< Revelation 19 >
1 After these things I heard [what sounded] like a huge crowd in heaven. They were shouting things like, “(Hallelujah!/Praise our God!)” “He has saved us!” “He is glorious and mighty!”
Baada ya mambo haya nilisikia sauti kama ya mlio mkubwa wa kundi kubwa la watu mbinguni ikisema, “Haleluya. Wokovu, utukufu, na nguvu ni vya Mungu wetu.
2 “Praise him because he judges truly and justly!” “He has punished the very evil cities that are like a prostitute, because their people persuaded the other people of earth [MTY] to act immorally and idolatrously like they do.” “Praise him because he has punished them for murdering his servants [MTY]!”
Hukumu zake ni kweli na za haki, kwa kuwa amemhukumu kahaba mkuu aliyeiharibu nchi kwa uzinzi wake. Amefanya kisasi kwa damu ya watumishi wake, ambayo aliimwaga yeye mwenyewe.”
3 [The crowd] shouted a second time saying: (Hallelujah!/Praise God!) The smoke of the fire that is burning the cities will rise forever! (aiōn )
Kwa mara ya pili walisema, “Haleluya! Moshi hutoka kwake milele na milele.” (aiōn )
4 The 24 elders and the four living [creatures] (prostrated themselves/knelt down) and worshipped God, who sits on the throne. Then they said, “[It] is true! (Hallelujah!/Praise God!)”
Wale wazee ishirini na wanne na viumbe hai wanne wakasujudu na kumwabudu Mungu akaaye kwenye kiti cha enzi. Walikuwa wakisema, “Amina. Haleluya!”
5 Someone spoke from the throne and said, “All you who are our God’s servants, praise him! All you who reverence him, [whether you are socially] significant or insignificant, praise him! [Everyone]!”
Ndipo sauti ilitoka kwenye kiti cha enzi, ikisema, “Msifuni Mungu wetu, enyi watumishi wake wote, ninyi mnaomcha yeye, wote wasio na umuhimu na wenye nguvu.”
6 I heard something like the noise of a huge crowd [of people], like the sound of a huge waterfall (OR, a great/wide river of rushing water), and like the sound of loud thunder. They were shouting: (Hallelujah!/Praise God!) Because the Lord God, the Almighty One, reigns!
Ndipo nilisikia sauti kama sauti ya kundi kubwa la watu, kama sauti ya ngurumo ya maji mengi, na kama ngurumo ya radi, ikisema, “Haleluya! Bwana ni Mungu wetu, mtawala juu ya wote, hutawala.
7 We should rejoice, we should be extremely glad, and we should honor him, because it is now time for Jesus, the one who is like a lamb, to be united permanently with his people, which will be like a man [MET] marrying his bride, and because those who belong to him have prepared themselves to be united with him.
Na tushangilie na kufurahi na kumpa utukufu kwa sababu harusi na sherehe ya Mwana Kondoo imekuja, na bibi harusi yuko tayari.”
8 God has permitted them to be completely pure, like a bride who [MET] dresses in fine linen that is bright and clean. Fine [bright and clean] linen represents the righteous acts of God’s people.
Aliruhusiwa kuvalishwa kitani safi na yenye kung'aa (kitani safi ni matendo ya haki ya waumini).
9 Then the angel said to me, “Write [this: God will abundantly] bless the people who are {whom [he] has} invited to the feast [that celebrates Jesus, the one who is like a] lamb, [permanently uniting with his people, like someone] [MET] [marrying a wife].” He also said [to me]: “These words that God [declares] are true!”
Malaika akasema nami, “Yaandike haya: Wamebarikiwa walioalikwa kwenye sherehe ya harusi ya Mwana kondoo.” Vilevile akaniambia, “Haya ni maneno ya kweli ya Mungu.”
10 I [immediately] (prostrated myself/knelt down) at his feet in order to worship him. But he said to me, “Do not [worship me]! I am [just] your [(sg)] fellow servant and the fellow servant of your [(sg)] fellow believers who tell people about Jesus. God is the one whom you should worship, because it is the Spirit of God who gives people the power to tell others about Jesus (OR, [those who tell others about] Jesus are [truly] declaring [the words that the Spirit of God has given them])!”
Nilisujudu mbele ya miguu yake nikamwabudu, lakini akaniambia, “Usifanye hivi! Mimi ni mtumishi mwenzako na wa ndugu zako mwenye kuushika ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu, kwa kuwa ushuhuda wa Yesu ni roho ya unabii.”
11 [In the vision] I saw heaven opened {open}, and I was surprised to see a white horse. [Jesus], the one who was riding on the horse, is called ‘Trustworthy and Genuine/True’. He judges [all people according to] what is right, and fights righteously [against his enemies].
Kisha niliona mbingu zimefunguka, na tazama kulikuwa na farasi mweupe! Na yule aliyekuwa amempanda anaitwa Mwaminifu na wa Kweli. Huhukumu kwa haki na kufanya vita.
12 His eyes [shone like] [MET] a flame of fire. There were many royal crowns on his head. A name had been written [on him]. Only he knows [the meaning of that name].
Macho yake ni kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake ana taji nyingi. Ana jina lililoandikwa juu yake asilolifahamu mtu yeyote isipokuwa yeye mwenyewe.
13 The robe he was wearing was drenched with blood. His name is [also] “(The one who expresses what God is like/The Word of God).”
Amevaa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aliitwa Neno la Mungu.
14 The armies of heaven were following him. [They were also] riding on white horses. They were wearing clothes [made of] clean white linen.
Majeshi ya mbinguni yalikuwa yakimfuata juu ya farasi weupe, walivalishwa kitani nzuri, nyeupe na safi.
15 [The words] that Jesus speaks [are like] [MTY] a sharp sword with which he will strike [the rebellious people of] the nations. He himself will rule them [powerfully, as though he had] [MET] an iron rod. He will crush [his enemies just like] [MET] [a person crushes grapes in a] winepress. [He will do this for] God Almighty, who is extremely angry [with them because of their sins].
Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao huyaangamiza mataifa, naye atawatawala kwa fimbo ya chuma. Naye hukanyaga vyombo vya mvinyo kwa hasira kali ya Mungu, hutawala juu ya wote.
16 On his cloak close to his thigh a name had been written {[he] had written a name}, which is “King who [rules over all other] kings and Lord who [rules over all other] lords.”
Naye ameandikwa juu ya vazi lake na katika paja lake jina, MFALME WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA.
17 I saw an angel who was standing in [the light of] [MTY] the sun. He called loudly to all the [flesh-eating] birds flying high in the sky, “Come and gather for the wonderful feast that God [is providing for you]!
Niliona malaika amesimama katika jua. Aliwaita kwa sauti kuu ndege wote warukao juu, “Njoni, kusanyikeni pamoja kwenye chakula kikuu cha Mungu.
18 [Come] and eat the flesh of all [God’s enemies who are dead—] the flesh of kings, army commanders, [people who fought] powerfully, horses and the [soldiers] who rode them, [and the flesh of all other kinds of people], whether [they were] free or slaves, [socially] insignificant or significant. [All kinds]!”
Njoni mle nyama ya wafalme, nyama ya majemedari, nyama ya watu wakubwa, nyama ya farasi na wapanda farasi, na nyama ya watu wote, walio huru na watumwa, wasio na umuhimu na wenye nguvu.”
19 Then I saw the beast and the kings of earth with their armies gathered together to fight against the Rider on the horse, and against his army.
Nilimwona mnyama na wafalme wa nchi pamoja na majeshi yao. Walikuwa wamejipanga kwa ajili ya kufanya vita na mmoja aliyepanda farasi na jeshi lake.
20 The beast and the false prophet were captured {[He] captured the beast and the false prophet}. The false prophet is the one who had performed miracles in the beast’s presence. By doing that he had deceived the people who had accepted the beast’s mark [on their foreheads] and who worshipped its image. The beast and the false prophet were thrown {[He] threw the beast and the one who falsely said that he spoke messages that came directly from God} alive into the lake of fire that burns with sulfur. (Limnē Pyr )
Mnyama alikamatwa na nabii wake wa uongo aliyezifanya ishara katika uwepo wake. Kwa ishara hizi aliwadanganya wale walioipokea chapa ya mnyama na walioisujudia sanamu yake. Wote wawili walitupwa wangali hai katika ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. (Limnē Pyr )
21 The rider on the horse killed the rest [of their armies] just by [speaking words], [which were like] [MTY] a sword that extended from his mouth. All those birds gorged themselves on the flesh of [the people whom he had killed].
Wale waliobaki waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa mmoja aliyepanda juu ya farasi. Ndege wote walikula mizoga ya miili yao.