< Psalms 146 >

1 Praise Yahweh! With my whole inner being I will praise Yahweh.
Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
2 I will praise Yahweh as long as I am alive; I will sing to praise my God for [the rest of] my life.
Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
3 [You people], do not trust in your leaders; do not trust humans because they cannot save/rescue you [from your difficulties/problems].
Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
4 And when they die, their corpses [decay and] become soil again. After they die, they can no longer do the things that they planned to do.
Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
5 But those whose helper is the God whom Jacob [worshiped] are happy. The one whom they confidently expect [to help them] is Yahweh, their God.
Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
6 He is the one who created heaven and the earth and the oceans and all [the creatures] that are in them. He always does what he has promised to do.
Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
7 He decides matters fairly for those who are (treated unfairly/oppressed), and he provides food for those who are hungry. He frees those who are in prison.
Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
8 Yahweh enables those who are blind to see again. He lifts up those who have fallen down. He loves righteous [people].
Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
9 Yahweh takes care of those from other countries who live in our land, and he helps widows and orphans. But he gets rid of wicked [people].
Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
10 Yahweh will [continue to] be our king forever; you people of Israel, your God will rule forever! Praise Yahweh!
Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.

< Psalms 146 >