< Mark 8 >

1 In those dayes whe ther was a very greate companye and had nothinge to eate Iesus called his disciples to him and sayd vnto the:
Katika siku hizo, kulikuwa tena na umati mkubwa, na hawakuwa na chakula. Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,
2 I have copassion on this people because they have nowe bene with me. iii. dayes and have nothinge to eate:
“Ninauhurumia umati huu, wameendelea kuwa nami kwa siku tatu na hawana chakula.
3 And yf I shuld sende the awaye fastinge to their awne houses they shulde faynt by the waye. For dyvers of the came from farre.
Nikiwatawanya warudi majumbani kwao bila kula wanaweza wakazimia njiani kwa njaa. Na baadhi yao wametoka mbali sana.”
4 And his disciples answered him: where shuld a man have breade here in the wildernes to satisfie these?
Wanafunzi wake wakamjibu, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwashibisha watu hawa katika eneo hili lililoachwa?”
5 And he axed them: how many loves have ye? They sayde: seven.
Akawauliza, “mna vipande vingapi vya mikate?” Wakasema, “Saba”.
6 And he commaunded the people to syt doune on the grounde. And he toke the. vii. loves gave thankes brake and gave to his disciples to set before them. And they dyd set the before the people.
Aliuamuru umati ukae chini. Akachukua mikate saba, akamshukuru Mungu, na kuivunja. Akawapa wanafunzi wake waiweke mbele yao, nao wakaiweka mbele ya umati.
7 And they had a feawe smale fysshes. And he blessed them and comaunded them also to be set before them.
Pia walikuwa na samaki wadogo wachache, na baada ya kushukuru, aliwaamuru wanafunzi wake wawagawie hivi pia.
8 And they ate and were suffysed: And they toke vp yf the broken meate that was lefte. vii. baskettes full.
Walikula na wakatosheka. Na walikusanya vipande vilivyo baki, vikapu vikubwa saba.
9 And they yt ate were in nomber aboute fowre thousand. And he sent them awaye.
Walikaribia watu elfu nne. Na aliwaacha waende.
10 And a none he entred into a ship wt his disciples and came into the parties of Dalmanutha.
Mara aliingia kwenye mashua na wanafunzi wake, na wakaenda katika ukanda ya Dalmanuta.
11 And the pharises cam forth and begane to dispute with him sekinge of him a signe fro heven and temptinge him.
Kisha Mafarisayo walitoka nje na kuanza kubishana naye. Walitaka awape ishara kutoka mbinguni, kwa kumjaribu.
12 And he sygthed in his sprete and sayde: why doth this generacion seke a signe? Verely I saye vnto you ther shall no signe be geven vnto this generacion.
Akatafakari kwa kina moyoni mwake akasema, “Kwa nini kizazi hiki kinatafuta ishara? Nawaambia ninyi kweli, hakuna ishara itakayotolewa kwa kizazi hiki.”
13 And he lefte the and went into the ship agayne and departed over the water.
Kisha akawaacha, akaingia ndani ya mashua tena, akaondoka kuelekea upande mwingine.
14 And they had forgotte to take breed wt the nether had they in the ship with them more then one loofe.
Wakati huo wanafunzi walisahau kuchukua mikate. Hawakuwa na mikate zaidi ya kipande kimoja kilichokuwa kwenye mashua.
15 And he charged the sayinge. Take hede and beware of ye leven of ye pharises and of ye leve of Herode.
Aliwaonya na kusema, “Muwe macho na mjilinde dhidi ya chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.
16 And they reasoned amonge the selves sayinge: we have no breed
Wanafunzi wakasemezana wao kwa wao, “Ni kwa sababu hatuna mikate.”
17 And whe Iesus knewe yt he sayde vnto the: why take ye thought because ye have no bread? perceave ye not yet nether vnderstonde? Have ye youre hertes yet blynded?
Yesu alilitambua hili, na akawaambia, “Kwa nini mnasemezana kuhusu kutokuwa na mikate? Hamjajua bado? Hamuelewi? Mioyo yenu imekuwa miepesi?
18 Have ye eyes and se not? and have ye eares and heare not? Do ye not remember?
Mna macho, hamuoni? Mna masikio, hamsikii? Hamkumbuki?
19 When I brake v. loves amonge. v. M. How many baskettes full of broke meate toke ye vp? They sayde vnto him twelve.
Nilipoigawanya mikate mitano kwa watu elfu tano, mlichukua vikapu vingapi vilivyo jaa vipande vya mikate?” Wakamjibu, “kumi na mbili.”
20 When I brake. vii. amonge. iiii. M. How many basketes of the levinges of broken meate toke ye vp? they sayde. vii.
“Na nilipoigawanya mikate saba kwa watu elfu nne, mlichukua vikapu vingapi?”
21 And he sayde vnto the: how is it yt ye vnderstonde not?
Wakasema, “Saba.” Akawaambia, “Bado hamuelewi?”
22 And he came to Bethsaida and they brought a blynde man vnto him and desyred him to touche him.
Wakaja Bethsaida. Watu hao walimleta kwa Yesu mtu kipofu na wakamsihi Yesu amguse.
23 And he caught the blynde by the honde and leade him out of the toune and spat in his eyes and put his hondes apon him and axed him whether he saw ought.
Yesu akamshika kwa mkono yule kipofu, na kumwongoza nje ya kijiji. Alipotema mate juu ya macho yake na kunyosha mikono yake juu yake, alimuuliza, “Unaona chochote?”
24 And he loked vp and sayde: I se ye men: For I se the walke as they were trees.
Alitazama juu na kusema, “Naona watu wanaonekana kama miti inatembea.”
25 After that he put his hondes agayne apon his eyes and made him see. And he was restored to his sight and sawe every ma clerly.
Ndipo akanyosha tena mikono yake juu ya macho yake, mtu yule akafungua macho yake, aliona tena, na akaona kila kitu vizuri.
26 And he sent him home to his housse sayinge: nether goo into the toune nor tell it to eny in the toune.
Yesu alimwacha aende nyumbani na akamwambia, “Usiingie mjini.”
27 And Iesus went out and his disciples into the tounes that longe to the cite called Cesarea Philippi. Aud by the waye he axed his disciples sayinge: whom do men saye yt I am?
Yesu aliondoka na wanafunzi wake kwenda vijiji vya Kaiseria ya Filipi. Wakiwa njiani aliwauliza wanafunzi, “Watu wanasema mimi ni nani?”
28 And they answered: some saye that thou arte Iohn Baptiste: some saye Helyas: and some one of the Prophetes.
Wakamjibu wakasema, “Yohana mbatizaji. Wengine wanasema, 'Eliya' na wengine, 'Mmoja wa Manabii.”
29 And he sayde vnto the: But whom saye ye that I am? Peter answered and sayd vnto him: Thou arte very Christe.
Akawauliza, “Lakini ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro kamwambia, “Wewe ni Kristo.”
30 And he charged them that they shuld tell no man of it.
Yesu akawaonya wasimwabie mtu yeyote kumuhusu Yeye.
31 And he beganne to teache them how that the sonne of man must suffre many thinges and shuld be reproved of the elders and of the hye prestes and scribes and be kylled and after thre dayes aryse agayne.
Na akaanza kuwafundisha ya kuwa Mwana wa Adamu lazima ateseke kwa mambo mengi, na atakataliwa na viongozi na makuhani wakuu, na waandishi, na atauawa, na baada ya siku tatu atafufuka.
32 And he spake that sayinge openly. And Peter toke him asyde and began to chyde him.
Alisema haya kwa uwazi. Ndipo Petro akamchukua pembeni na akaanza kumkemea.
33 Then he tourned aboute and looked on his disciples and rebuked Peter sayinge: Goo after me Satan. For thou saverest not ye thinges of God but the thinges of men.
Lakini Yesu aligeuka na kuwatazama wanafunzi wake na akamkemea Petro na kusema, “Pita nyuma yangu Shetani! Hujali mambo ya Mungu, isipokuwa mambo ya watu.”
34 And he called the people vnto him with his disciples also and sayd vnto them: Whosoever will folowe me let him forsake him sylfe and take vp his crosse and folowe me.
Kisha akauita umati na wanafunzi wake pamoja, na kuwaambia, “Kama kuna mtu anataka kunifuata, ajikane mwenyewe, achukue msalaba wake, na anifuate.
35 For whosoever will save his lyfe shall lose it But whosoever shall lose his lyfe for my sake and ye gospels ye same shall save it.
Kwa kuwa yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayepoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya injili, atayaokoa.
36 What shall it profet a ma yf he shuld wynne all ye worlde and loose his awne soule?
Inamfaidia nini mtu, kupata ulimwengu wote, na kisha kupata hasara ya maisha yake?
37 or els what shall a ma geve to redeme his soule agayne?
Mtu anaweza kutoa nini badala ya maisha yake?
38 Whosoever therfore shall be asshamed of me and of my wordes amonge this advoutrous and sinfull generacion: of him shall the sonne of man be ashamed when he cometh in the glory of his father wt the holy angels.
Yeyote anioneaye aibu na maneno yangu katika kizazi hiki cha wazinzi na kizazi cha wenye dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea aibu atakapokuja katika ufalme wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.

< Mark 8 >