< Acts 11 >

1 And the Apostles and the brethren that were thorowout Iewry harde saye that the hethen had also receaved the worde of God.
Mitume na ndugu walioamini waliokuwa huko Uyahudi wakasikia kuwa watu wa Mataifa nao wamepokea neno la Mungu.
2 And when Peter was come vp to Ierusalem they of the circumcision reasoned wyth him
Hivyo Petro alipopanda Yerusalemu, wale wa tohara waliokuwa wameamini wakamshutumu,
3 sayinge: Thou wentest in to men vncircumcised and atest with them.
wakisema, “Ulikwenda kwa watu wasiotahiriwa na kula pamoja nao.”
4 Then Peter began and expounded ye thinge in order to the sayinge:
Ndipo Petro akaanza kuwaeleza kuhusu mambo yote yalivyotokea hatua kwa hatua akisema,
5 I was in the cyte of Ioppa prayinge and in a traunce I sawe a vision a certen vessell descende as it had bene a large lynnyn clothe let doune from hevin by the fower corners and it cam to me.
“Nilikuwa katika mji wa Yafa nikiomba, nami nikapitiwa na usingizi wa ghafula, nikaona maono. Kulikuwa na kitu kama nguo kubwa ikishuka kutoka mbinguni, ikishushwa kwa ncha zake nne, nayo ikanikaribia.
6 Into the which when I had fastened myn eyes I consydered and sawe fowerfoted beastes of ye erth and vermen and wormes and foules of the ayer.
Nilipoangalia ndani yake kwa karibu niliona wanyama wenye miguu minne wa nchini, wanyama wa mwitu, watambaao na ndege wa angani.
7 And I herde a voyce sayinge vnto me: aryse Peter sley and eate.
Ndipo nikasikia sauti ikiniambia, ‘Petro, ondoka uchinje na ule.’
8 And I sayd: God forbyd lorde for nothinge comen or vnclene hath at eny tyme entred into my mouth.
“Nikajibu, ‘La hasha Bwana! Kitu chochote kilicho najisi hakijaingia kinywani mwangu.’
9 But the voyce answered me agayne from heven cout not thou those thinges come which god hath clensed.
“Sauti ikasema kutoka mbinguni mara ya pili, ‘Usikiite najisi kitu chochote Mungu alichokitakasa.’
10 And this was done thre tymes. And all were takin vp agayne into heven.
Jambo hili lilitokea mara tatu, ndipo kile kitu kikavutwa tena mbinguni.
11 And beholde immediatly ther were thre men come vnto the housse where I was sent from Cesarea vnto me.
“Wakati ule ule watu watatu, waliokuwa wametumwa kutoka Kaisaria waliwasili katika nyumba niliyokuwa nikikaa.
12 And the sprete sayde vnto me that I shuld go with them with out doutinge. Morover the sixe brethren accompanyed me: and we entred into the mas housse.
Roho Mtakatifu akaniambia niende nao bila kuwa na ubaguzi kati yao na sisi. Hawa ndugu sita pia walifuatana nami, nasi tukaingia nyumbani mwa huyo Kornelio.
13 And he shewed vs how he had sene an angell in his housse which stod and sayde to him: Send men to Ioppa and call for Symon named also Peter:
Akatuambia jinsi alivyoona malaika aliyekuwa amesimama katika nyumba yake na kusema, ‘Tuma watu waende Yafa wakamlete Simoni aitwaye Petro.
14 he shall tell the wordes wherby both thou and all thyne housse shalbe saved.
Yeye atakupa ujumbe ambao kwa huo wewe na wa nyumbani mwako wote mtaokoka.’
15 And as I begane to preach ye holy goost fell on them as he dyd on vs at the begynninge.
“Nami nilipoanza kusema, Roho Mtakatifu akashuka juu yao kama vile alivyotushukia sisi hapo mwanzo.
16 Then came to my remembrauce ye wordes of the Lorde how he sayde: Iohn baptised with water but ye shalbe baptysed with the holy goost.
Nami nikakumbuka neno la Bwana alivyosema, ‘Yohana alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu.’
17 For as moche then as God gave the lyke gyftes as he dyd vnto vs when we beleved on the Lorde Iesus Christ: what was I that I shuld have with stonde God?
Basi ikiwa Mungu aliwapa hawa watu kipawa kile kile alichotupa sisi tuliomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani hata nifikirie kuwa ningeweza kumpinga Mungu?”
18 when they hearde this they helde their peace and gloryfied God sayinge: then hath God also to the gentyls graunted repentaunce vnto lyfe.
Waliposikia haya hawakuwa na la kupinga zaidi. Nao wakamwadhimisha Mungu wakisema, “Basi, Mungu amewapa hata watu wa Mataifa toba iletayo uzima wa milele.”
19 They which were scattryd abroade thorow the affliccion that arose aboute Steven walked thorow oute tyll they came vnto Phenices and Cypers and Antioche preachynge ye worde to no man but vnto the Iewes only.
Basi wale waliotawanyika kwa ajili ya mateso yaliyotokana na kifo cha Stefano, wakasafiri hadi Foinike na Kipro na Antiokia. Nao hawakuhubiri lile Neno kwa mtu yeyote isipokuwa Wayahudi.
20 Some of them were men of Cypers and Syrene which when they were come into Antioche spake vnto the Grekes and preched the Lorde Iesus.
Lakini baadhi yao walikuwepo watu wa Kipro na Kirene, ambao walipokuja Antiokia walinena na Wayunani pia wakiwahubiria habari njema za Bwana Yesu.
21 And the honde of the Lorde was with them and a greate nombre beleved and turned vnto the Lorde.
Mkono wa Bwana ulikuwa pamoja nao, nayo idadi kubwa ya watu wakaamini na kumgeukia Bwana.
22 Tydinges of these thinges came vnto ye eares of the congregacion which was in Ierusalem. And they sente forth Barnabas that he shuld go vnto Antioche.
Habari hizi zilipofika masikioni mwa kanisa huko Yerusalemu, wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23 Which when he was come and had sene the grace of God was glad and exhorted them all that with purpose of hert they wolde continually cleave vnto ye Lorde.
Alipofika na kuona madhihirisho ya neema ya Mungu, akafurahi na kuwatia moyo waendelee kuwa waaminifu kwa Bwana kwa mioyo yao yote.
24 For he was a good man and full of the holy goost and of faythe: and moche people was added vnto the Lorde.
Barnaba alikuwa mtu mwema, aliyejaa Roho Mtakatifu, mwenye imani, nayo idadi kubwa ya watu wakaongezeka kwa Bwana.
25 Then departed Barnabas to Tarsus for to seke Saul.
Kisha Barnaba akaenda Tarso kumtafuta Sauli,
26 And when he had founde him he brought him vnto Antioche. And it chaunsed yt a whole yere they had their conversacion with the congregacio there and taught moche people: in so moche that the disciples of Antioche were the fyrst that were called Christen.
naye alipompata akamleta Antiokia. Hivyo kwa mwaka mzima Barnaba na Sauli wakakutana na kanisa na kufundisha idadi kubwa ya watu. Ilikuwa ni katika kanisa la Antiokia kwa mara ya kwanza wanafunzi waliitwa Wakristo.
27 In those dayes came Prophetes fro Ierusalem vnto Antioche.
Wakati huo manabii walishuka toka Yerusalemu hadi Antiokia.
28 And ther stode vp one of them named Agabus and signified by the sprete that ther shuld be great derth throughoute all the worlde which came to passe in ye Emproure Claudius dayes.
Mmoja wao, jina lake Agabo, akasimama akatabiri kwa uweza wa Roho Mtakatifu kwamba njaa kubwa itaenea ulimwengu mzima. Njaa hiyo ilitokea wakati wa utawala wa Klaudio.
29 Then the disciples every man accordinge to his abilite purposed to sende socoure vnto the brethren which dwelt in Iewry.
Mitume wakaamua kwamba kila mtu, kulingana na uwezo alio nao, atoe msaada kwa ajili ya ndugu wanaoishi Uyahudi.
30 Which thinge they also dyd and sent it to the elders by the hondes of Barnabas and Saul.
Wakafanya hivyo, misaada yao ikapelekwa kwa wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli.

< Acts 11 >