< Psalms 52 >
1 You people [think that you] are strong and brag about the sins that you have committed, while you plan to harm godly people.
Kwa nini wewe unajivunia kufanya uovu, wewe mtu mwenye nguvu? Uaminifu wa agano la Mungu huja kila siku.
2 All during the day you plan to get rid of [others]; what you say [MTY] [injures others] like a sharp razor [SIM], and you are [always] deceiving [others].
Ulimi wako hupanga uharibifu kama wembe mkali, na kufanya udanganyifu.
3 You like [doing what is] evil more than you like doing what is good, and you like telling lies more than you like telling the truth.
Wewe unapenda uovu kuliko wema na udanganifu kuliko kuongea haki. (Selah)
4 You who say things [MTY] to deceive people, you like to say (things that hurt people/cruel things)!
Wewe hupenda maneno ambayo huwaumiza wengine, wewe ulimi mdanganyifu.
5 But God will get rid of you forever; he will grab you and drag you from your home and take you away from this world where people are alive.
Vivyo hivyo Mungu atakuadhibu wewe milele; yeye atakuchukua na kukuondoa katika hema yako na kukung'oa katika ardhi ya uhai. (Selah)
6 When righteous [people] see that, they will be awestruck, and they will laugh at [what happened to] you, and say,
Wenye haki pia wataona na kuogopa; watamcheka na kusema,
7 “Look [what happened to] the man who would not ask God to protect him; he trusted that his great wealth [would save him]; he trusted in the money that he got by wickedly taking it from others!”
“Tazama, huyu ni mtu ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake la usalama, bali aliamini katika wingi wa mali zake, naye alikuwa na nguvu alipowaharibu wengine.”
8 But I am [secure/safe because I worship] in God’s temple; I am like a [strong] green olive tree. I trust in God, who faithfully loves us forever.
Lakini kwangu mimi, niko kama mti bora wa mzeituni katika nyumba ya Mungu; Nami nitaamini uaminifu wa agano la Mungu milele na milele.
9 God, I will always thank you for the things that you have done. As I stand before godly [people], I will proclaim that you are good (OR, the many good [MTY] [things you have done for us]).
Nitakushukuru wewe daima kwa uliyo tenda. Nitalisubiri jina lako, kwa sababu ni zuri, uweponi mwa wantu wako wa kimungu.