< Revelation 9 >
1 The fifth angel blew his trumpet. Then I saw [an evil angel. He was like] a star that had fallen from the sky to the earth. He was given {[Someone] gave him} the key to the shaft [that descended] ([to] the underworld/[to] the deep dark pit). (Abyssos )
Malaika wa tano akaipiga tarumbeta yake, nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka toka angani hadi ardhini. Nyota hiyo ilipewa ufunguo wa lile Shimo. (Abyssos )
2 When he opened that shaft, smoke arose from it like smoke from a huge burning furnace. The smoke prevented [anyone from seeing] the sky and the light of the sun. (Abyssos )
Alipolifungua hilo Shimo, moshi ukapanda kutoka humo kama moshi wa tanuru kubwa sana. Jua na anga vikatiwa giza na ule moshi uliotoka katika hilo Shimo. (Abyssos )
3 Locusts came out of the smoke onto the earth. [They were given] {[God] gave them} power [to sting people], like scorpions [sting people].
Ndipo katika ule moshi wakatoka nzige wakaenda juu ya nchi, nao wakapewa nguvu kama zile za nge wa duniani.
4 [God] told the locusts that they should not harm grass, nor any plants, nor any tree. [God said that they should harm only] those people who did not have a mark on the forehead [to show that they belonged to God].
Wakaambiwa wasidhuru nyasi ya nchi, wala mmea wala mti wowote, bali wawadhuru tu wale watu ambao hawana muhuri wa Mungu kwenye vipaji vya nyuso zao.
5 [God] did not allow the locusts to kill those people. Instead, [he] allowed them to continue torturing people for five months. When they tortured people, the pain those people felt was like the pain a scorpion causes when it stings someone.
Wakaruhusiwa kuwatesa kwa muda wa miezi mitano, lakini wasiwaue. Uchungu wa kuuma kwao ulikuwa kama ule wa mtu aumwapo na nge.
6 During the time [when the locusts torture rebellious people, the pain will be so bad that] people will want to find a way to die, but they will not be able to [PRS].
Katika siku hizo watu watatafuta kifo lakini hawatakiona, watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia.
7 The locusts looked like horses that are ready for battle. They had on their heads what looked like golden crowns. Their faces were like the faces of people.
Wale nzige walikuwa na umbo kama la farasi waliotayarishwa kwa ajili ya vita. Kwenye vichwa vyao kulikuwa na kitu kama taji za dhahabu na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
8 They had [long] hair like the [long] hair of women. Their teeth were [strong], like lions’ teeth.
Walikuwa na nywele kama za wanawake, na meno yao yalikuwa kama ya simba.
9 They wore metal breastplates. [When they were flying], their wings made a noise like the roar when many horses [pull chariots as they are] rushing into battle.
Walikuwa na dirii kama za chuma, na sauti za mabawa yao zilikuwa kama ngurumo za farasi wengi na magari mengi yakikimbilia vitani.
10 They had tails like scorpions have. With their tails they stung [people] for five months.
Walikuwa na mikia yenye miiba ya kuumia kama nge. Nguvu yao ya kutesa watu kwa huo muda wa miezi mitano ilikuwa katika hiyo mikia yao.
11 The king who ruled over them was the angel of the underworld. His name in the Hebrew language is Abaddon. In the Greek language it is Apollyon. [Both of] those names [mean ‘Destroyer’]. (Abyssos )
Walikuwa na mfalme wao, ambaye ni malaika wa lile Shimo, ambaye jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kiyunani ni Apolioni. (Abyssos )
12 That was the end of the first terrible event. [Be aware that] two tragic events are still to come.
Ole ya kwanza imepita, bado nyingine mbili zinakuja.
13 The sixth angel blew his trumpet. Then I heard a voice from the four corners of the golden altar that is in God’s presence.
Malaika wa sita akaipiga tarumbeta yake, nami nikasikia sauti ikitoka katika zile pembe za madhabahu ya dhahabu iliyoko mbele za Mungu.
14 It was saying to the sixth angel, the one who had the trumpet, “Release the four angels whom [I] have bound at the great river Euphrates!”
Ile sauti ikamwambia yule malaika wa sita mwenye tarumbeta, “Wafungulie wale malaika wanne waliofungwa kwenye ule mto mkubwa Frati.”
15 The four angels were released, those who had been {[He] released the four angels, whom [God] had} kept ready for that [exact] hour of that day, of that month, of that year. They were released {[He] released them} in order that they might enable [their soldiers to] kill a third of the [rebellious] people.
Basi wale malaika wanne, waliokuwa wamewekwa tayari kwa ajili ya saa hiyo, na siku hiyo, na mwezi huo, na mwaka huo ili wawaue theluthi ya wanadamu wakafunguliwa.
16 The number of the soldiers riding on horses who did that was 200 million. I heard [someone say] how many there were.
Idadi ya majeshi wapanda farasi ilikuwa 200,000,000. Nilisikia idadi yao.
17 In the vision I saw what the horses and the [beings] that rode them looked like. They [wore] breastplates that were [red] like fire, [dusky blue] like smoke, and [yellow] like sulfur. The heads of the horses were like the heads of lions. From their mouths came fire, smoke, and [fumes of burning] sulfur.
Hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika maono yangu: Wapanda farasi walivaa dirii vifuani zenye rangi nyekundu sana kama ya moto na yakuti samawi na kiberiti. Vichwa vya hao farasi vilikuwa kama vichwa vya simba, na moto, moshi na kiberiti vilitoka vinywani mwao.
18 Those three things—the fire, the smoke, and the [burning] sulfur from [the horses’] mouths—killed a third of the [rebellious] people.
Theluthi ya wanadamu wakauawa kwa mapigo hayo matatu, yaani, huo moto, moshi na kiberiti, vilivyotoka kwenye vinywa vya hao farasi.
19 The horses had power with their mouths and with their tails. Their tails have heads like snakes by which they harm people.
Nguvu za hao farasi zilikuwa katika vinywa vyao na kwenye mikia yao, kwa sababu mikia yao ilikuwa kama nyoka, yenye vichwa ambayo waliitumia kudhuru.
20 The rest of the [rebellious] people, those who were not killed by these plagues of [fire and smoke and burning sulfur], did not turn from their sinful behavior. [They did not stop worshipping] the idols that they had made with their own hands. They did not stop worshipping demons and idols [that were made] of gold, of silver, of bronze, of stone, and of wood, [even though they are idols] that can neither see nor hear nor walk.
Wanadamu waliosalia, ambao hawakuuawa katika mapigo hayo, bado walikataa kutubia kazi za mikono yao na hawakuacha kuabudu mashetani na sanamu za dhahabu, za fedha, za shaba, za mawe na za miti, ambazo haziwezi kuona, kusikia wala kutembea.
21 They did not stop murdering people, or practicing sorcery, or acting in sexually immoral ways, or stealing [things].
Wala hawakutubu na kuacha matendo yao ya uuaji, uchawi, uasherati wala wizi wao.