< Revelation 11 >
1 [An angel gave] to me a reed similar to a measuring stick. He said [to me], “[Christ says this: ‘Go] to the temple [where people worship] God, measure it and the altar [in it], and count the people who worship there.
Kisha nikapewa mwanzi uliokuwa kama kijiti cha kupimia, nikaambiwa, “Inuka, ukalipime Hekalu la Mungu, madhabahu ya kufukizia ubani, na ukawahesabu watu wanaoabudu ndani ya Hekalu.
2 But do not measure the courtyard outside [of the temple] [DOU], because [it] has been given {[God] has given it} to [the] non-Jewish [people. As a result], they will trample [Jerusalem city] for 42 months.
Lakini uache ukumbi ulio nje ya Hekalu; usiupime, maana huo umekabidhiwa watu wa mataifa mengine, ambao wataukanyanga mji Mtakatifu kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
3 I will appoint my two (witnesses/men who will tell others about me). They will proclaim what I reveal to them for 1,260 days. They will wear [rough] clothes made from goat’s hair [to show that they are sad about people’s sin].’”
Nami nitawatuma mashahidi wangu wawili ili watangaze ujumbe wa Mungu kwa muda huo wa siku elfu moja mia mbili na sitini wakiwa wamevaa mavazi ya magunia.”
4 Those [witnesses are the ones] that are represented by the two olive trees and the two lampstands that are in the presence of the Lord [who rules] the earth [SYM].
Hao mashahidi wawili ni miti miwili ya Mizeituni na taa mbili zinazosimama mbele ya Bwana wa dunia.
5 If enemies try to harm those [witnesses], fire will come from the mouths of the witnesses and destroy them. If people want to harm them, [the two witnesses] will certainly kill them similarly.
Kama mtu akijaribu kuwadhuru, moto hutoka kinywani mwao na kuwaangamiza adui zao; na kila mtu atakayejaribu kuwadhuru atakufa namna hiyo.
6 Those [witnesses] will have authority to keep rain from falling during the time that they are proclaiming what God reveals to them. They also will have authority to cause water [everywhere] to become [red like] [MET] blood, and [authority] to cause all kinds of plagues to occur. They will do this as often as they want to.
Hao wanayo mamlaka ya kufunga anga, mvua isinyeshe wakati wanapotangaza ujumbe wa Mungu. Tena wanayo mamlaka ya kuzigeuza chemchemi zote za maji ziwe damu, na ya kusababisha maafa ya kila namna duniani kila mara wapendavyo.
7 When they have finished proclaiming [to people the message from God], the beast that comes up (from the underworld/from the deep dark pit) will attack them, overcome them, and kill them. (Abyssos )
Lakini wakisha maliza kutangaza ujumbe huo, mnyama atokaye shimoni kuzimu atapigana nao, atawashinda na kuwaua. (Abyssos )
8 The dead bodies of the [two] witnesses will lie in the street of the great city where their Lord was crucified, the city that is symbolically named Sodom or Egypt [because its people are very evil, like the people who lived in Sodom and Egypt].
Maiti zao zitabaki katika barabara za mji mkuu ambapo Bwana wao alisulubiwa; jina la kupanga la mji huo ni Sodoma au Misri.
9 Individuals of many people-[groups], tribes, language [groups] [MTY], and nations will look at their dead bodies for three and a half days. But these individuals will not allow [anyone] to bury their bodies.
Watu wa kila kabila, lugha, taifa na rangi wataziangalia maiti hizo kwa muda wa siku tatu na nusu, na hawataruhusu zizikwe.
10 When the [rebellious] people who live on the earth [see that the witnesses are dead], they will rejoice and celebrate. They will send gifts to each other, because these two prophets had [caused plagues to occur which] tormented the [rebellious] people on the earth.
Watu waishio duniani watafurahia kifo cha hao wawili. Watafanya sherehe na kupelekeana zawadi maana manabii hawa wawili walikuwa wamewasumbua mno watu wa dunia.
11 But after three and a half days, God will cause those two witnesses to breathe again and live. They will stand up, and those who see them will be terrified.
Lakini baada ya zile siku tatu na nusu pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu iliwaingia, nao wakasimama; wote waliowaona wakaingiwa na hofu kuu.
12 The [two witnesses] will hear a loud voice which came from heaven saying to them: “Come up here!” Then they will go up to heaven in a cloud. Their enemies will see them [as they ascend].
Kisha hao manabii wawili wakasikia sauti kubwa kutoka mbinguni ikiwaambia, “Njoni hapa juu!” Nao wakapanda juu mbinguni katika wingu, maadui wao wakiwa wanawatazama.
13 At that same time there will be a terrible earthquake, which will cause a tenth of [the buildings in] [MTY] the city will collapse, and 7,000 people will die. The rest of the people will be afraid and [acknowledge] that the God [who rules in] heaven is awesome.
Wakati huohuo, kukatokea tetemeko kubwa la ardhi, sehemu moja ya kumi ya ardhi ikaharibiwa. Watu elfu saba wakauawa kwa tetemeko hilo la ardhi. Watu waliosalia wakaogopa sana, wakamtukuza Mungu wa mbinguni.
14 That will be the second terrible event. [Be aware that] the third tragic event will happen soon.
Maafa ya pili yamepita; lakini tazama! Maafa ya tatu yanafuata hima.
15 Then the seventh angel blew [his trumpet]. Angels in heaven shouted loudly, “Our Lord [God] and the Messiah [whom he has appointed] can now govern [everyone in] [MTY] the world, and they will continue to rule people forever!” (aiōn )
Kisha malaika wa saba akapiga tarumbeta yake. Na sauti kuu zikasikika mbinguni zikisema, “Sasa utawala juu ya ulimwengu ni wa Bwana wetu na Kristo wake. Naye atatawala milele na milele!” (aiōn )
16 The 24 elders who sit on their thrones in God’s presence (prostrated themselves/bowed down low) and worshipped him.
Kisha wale wazee ishirini na wanne walioketi mbele ya Mungu katika viti vyao vya enzi, wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu,
17 They said: Lord God, you are the Almighty One! You are the one who exists now! You are the one who has always existed! We thank you that you have defeated by your power everyone who has rebelled against you, and you now rule over everyone in the world.
wakisema: “Bwana Mungu Mwenye uwezo, uliyeko na uliyekuwako! Tunakushukuru, maana umetumia nguvu yako kuu ukaanza kutawala!
18 The unbelieving people of [MTY] the nations were raging at you. As a result you have become very angry with them. You have decided that this is the appropriate time for you to judge all the dead people. You have also decided that it is the time for you to reward all your servants, both the prophets and the rest of your people who reverence you [MTY], whether they were considered socially significant/important or socially insignificant/unimportant. It is time for you to reward all of them! You have also decided it is the time for you to destroy the people who are destroying others on the earth.
Watu wa mataifa waliwaka hasira, maana wakati wa ghadhabu yako umefika, wakati wa kuwahukumu wafu. Ndio wakati wa kuwatuza watumishi wako manabii, watu wako na wote wanaolitukuza jina lako, wakubwa kwa wadogo. Ni wakati wa kuwaangamiza wale wanaoangamiza dunia.”
19 Then God’s temple in heaven was opened {was open} and [I] saw in the temple the sacred box/chest that contains God’s commandments. Lightning was flashing, it was thundering and rumbling, the earth shook, and large hailstones [fell from the sky].
Hekalu la Mungu mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana Hekaluni mwake. Kisha kukatokea umeme, sauti, ngurumo, tetemeko la ardhi, na mvua kubwa ya mawe.