< Romans 1 >
1 [I], Paul, who serve Christ Jesus, [am writing this letter]. God chose me to be an apostle, and I was appointed by him {he appointed me} in order that [I should proclaim] (the good message/the gospel) that [comes from him].
Paulo, mtumishi wa Yesu Kristo, aliyeitwa kuwa mtume, na kutengwa kwa ajili ya Injili ya Mungu.
2 Long before [Jesus came to earth, God] promised [that he would reveal] this good message by means of what his prophets [wrote] in the sacred Scriptures.
Hii ndio ile Injili aliyoiahidi zamani kupitia manabii wake katika maandiko matakatifu.
3 This good message is [about the one whom we know as] his Son. As to his Son’s physical/human nature, he was born a descendant of [King] David.
Ni kuhusu Mwana wake, aliyezaliwa kutoka ukoo wa Daudi kwa jinsi ya mwili.
4 As to his divine nature, it was shown {[God] showed} powerfully that he is (God’s own Son/the man who is also God). [God] showed this by his Holy Spirit causing him to become alive again after he died. He is Jesus Christ our Lord.
Yeye alitangazwa kwa Mwana wa Mungu kwa nguvu ya Roho ya utakatifu kwa ufufuo wa wafu, Yesu Kristo Bwana wetu.
5 He is the one who appointed me, who did not deserve it, [to be] an apostle. He did that in order that [many] among the non-Jews would honor [him] and would obey him as a result of their believing [my message about him].
Kupitia yeye tumepokea neema na utume kwa utii wa imani kati ya mataifa yote, kwa ajili ya jina lake.
6 You [believers] who are living in Rome [city] are included among those whom God has chosen to belong to Jesus Christ.
Kati ya mataifa haya, ninyi pia mmeitwa kuwa wa Yesu Kristo.
7 [I am writing this letter] to all of [you in Rome] whom God loves and whom he has chosen [to become his] people. [I pray that] God our Father and Jesus Christ our Lord will [continue to] act kindly toward you and [will continue to] cause you to have [inner] peace.
Barua hii ni kwa wote walioko Rumi, wapendwao na Mungu, walioitwa kuwa watu watakatifu. Neema na iwe kwenu, na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
8 As I begin [this letter], I thank my God for all you [believers in Rome]. It is because of [what] Jesus Christ [has done for us that] I [am able to do that]. I thank him because your trusting [in Jesus Christ] is something that people all over [the Roman Empire] [HYP] are talking about.
Kwanza, namshukuru Mungu wangu katika Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inahubiriwa katika dunia nzima.
9 God, whom I devotedly serve as I [proclaim to people] the gospel concerning his Son, knows that I tell the truth when I say that I always mention you whenever [DOU] I pray [to God] [HYP].
Kwa maana Mungu ni shahidi wangu, ambaye ninamtumikia kwa roho yangu katika injili ya Mwana wake, jinsi ninavyodumu katika kuwataja.
10 I especially ask God that if he desires [me to visit you], somehow at last I shall be able to do so.
Daima naomba katika sala zangu kwamba kwa njia yoyote nipate mwishowe kuwa na mafanikio sasa kwa mapenzi ya Mungu katika kuja kwenu.
11 [I pray this] because I long to visit you to help you spiritually, in order that you will become stronger [spiritually].
Maana natamani kuwaona, ili nipate kuwapa ninyi baadhi ya karama za rohoni, nipate kuwaimarisha.
12 I long to visit you in order that you and I might encourage each other [by means of our sharing with each other] how each of us trusts [in Jesus].
Yaani, natazamia kutiwa moyo pamoja nanyi, kwa njia ya imani ya kila mmoja wetu, yenu na yangu.
13 My fellow believers, many times I planned to visit you. I certainly want you to know [LIT] that. [But I have not been able to come to you because] I have been hindered {[things] have always prevented me} until the present time. I have wanted to come in order that I might help you to mature spiritually [IDM], as [I have helped people to mature spiritually] in many other non-Jewish groups [HYP].
Sasa ndugu, sitaki mkose kufahamu kwamba, mara nyingi nimekusudia kuja kwenu, lakini nimezuiliwa mpaka sasa. Nilitaka hivi ili kuwa na matunda kwenu kama ilivyo pia miongoni mwa watu wa mataifa.
14 I feel obliged [to proclaim the gospel to all non-Jewish people], specifically to [people who know] the Greek [language and culture] and to those who do not know it, to people who are educated and to those who are uneducated.
Nadaiwa na Wayunani na wageni pia, werevu na wajinga.
15 So what I have eagerly desired is that I might proclaim this good message to you who are living in Rome also.
Kwa hiyo, kwa upande wangu, mimi niko tayari kutangaza injili kwenu pia ninyi mlio huko Roma.
16 [That leads me to say that] I very confidently proclaim [LIT] the good message [about what Christ has done], because this good message is the powerful [means] that God [uses] to save [from the guilt of their sins] all people who trust [in what Christ has done for them]. Specifically, God first has saved the Jews [who believe the good message], and then he has saved non-Jews.
Kwa maana siionei haya injili, kwa kuwa ni uweza wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza na kwa Myunani pia.
17 By means of this good message God reveals how he erases the record of people’s sins (OR, declares people no longer guilty for having sinned); and his doing this is entirely because [IDM] they trust [in Christ. This is confirmed] by what [a prophet long ago] wrote [that God said], “Those (whose record of sin [I] have erased/whom [I] have declared no longer guilty for sin) because they trust [in me] will live [forever].”
Kwa maana haki ya Mungu imedhihirishwa kutoka imani hata imani, kama ilivyo andikwa, “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
18 From [where God rules in] heaven he is making it clear to all [non-Jewish] people who show no respect for God and who do wicked things, that he is angry with them [and that they deserve to be punished] {[that he would punish them]} [MTY]. By means of [their behaving] wickedly, they keep other people [from believing what they know] to be true [about God].
Maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi na uovu wote wa watu, ambao kwa njia ya udhalimu huificha kweli.
19 [Everyone] can clearly know what God [is like], because God himself has revealed to everyone [what he is like].
Hii ni kwa sababu, yote yanayoweza kujulikana juu ya Mungu ni wazi kwao. Maana Mungu amewafahamisha.
20 [People] cannot see what God is like. But ever since he created the world, by means of what he created he has clearly revealed what he is like. He has made clear to everyone that he has always been able to do very powerful things. [Therefore, we should recognize that] God is powerful, [completely different from all that he created]. So no one has a basis for saying, [“We never knew about God].” (aïdios )
Maana mambo yake yasioonekana vizuri yamekuwa wazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Yanaeleweka kupitia vitu vilivyoumbwa. Mambo haya ni uwezo wake wa milele na asili ya uungu. Matokeo yake, watu hawa hawana udhuru. (aïdios )
21 Although [the non-Jews] knew what God [is like], they did not honor him as God, nor did they thank [him for what he had done]. But instead, they began to think foolish [things about him], and they became unable to understand [MET] [what he wanted them to know].
Hii ni kwa sababu, ingawa walijua kuhusu Mungu, hawakumtukuza yeye kama Mungu, wala hawakumpa shukrani. Badala yake, wamekuwa wapumbavu katika mawazo yao, na mioyo yao yenye ujinga ilitiwa giza.
22 Although they claimed that they were wise, they became foolish,
Walijiita kuwa ni werevu, lakini wakawa wajinga.
23 and they refused to [admit that] God is glorious and will never die. Instead, they made and worshipped idols [that resembled people who] will some day die, and [then they made other idols that resembled] birds and four-footed animals, and [finally] they made idols that resembled reptiles.
Waliubadili utukufu wa Mungu asie na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya ndege, ya wanyama wenye miguu minne, na ya viumbe vitambaavyo.
24 So God allowed [the non-Jews] do immoral sexual things that they [SYN] strongly desired, things [that their desires were compelling them to do]. As a result, they [began to] dishonor each other’s bodies [by their sexual actions].
Kwa hiyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa za mioyo yao kwa uchafu, kwa miili yao kufedheheshwa baina yao.
25 Also, they [chose to worship] false [gods] instead (of admitting/of choosing to believe) what is true [about] God. They worshipped and served things [that God] created instead of [worshipping and serving God himself], the one who created [everything. They did this even though] he [deserves that those he created] would forever praise him. Amen!/May it be so! (aiōn )
Ni wao walioibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, na ambao waliabudu na kutumikia viumbe badala ya Muumbaji, ambaye anasifiwa milele. Amina. (aiōn )
26 So, God allowed [the non-Jews to do] shameful [sexual] things that they [strongly] desired. As a result, many women did not have natural sexual relations [with their husbands] [EUP]. Instead, they were doing sexual actions with other women [EUP].
Kwa sababu hii, Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, kwa kuwa wanawake wao walibadilisha matumizi yao ya asili kwa kile kilicho kinyume na asili.
27 Similarly, [many] men stopped having/did not have natural sexual relations with women [EUP]. Instead, they strongly desired to have sexual relations with other men. They committed [homosexual] acts with other men, acts that were shameful. As a result, [God has] punished them [by sicknesses] in their bodies, which is what they deserve [because] they [thought] wrongly [that God would not punish them for doing that].
Hali kadhalika, wanaume pia wakaacha matumizi yao ya asili kwa wanawake na kuwakwa na tamaa dhidi yao wenyewe. Hawa walikuwa wanaume ambao walifanya na wanaume wenzao yasiyo wapasa, na ambao walipokea adhabu iliyostahili upotovu wao.
28 Furthermore, because they decided that it was not [worthwhile] to know God, he allowed their own worthless thoughts [to completely control them]. As a result, they began doing [evil] things that [God says that people] should not do.
Kwa sababu walikataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wafanye mambo yale yasiyofaa.
29 They strongly desire to do all [kinds of] unrighteous [things]. They strongly desire to do all [kinds of] evil things [to others]. They strongly desire to possess things that [belong to others]. They strongly desire to harm [others] in various ways. [Many non-Jews] are constantly envying [other people. Many] constantly desire to murder [people. Many] constantly desire to cause strife [between people. Many] constantly desire to deceive [others. Many] constantly desire to speak hatefully [about others] (OR, [to speak harmful things about others, things that are not true]). [Many] gossip [about others].
Wamejawa na udhalimu wote, uovu, tamaa na ubaya. Wamejawa na wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu, na nia mbaya.
30 [Many] slander [others. Many] act especially hatefully toward God. [Many] speak or act in an insulting way [toward others. Many] treat others contemptuously. [Many] boast [about themselves to others. Many] invent new ways to do evil things. [Many non-Jewish children] disobey their parents.
Wao pia ni wasengenyaji, wasingiziaji, na wenye kumchukia Mungu. Wenye vurugu, kiburi, na majivuno. Wao ni watunga mabaya, na wasiotii wazazi wao.
31 [Many non-Jews] act in other morally foolish ways. [Many] do not do what they promised [others that they would do. Many] do not [even] love [their own family members. And many] do not act mercifully [toward other people].
Wao hawana ufahamu; wasioaminika, hawana mapenzi ya asili, na wasio na huruma.
32 Although they know that God has declared that those who do such things deserve to be killed, they not only habitually do these [kinds of evil] things, but they also approve of others who habitually do them.
Wanaelewa kanuni za Mungu, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo wanastahili kifo. Lakini si tu wanafanya mambo hayo, wao pia wanakubaliana na wale wanaofanya mambo hayo.