< Psalms 138 >

1 Yahweh, I thank you with all my inner being. I sing to praise you in front of [the idols of false] gods [to ridicule/belittle them].
Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
2 I bow down while I look towards your sacred temple, and I thank you [MTY] because you faithfully love [us] and faithfully do all that you have promised. You have shown that both you [MTY] and what you have promised to do are greater than anything else.
Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
3 On the day when I called out to you, you answered me; you enabled me to be strong and brave.
Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
4 Yahweh, [some day] all the kings of this earth will praise you, because they will have heard what you have said.
Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
5 They will sing about what you have done; they will sing and say that you are very great.
Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
6 Yahweh, you are supreme, but you take care of people [who are considered to be] unimportant. And you know what proud people [are doing], even though they are far away [from you and think that you do not see them].
Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
7 When I am in the midst of [many] troubles/difficulties, you save/rescue me. With your hand/power [MTY] you rescue me from my enemies who are angry at me.
Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
8 Yahweh, you will do for me everything that you promised; you faithfully love [us] forever. Finish what you started to do [for us, your Israeli people.]
Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.

< Psalms 138 >