< Psalms 120 >
1 When I had troubles, I called out to Yahweh and he answered me.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 [I prayed], “Yahweh, rescue/save me from people [SYN, MTY] who lie to me and [try to] deceive me!”
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 You people who lie to me, [I will tell you] [RHQ] what [God] will do to you and what he will do to punish you.
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 He will shoot sharp arrows at you like soldiers do, and he will [burn you with] red-hot coals from [the wood of] a broom tree.
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 It is terrible for me, living among cruel/savage [DOU] people [like those who live] in Meshech [region] and Kedar [region].
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 I have lived for a long time among people who hate [to live with others] peacefully.
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 Every time I talk about living together peacefully, they talk about starting a war.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.