a God of knowledge; by him actions are weighed.
Msijivune sana hivyo kwa kiburi; vinywa vyenu visitoke majivuno. Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa; yeye huyapima matendo kwa mizani.
4 The bow of the mighty men are broken, but those who stumble put on strength like a belt.
Pinde za mashujaa zimevunjika, bali wale wanaojikwaa hujivika nguvu kama mshipi.
5 Those who were full have hired themselves out for bread; those who were hungry have stopped being hungry. Even the barren one gives birth to seven, but the woman who has many children languishes.
Wale walio na shibe ya kutosha wamejikodisha ili wapate chakula; wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Hata yule aliye kuwa tasa amezaa watoto saba, bali mwanamke mwenye watoto wengi amenyong'onyea.
6 Yahweh kills and brings to life. He brings down to Sheol and raises up. (Sheol h7585)
BWANA huua na huuisha. Hushusha kuzimu na huleta tena juu. (Sheol h7585)
7 Yahweh makes some people poor and some rich. He humbles, but he also lifts up.
BWANA humfanya maskini, na yeye ndiye humtajirisha mtu. Yeye hudhili, lakini pia hukweza
8 He raises up the poor out of the dust. He lifts the needy from the ash heap to make them sit with princes and inherit the seat of honor. For the pillars of the earth are Yahweh's and he has set the world upon them.
Yeye humwinua juu maskini toka mavumbini: Huwainua wahitaji toka jalalani na kuwaketisha pamoja na wakuu na kuwarithisha kiti cha enzi cha utukufu. Kwa kuwa nguzo za dunia ni za BWANA na ameukalisha ulimwengu juu yake.
9 He will guard the feet of his faithful people, but the wicked will be put to silence in darkness, for no one will prevail by strength.
Yeye atazilinda nyayo za watu wake waaminifu, bali waovu watanyamazishwa gizani, kwa maana hakuna atayeshinda kwa nguvu zake.
10 Those who oppose Yahweh will be broken to pieces; he will thunder against them from heaven. Yahweh will judge the ends of the earth; he will give strength to his king and exalt the horn of his anointed.”
Wale wampingao BWANA watavunjwa vipande vipande; atawapiga radi kutokea mbinguni. BWANA atahukumu miisho ya dunia; atampa nguvu mfalme wake na kuinua pembe ya mtiwa mafuta wake.”
11 Then Elkanah went to Ramah, to his house. The child served Yahweh in the presence of Eli the priest.
Nndipo Elikana akenda Rama, nyumbani kwake. Na yule mtoto akamtumikia BWANA machoni pa Eli, kuhani.
12 Now the sons of Eli were worthless men. They did not know Yahweh.
Basi, watoto wa Eli walikuwa wakorofi. Wao hawakumheshimu BWANA.
13 The custom of the priests with the people was that when any man offered a sacrifice, the priest's servant would come with a three-pronged fork in his hand, while the meat was boiling.
Desturi ya makuhani na watu ilikuwa kwamba endapo mtu yeyote ametoa dhabihu, mtumishi wa kuhani angekuja akiwa na uma wa meno matatu mkononi mwake, nyama ilipokuwa inatokoswa.
14 He would stick it into the pan, or kettle, or cauldron, or pot. All that the fork brought up the priest would take for himself. They did this in Shiloh with all the Israelites that came there.
Naye angeutia uma huo sufuriani, au birikani au chomboni au chunguni; nyama yote ambayo ingeinuliwa na uma huo ingetwaliwa na kuhani mwenyewe. Ndivyo walivyofanya huko Shilo kwa Waisraeli wote waliokwenda huko.
15 Worse, before they burned the fat, the priest's servant came, and said to the man who was sacrificing, “Give meat to roast for the priest; for he will not accept boiled meat from you, but only raw.”
Tena, kabla ya kuteketeza mafuta, mtumishi wa kuhani alikuja, na kumwambia aliyekuwa akitoa dhabihu, “Tenga nyama ya kuchoma kwa ajili ya kuhani; kwa sababu hataikubali ile ya kutokosa kutoka kwako, bali tu ile mbichi.”
16 If the man said to him, “They must burn the fat first, and then take as much as you want.” Then he would say, “No, you will give it me now; if not, I will take it by force.”
Ikiwa mtu atamwambia, “Wachome mafuta kwanza, na kisha uchukue kiasi utakacho.” Ndipo angesema, “Hapana, utanipatia sasa hivi; la sivyo; Nitaichukua kwa lazima.”
17 The sin of these young men was very great before Yahweh, for they despised Yahweh's offering.
Dhambi ya vijana hawa ilikuwa mbaya sana mbele za BWANA, kwa sababu waliidharau dhabihu ya BWANA.
18 But Samuel served Yahweh as a child clothed with a linen ephod.
Lakini Samweli alimtumikia BWANA akiwa mdogo akivaa nguo ya naivera ya kitani.
19 His mother would make him a little robe and bring it to him from year to year, when she came up with her husband to offer the yearly sacrifice.
Kila mwaka mama yake alimtengenezea kanzu dogo na kumletea, wakati wakija na mmewe kutoa dhabihu ya kila mwaka.
20 Eli would bless Elkanah and his wife and say, “May Yahweh give you more children by this woman because of the request she made of Yahweh.” Then they would return to their own home.
Eli aliwabariki Elikana na mke wake na kusema, “BWANA akupatie watoto zaidi kwa mwanamke huyu kwa sababu ya ahadi yake aliyoitoa kwa BWANA.” Baadaye walirudi nyumbani kwao.
21 Yahweh again helped Hannah, and again she became pregnant. She bore three sons and two daughters. Meanwhile, the child Samuel grew before Yahweh.
BWANA alimsaidia tena Hana, akawa amebeba mimba nyingine. Akazaa watoto watatu wa kiume na wa kike wawili. Wakati huo huo mtoto Samweli akakua akiwa mbele za BWANA.
22 Now Eli was very old; he heard all that his sons were doing to all Israel, and how they slept with the women who served at the entrance to the tent of meeting.
Basi Eli alikuwa mzee sana, akayasikia yote ambayo watoto wake walikuwa wakiwafanyia Waisraeli wote, na jinsi walivyotembea na mwanamke aliyekuwa akitumika katika lango la hema ya kukutania.
23 He said to them, “Why do you such things? For I hear of your evil actions from all these people.”
Akawaambia, “Kwa nini mnafanya mambo hayo? Kwa maana nasikia matendo yenu maovu kutoka kwa watu hawa wote.”
24 No, my sons; for it is not a good report that I hear. You make Yahweh's people disobey.
Sivyo hivyo, watoto wangu, maana hii ninayoisikia siyo taarifa njema. Mnawakosesha watu wa BWANA.
25 “If one man sins against another, God will judge him; but if a man sins against Yahweh, who will speak for him?” But they would not listen to the voice of their father, because Yahweh intended to kill them.
“Kama mtu mmoja akimkosea mwenzake, Mungu atamhukumu; Lakini mtu akimkosea BWANA, ni nani atakayemtetea mtu huyo?” Lakini hawakuitii sauti ya baba yao, sababu BWANA alinuia kuwaua.
26 The child Samuel grew up, and increased in favor with Yahweh and also with men.
Yule mtoto Samweli aliongezeka umri, na kupata kibali kwa BWANA na kwa watu pia.
27 Now a man of God came to Eli and said to him, “Yahweh says, 'Did I not reveal myself to the house of your ancestor, when they were in Egypt in bondage to Pharaoh's house?
Kisha mtu wa Mungu akamwendea Eli na kumwambia, “BWANA asema, 'Je, sikujifunua mwenyewe kwa nyumba ya baba zako, walipokuwa Misri utumwani nyumbani mwa Farao?
28 I chose him out of all the tribes of Israel to be my priest, to go up to my altar, and to burn incense, to wear an ephod before me. I gave to the house of your ancestor all the offerings of the people of Israel made with fire.
Mimi nilimchagua yeye kutoka makabila yote ya Israeli awe kuhani wangu, apande madhabahuni kwangu, na kufukiza uvumba, na kuvaa kanzu ya naivera mbele yangu. Niliwapa nyumba ya baba zako dhabihu zote za wana wa Israeli zilizotolewa kwa moto.
29 Why, then, do you scorn my sacrifices and offerings that I required in the place where I live? Why do you honor your sons above me by making yourselves fat with the best of every offering of my people Israel?'
Kwanini basi, unaidharau dhabihu yangu na sadaka ambazo ninazitaka mahali ninapoishi? Kwanini unawaheshimu watoto wako kuliko mimi, kwa kujinenepesha ninyi wenyewe kwa uzuri wa kila sadaka ya watu wangu Israeli?'
30 For Yahweh, the God of Israel, says, 'I promised that your house, and the house of your ancestor, should walk before me forever.' But now Yahweh says, 'Far be it from me to do this, for I will honor those who honor me, but those who despise me will be lightly esteemed.
Maana, BWANA, Mungu wa Isareli, asema, niliahidi kwamba nyumba yako, na nyumba ya baba yako, yawapasa kwenda mbele zangu milele,' Lakini sasa BWANA asema. 'Mambo haya yapishe mbali. nami nisifanye hivi, maana nitawaheshimu wanaoniheshimu, bali wanaonidharau mimi hawatakuwa na thamani.
31 See, the days are coming when I will cut off your strength and the strength of your father's house, so that there will no longer be any old man in your house.
Tazama, siku zinakuja nitakapoondoa nguvu zako na nguvu za nyumba za baba yako, ili kwamba pasije kuwepo mtu mzee katika nyumba yako.
32 You will see distress in the place where I live. Although good will be given to Israel, there will no longer be any old man in your house.
Nawe utalitazama hangaiko katika makao yangu. Ingawa Israeli watapewa jambo jema, hapatakuwapo tena mtu yeyote mzee katika nyumba yako.
33 Any one of you that I do not cut off from my altar, I will cause your eyes to fail, and I will cause grief for your life. All the men born in your family will die.
Yeyote miongoni mwenu nisiye mwondoa kutoka madhabahuni pangu, Nitasababisha macho yenu yaanguke, na ita nitasababisha huzuni maishani mwenu. Wanaume wote waliozaliwa katika familia yako watakufa.
34 This will be the sign for you that will come on your two sons, on Hophni and Phinehas: They will both die on the same day.
Hii ndiyo itakuwa ishara kwako ambayo itawaijia watoto wako wakiume wawili, juu ya Hofni na Finehasi: Wote wawili watakufa siku moja.
35 I will raise up for myself a faithful priest who will do what is in my heart and in my soul. I will build him a sure house; and he will walk before my anointed king forever.
Nami nitamwinua juu kuhani wangu mwaminifu atakaye fanya kile kilichomo moyoni mwangu na nafisini mwangu. Nami nitamjengea nyumba madhubuti; naye atakwenda mbele ya mfalme wangu mbarikiwa milele.
36 Everyone who is left in your house will come and bow down to him, asking for a piece of silver and a loaf of bread, and will say, “Please assign me to one of the priests' positions so I can eat a piece of bread.”'”
Kila mmoja aliyebakia nyumbani mwako atakuja na kusujudu mbele ya mtu huyo, akiomba kipande cha fedha na mkate mmoja, naye atasema, “Tafadhali uniajiri katika moja ya nafasi za kuhani ili niweze kula kipande cha mkate'”'

< 1 Samuel 2 >