< 1 Chronicles 3 >

1 Now these are the sons of David who were born to him in Hebron: the firstborn was Amnon, by Ahinoam from Jezreel; the second was Daniel, by Abigail from Carmel;
Hawa ndio waliokuwa wana wa Daudi waliozaliwa huko Hebroni: Mzaliwa wa kwanza alikuwa Amnoni ambaye mama yake aliitwa Ahinoamu wa Yezreeli; wa pili, Danieli ambaye mama yake alikuwa Abigaili wa Karmeli;
2 the third was Absalom, whose mother was Maakah, daughter of Talmai king of Geshur. The fourth was Adonijah son of Haggith;
wa tatu alikuwa Absalomu, ambaye mama yake alikuwa Maaka, binti Talmai mfalme wa Geshuri; wa nne, Adoniya, ambaye mama yake alikuwa Hagithi;
3 the fifth was Shephatiah by Abital; the sixth was Ithream by Eglah his wife.
wa tano alikuwa Shefatia ambaye mama yake alikuwa Abitali; wa sita alikuwa Ithreamu, aliyezaliwa na mke wake Egla.
4 These six were born to David in Hebron, where he reigned seven years and six months. He then ruled thirty-three years in Jerusalem.
Hawa sita walizaliwa huko Hebroni ambako Daudi alitawala kwa miaka saba na miezi sita. Daudi alitawala Yerusalemu kwa miaka thelathini na mitatu,
5 These four sons, by Bathsheba daughter of Ammiel, were born to him in Jerusalem: Shammua, Shobab, Nathan, and Solomon.
nao hawa ndio watoto wa Daudi waliozaliwa huko Yerusalemu: mkewe Bathsheba, binti Amieli, alimzalia Shamua, Shobabu, Nathani na Solomoni.
6 David's other nine sons were: Ibhar, Elishua, Eliphelet,
Pia kulikuwa na wana wengine: Ibihari, Elishua, Elifeleti,
7 Nogah, Nepheg, Japhia,
Noga, Nefegi, Yafia,
8 Elishama, Eliada, and Eliphelet.
Elishama, Eliada na Elifeleti; wote walikuwa tisa.
9 These were David's sons, not including the sons by his concubines. Tamar was their sister.
Hawa wote walikuwa wana wa Daudi, mbali na wale wana waliozaliwa na masuria. Naye Tamari alikuwa dada yao.
10 Solomon's son was Rehoboam. Rehoboam's son was Abijah. Abijah's son was Asa. Asa's son was Jehoshaphat.
Mwana wa Solomoni alikuwa Rehoboamu, mwanawe huyo alikuwa Abiya, mwanawe huyo alikuwa Yehoshafati, mwanawe huyo alikuwa Asa,
11 Jehoshaphat's son was Jehoram. Jehoram's son was Ahaziah. Ahaziah's son was Joash.
mwanawe huyo alikuwa Yehoramu, mwanawe huyo alikuwa Ahazia, mwanawe huyo alikuwa Yoashi,
12 Joash's son was Amaziah. Amaziah's son was Azariah. Azariah's son was Jotham.
mwanawe huyo alikuwa Amazia, mwanawe huyo alikuwa Azaria, mwanawe huyo alikuwa Yothamu,
13 Jotham's son was Ahaz. Ahaz's son was Hezekiah. Hezekiah's son was Manasseh.
mwanawe huyo alikuwa Ahazi, mwanawe huyo alikuwa Hezekia, mwanawe huyo alikuwa Manase,
14 Manasseh's son was Amon. Amon's son was Josiah.
mwanawe huyo alikuwa Amoni na mwanawe huyo alikuwa Yosia.
15 Josiah's sons were his firstborn Johanan, his second son Jehoiakim, his third son Zedekiah, and his fourth son Shallum.
Wana wa Yosia walikuwa: Yohanani mzaliwa wake wa kwanza, Yehoyakimu mwanawe wa pili, wa tatu Sedekia, wa nne Shalumu.
16 Jehoiakim's sons were Jehoiachin and Zedekiah.
Walioingia mahali pa Yehoyakimu kama wafalme ni: Yekonia mwanawe, na Sedekia.
17 The sons of Jehoiachin, the captive, were Shealtiel,
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yekonia aliyekuwa mateka: Shealtieli mwanawe,
18 Malkiram, Pedaiah, Shenazzar, Jekamiah, Hoshama, and Nedabiah.
Malkiramu, Pedaya, Shenasari, Yekamia, Hoshama na Nedabia.
19 Pedaiah's sons were Zerubbabel and Shimei. Zerubbabel's sons were Meshullam and Hananiah; Shelomith was their sister.
Wana wa Pedaya walikuwa: Zerubabeli na Shimei. Wana wa Zerubabeli walikuwa: Meshulamu na Hanania. Shelomithi alikuwa dada yao.
20 His other five sons were Hashubah, Ohel, Berekiah, Hasadiah, and Jushab-Hesed.
Pia walikuwepo wengine watano: Hashuba, Oheli, Berekia, Hasadia na Yushab-Hesedi.
21 Hananiah's sons were Pelatiah and Jeshaiah. His son was Rephaiah, and further descendants were Arnan, Obadiah, and Shekaniah.
Wazao wa Hanania walikuwa: Pelatia na Yeshaya, na wana wa Refaya, na wana wa Arnani, na wana wa Obadia, na wana wa Shekania.
22 Shekaniah's son was Shemaiah. Shemaiah's sons were Hattush, Igal, Bariah, Neariah, and Shaphat.
Wazao wa Shekania: Shemaya na wanawe: Hatushi, Igali, Baria, Nearia na Shafati; jumla yao walikuwa sita.
23 Neariah's three sons were Elioenai, Hizkiah, and Azrikam.
Wana wa Nearia walikuwa: Elioenai, Hizkia na Azrikamu; jumla yao watatu.
24 Elioenai's seven sons were Hodaviah, Eliashib, Pelaiah, Akkub, Johanan, Delaiah, and Anani.
Wana wa Elioenai walikuwa: Hodavia, Eliashibu, Pelaya, Akubu, Yohanani, Delaya na Anani; jumla yao wote saba.

< 1 Chronicles 3 >