< Psalms 45 >
1 In my inner being I am stirred by a beautiful message which will be sung to the king. The words of this message will be written with a pen by me, a skilled writer.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
2 [O King], you are the most handsome man in the world, and you always speak [MTY] eloquently, because God has always blessed you.
Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
3 You who are a mighty warrior, put on your sword! You are glorious and majestic.
Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
4 Ride on like a great chief to defend the truth that you speak and the fair decisions that you make! Because you are strong [MTY], you will do awesome deeds.
Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
5 Your arrows are sharp, and they pierce the hearts of your enemies. Soldiers of many nations will fall dead at your feet.
Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
6 The kingdom [MTY] that God will give to you will remain forever. You rule [MTY] people justly.
Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
7 You love right actions, and you hate evil actions. Therefore God, your God, has chosen [MTY] you [to be king] and caused you to be happier [MET] than any other king.
Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
8 The perfume of various spices is on your robes. [People] (entertain you/make you happy) in ivory palaces by playing stringed instruments.
Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
9 Among the women who stay near you [EUP] stay are daughters of [other] kings. And at your right hand stands [your bride], the queen, wearing beautiful ornaments of gold that comes from Ophir.
Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
10 [Now I will say something] to your bride: Listen to me carefully [DOU]! Forget the people who live in your home country, forget your relatives!
Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
11 Because you are [very], the king will desire [to sleep with] [EUP] you. He is your master, so you must obey him.
Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
12 The people from Tyre [city] will bring gifts to you; their rich people will try to persuade you to do favors for them.
Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
13 [O king], your bride will be entering the palace wearing beautiful robes made from gold thread.
Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
14 While she is wearing a gown that has many colors, her companions will lead her to you. She will have many other young women who accompany her.
Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
15 They will be very joyful [DOU] as they are led along to enter your palace.
Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
16 Some day, your sons and your grandsons will become kings, just like your ancestors were. You will enable them to become rulers in many countries [HYP].
Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
17 And as for me, I will enable people in every generation to remember the great things that you [MTY] have done, and people will praise you forever.
Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.