< Psalms 26 >
1 Yahweh, show that I (am innocent/have not done what is wrong). I always do what is right; I have trusted in you and never doubted [that you would help me].
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
2 Yahweh, examine what I have done and test me; thoroughly evaluate what I think [IDM].
Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
3 I never forget that you faithfully love me, I conduct my life according to your truth.
kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
4 I do not spend my time with liars and I stay away from hypocrites.
Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
5 I do not like to be with evil people, and I avoid wicked people.
ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
6 Yahweh, I wash my hands to show that I (am innocent/have not done what was wrong). As I join with others marching around your altar,
Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
7 we sing songs to thank you, and we tell others the wonderful things that you [have done].
nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
8 Yahweh, I love [to be in] the temple where you live, in the place where your glory appears.
Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
9 Do not get rid of me like you get rid of sinners; do not cause me to die like you cause those who murder [MTY] people to die,
Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
10 and people who [SYN] are ready to do wicked things and people who are always taking bribes.
ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
11 But as for me, I always try to do what is right. So be kind to me and rescue me.
Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
12 I stand in places where I am safe, and when [all your people] gather together, I praise you.
Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.