< Psalms 34 >
1 I will always thank Yahweh; I will constantly praise him [MTY].
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2 I will boast about what Yahweh [has done]. All those who are oppressed/discouraged should hear me and rejoice.
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
3 Join with me in telling others that Yahweh is great! You and I should together proclaim how glorious he is!
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4 I prayed to Yahweh, and he (answered my prayer/did what I asked him to do); he rescued me from [all those who caused me] to be afraid.
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5 Those who trust [IDM] that he [will help them] will be joyful; (they will never be disappointed/he will always do for them the things that he promises) [LIT].
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6 I was miserable/helpless, but I called out to Yahweh, and he heard me. He rescued me from all my troubles.
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
7 An angel from Yahweh guards those who revere him, and the angel rescues them.
Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
8 Find out for yourself, and you will experience that Yahweh is good to you! He is very pleased with those who ask him to protect them.
Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
9 All you who belong to him, revere him! Those who do that will always have the things that they need [LIT].
Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
10 Lions [are usually] very strong, [but sometimes] even young lions are hungry and become weak, but those who trust in Yahweh will (have everything/not lack any good thing) [LIT] [that they need].
Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
11 You (who are my students/whom I teach), come and listen to me, and I will teach you how to revere Yahweh.
Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
12 If [RHQ] any of you wants to enjoy life and have a good long life,
Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
13 do not say anything that is evil! Do not tell lies!
basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
14 Turn away from doing evil, and do what is good! Always try hard to enable people to live peacefully [with each other.]
Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
15 Yahweh [MTY] carefully watches over those who [act] righteously; he always responds [MTY] to them when they call [to him for help].
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16 But Yahweh [SYN] (is opposed to/turns away from) those who do what is evil. [And after they die], people will forget them completely.
Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17 Yahweh hears righteous people when they call out to him; he rescues them from all their troubles.
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18 Yahweh is always ready to help those who are discouraged; he rescues those who have nothing good to hope for.
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Righteous people may have many troubles, but Yahweh rescues them from all those troubles.
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20 Yahweh protects them from being harmed; [when their enemies attack them], they will not break any bones of those righteous people.
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21 Wicked people will be killed by their own evil deeds (OR, by [people doing to them] the same evil things [that the wicked do to others]) [PRS], and Yahweh will punish those who oppose righteous people.
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22 Yahweh will save those who serve him. He will (not condemn/forgive) [LIT] those who trust in him.
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.