< John 4 >

1 Now, when the Master heard that the Pharisees had been told that he was making and baptizing more disciples than John
Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.
2 (Though it was not Jesus himself, but his disciples, who baptized),
(Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)
3 he left Judea, and set out again for Galilee.
Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;
4 He had to pass through Samaria,
na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
5 and, on his way, he came to a Samaritan town called Shechem, near the plot of land that Jacob gave to his son Joseph.
Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.
6 Jacob’s Spring was there, and Jesus, being tired after his journey, sat down beside the spring, just as he was. It was then about mid-day.
Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
7 A woman of Samaria came to draw water; and Jesus said to her — “Give me some to drink,”
Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, “Nipatie maji ninywe.”
8 For his disciples had gone into the town to buy food.
(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
9 “How is it,” replied the Samaritan woman, “that you who are a Jew ask for water from a Samaritan woman like me?” (For Jews do not associate with Samaritans).
Lakini huyo mwanamke akamwambia, “Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?” (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)
10 “If you knew of the gift of God,” replied Jesus, “and who it is that is saying to you ‘Give me some water,’ you would have asked him, and he would have given you ‘living water’.”
Yesu akamjibu, “Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: Nipatie maji ninywe, ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai.”
11 “You have no bucket, Sir, and the well is deep,” she said; “where did you get that ‘living water?’
Huyo mama akasema, “Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?
12 Surely you are not greater than our ancestor Jacob who gave us the well, and used to drink from it himself, and his sons, and his cattle!”
Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki.”
13 “All who drink of this water,” replied Jesus, “will be thirsty again;
Yesu akamjibu, “Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
14 but whoever once drinks of the water that I will give him shall never thirst any more; but the water that I will give him shall become a spring welling up within him — a source of Immortal Life.” (aiōn g165, aiōnios g166)
Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
15 “Give me this water, Sir,” said the woman, “so that I may not be thirsty, nor have to come all the way here to draw water.”
Huyo mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji.”
16 “Go and call your husband,” said Jesus, “and then come back.”
Yesu akamwambia, “Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa.”
17 “I have no husband,” answered the woman. “You are right in saying ‘I have no husband,’” replied Jesus,
Huyo mwanamke akamwambia, “Mimi sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli, kwamba huna mume.
18 “For you have had five husbands, and the man with whom you are now living is not your husband; in saying that, you have spoken the truth.”
Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli.”
19 “I see, Sir, that you are a Prophet!” exclaimed the woman.
Huyo Mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.
20 “It was on this mountain that our ancestors worshiped; and yet you Jews say that the proper place for worship is in Jerusalem.”
Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu.”
21 “Believe me,” replied Jesus, “a time is coming when it will be neither on this mountain nor in Jerusalem that you will worship the Father.
Yesu akamwambia, “Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22 You Samaritans do not know what you worship; we know what we worship, for Salvation comes from the Jews.
Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.
23 But a time is coming, indeed it is already here, when the true worshipers will worship the Father spiritually and truly; for such are the worshipers that the Father desires.
Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
24 God is Spirit; and those who worship him must worship spiritually and truly.”
Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake.”
25 “I know,” answered the woman, “that the Messiah, who is called the Christ, is coming; when once he has come, he will tell us everything.”
Huyo mama akamwambia, “Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu.”
26 “I am he,” Jesus said to her, “I who am speaking to you.”
Yesu akamwambia, “Mimi ninayesema nawe, ndiye.”
27 At this moment his disciples came up, and were surprised to find him talking with a woman; but none of them asked ‘What do you want?’ or ‘Why are you talking with her?’
Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: “Unataka nini?” au, “Kwa nini unaongea na mwanamke?”
28 So the woman, leaving her pitcher, went back to the town, and said to the people:
Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
29 “Come and see someone who has told me everything that I have done. Can he be the Christ?”
“Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?”
30 And the people left the town and went to see Jesus.
Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
31 Meanwhile the disciples kept saying to him: “Take something to eat, Rabbi.”
Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: “Mwalimu, ule chakula.”
32 “I have food to eat,” he answered, “of which you know nothing.”
Lakini Yesu akawaambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
33 “Can any one have brought him anything to eat?” the disciples said to one another.
Wanafunzi wake wakaulizana, “Je, kuna mtu aliyemletea chakula?”
34 “My food,” replied Jesus, “is to do the will of him who sent me, and to complete his work.
Yesu akawaambia, “Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
35 Do not you say that it still wants four months to harvest? Why, look up, and see how white the fields are for harvest!
Ninyi mwasema: Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika! Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.
36 Already the reaper is receiving wages and gathering in sheaves for Immortal Life, so that sower and reaper rejoice together. (aiōnios g166)
Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja. (aiōnios g166)
37 For here the proverb holds good — ‘One sows, another reaps.’
Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: Mmoja hupanda na mwingine huvuna.
38 I have sent you to reap that on which you have spent no labour; others have laboured, and you have entered upon the results of their labour.”
Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao.”
39 Many from that town came to believe in Jesus — Samaritans though they were — on account of the woman’s statement — ‘He has told me everything that I have done.’
Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: “Ameniambia mambo yote niliyofanya.”
40 And, when these Samaritans had come to Jesus, they begged him to stay with them, and he stayed there two days.
Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
41 But far more came to believe in him on account of what he said himself,
Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.
42 and they said to the woman: “It is no longer because of what you say that we believe in him, for we have heard him ourselves and know that he really is the Saviour of the world.”
Wakamwambia yule mama, “Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu.”
43 After these two days Jesus went on to Galilee;
Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.
44 for he himself declared that ‘a Prophet is not honoured in his own country.’
Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, “Nabii hapati heshima katika nchi yake.”
45 When he entered Galilee, the Galileans welcomed him, for they had seen all that he did at Jerusalem during the Festival, at which they also had been present.
Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
46 So Jesus came again to Cana in Galilee, where he had turned the water into wine. Now there was one of the King’s officers whose son was lying ill at Capernaum.
Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
47 When this man heard that Jesus had returned from Judea to Galilee, he went to him, and begged him to come down and cure his son; for he was at the point of death.
Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
48 Jesus answered: “Unless you all see signs and wonders, you will not believe.”
Yesu akamwambia, “Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!”
49 “Sir,” said the officer, “come down before my child dies.” And Jesus answered: “Go, your son is living.”
Huyo ofisa akamwambia, “Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa.”
50 The man believed what Jesus said to him, and went;
Yesu akamwambia, “Nenda tu, mwanao yu mzima.” Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
51 and, while he was on his way down, his servants met him, and told him that his child was living.
Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.
52 So he asked them at what time the boy began to get better. “It was yesterday, about one o’clock,” they said, “that the fever left him.”
Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, “Jana saa saba mchana, homa ilimwacha.”
53 By this the father knew that it was at the very time when Jesus had said to him ‘Your son is living’; and he himself, with all his household, believed in Jesus.
Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: “Mwanao yu mzima.” Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.
54 This was the second occasion on which Jesus gave a sign of his mission on coming from Judea to Galilee.
Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.

< John 4 >