< Psalms 73 >

1 God truly is good to [us] Israeli people, to those who totally want to do all that God desires.
Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
2 As for me, I almost [stopped trusting in God]; [it was as though] my feet slipped and I stumbled [MET],
Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
3 because I envied those who proudly [said that they did not need God], and I saw that they prospered [even though] they were wicked.
kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
4 Those people do not have any pains; they are [always] strong and healthy.
Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
5 They do not have the troubles/difficulties that other people have; they do not have problems like others do.
Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
6 So they are proud, and their being proud is [like] a necklace [that they show to others], and they show off their violent actions like people show off their beautiful robes.
Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
7 From their inner beings they (pour out/do) evil deeds, and they are always thinking about more evil things to do.
Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
8 They scoff at [other people], and they talk about doing evil things to them; they are proud while they plan to oppress others.
Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
9 They say evil things about [God who is in] heaven [MTY], and they talk boastfully/proudly about things [that they have done] here on the earth.
Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
10 The result is that people listen to what they say and praise them and do not think that they have done anything that is wrong.
Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
11 Wicked people say [to themselves], “God will certainly not [RHQ] know [what we have done]; [people say that] he is greater than any other god, but he does not know [everything].”
Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
12 That is what wicked people are like; they never worry about anything, and they are always becoming richer.
Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
13 [So, God], I think it is useless that I have [RHQ] always done what you want me to, and that I have not sinned.
Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
14 All day long I have problems, and every morning you punish me.
Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
15 If I had said the things that the wicked people say, I would have been sinning against your people.
Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
16 And when I tried to think about all this, it was very difficult for me [to understand it].
Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
17 But when I went to your temple, [you spoke to me], and I understood what will happen to the wicked people [after they die].
Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
18 [Now I know that] you will surely put them in slippery places, and they will fall down and die.
Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
19 They will be destroyed instantly; they will die in terrible ways.
Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
20 They [will disappear as quickly] as a dream disappears when a person awakes in the morning; Lord, when you arise, you will (cause them to disappear/forget all about them).
Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
21 When I felt sad/bitter, and brokenhearted,
Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
22 I was stupid and ignorant, and I behaved like an animal toward you.
Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
23 But I am always close to you, and you hold my hand.
Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
24 You guide me by teaching me, and (at the end [of my life]/when I die), you will receive me and honor me.
Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
25 You are in heaven and I belong to you [RHQ], and there is nothing on this earth that I desire more than that.
Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
26 My body and my mind may become very weak, but God, you continue to enable me to be strong; I belong to you forever.
Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
27 Those who remain far from you will be destroyed; you will get rid of those who abandon you.
Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 But [as for] me, it is wonderful to be near to God and to be protected by Yahweh, and to proclaim to others all that he has done [for me].
Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.

< Psalms 73 >