< Psalms 106 >

1 Praise Yahweh! Praise Yahweh, because he does good things [for us]; he faithfully loves [us] forever/continually!
Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 [Because Yahweh has done many great things], no one can [RHQ] tell all the great things that Yahweh has done, and no one can praise him enough/sufficiently.
Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
3 (Happy are/He is pleased with) those who act fairly/justly, with those who always do what is right.
Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
4 Yahweh, be kind to me when you help your people; help me when you rescue/save them.
Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
5 Allow me to see it when your people become prosperous again and when [all the people of] your nation, [Israel], are happy; allow me to be happy with them! I want to praise you along with [all] those [others] who belong to you.
Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
6 We and our ancestors have sinned; we have done things that were very wicked [DOU].
Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
7 When our ancestors were in Egypt, they did not pay attention to the wonderful things that Yahweh did; they forgot about the many times that he showed that he faithfully loved them. Instead, when they were at the Red Sea, they rebelled against God, who is greater than any other god.
Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
8 But he rescued them for the sake of his own [reputation] in order that he could show that he is very powerful.
Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
9 He rebuked the Red Sea and it became dry, and [then] while he led our ancestors across it, they walked through it as though it were as dry as a desert [SIM].
Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
10 In that way he rescued them from the power [MTY] of their enemies who hated them [DOU].
Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
11 [Then] their enemies were drowned in the water [of the Red Sea]; not one of them was left.
Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
12 When that happened, our ancestors believed [that Yahweh had truly done for them] what he had promised to do, and they sang to praise him.
Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
13 But they soon forgot what he had done for them; they [did things] without waiting to find out what Yahweh wanted them to do.
Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
14 They intensely wanted [food like they formerly ate in Egypt]. They [did evil things to] find out [if they could do those things without God punishing them].
Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
15 [So] he gave them what they requested, but he [also] caused a terrible disease to afflict them.
Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
16 [Later] when [some of] the men became jealous of Moses and [his older brother] Aaron, who was dedicated [to serve Yahweh by being a priest],
Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
17 the ground opened up and swallowed Dathan and [also] buried Abiram and his family.
Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
18 And [God sent] a fire down [from heaven] which burned up [all] the wicked [people who (supported them/agreed with) them].
Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
19 Then the [Israeli leaders] made a gold statue at Sinai [Mountain] and worshiped it.
Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
20 Instead of worshiping [our] glorious God, they [started to] worship a statue of a bull that eats grass!
Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
21 They forgot about God, who had rescued them by the great miracles that he performed in Egypt.
Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
22 They forgot about the wonderful things that he did for them in Egypt and the amazing/awesome things that he did for them at the Red Sea.
Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
23 Because of that, God said that he would get rid of the Israelis, but Moses, whom God had chosen [to serve him], pleaded with God [not to get rid of them]. And as a result God did not destroy them.
Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
24 [Later], our ancestors (refused/were afraid) to enter beautiful [Canaan] land because they did not believe [that God would enable them to take the land from the people who were living there, as] he had promised.
Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
25 They stayed in their tents and grumbled and would not pay attention to what Yahweh said that they should do.
bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
26 So he solemnly [MTY] told them that he would cause them to die [there] in the desert,
Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
27 and that he would scatter their descendants among the [people of other] nations/people-groups [who did not believe in him], and that he would allow them to die in those lands.
akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
28 Later the Israeli people [started to] worship [the idol of] Baal [who they thought lived] at Peor [Mountain], and they ate [meat that had been] sacrificed to [Baal and those other] lifeless gods.
Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
29 Yahweh became [very] angry because of what they had done, [so again] he sent a terrible disease to attack/strike them.
Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
30 But Phinehas stood up and punished/killed [the ones who had sinned greatly], and as a result the (plague/serious disease) ended.
Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
31 People have remembered that righteous thing that Phinehas did, and in future years people will remember it.
Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
32 [Then] at Meribah Springs our ancestors caused Yahweh to become angry, and as a result Moses had trouble.
Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
33 They caused Moses to become very angry [IDM], and he said things that were foolish.
Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
34 Our ancestors did not destroy the people [who did not believe in Yahweh] like he told them to do.
Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
35 Instead, they mingled with people from those people-groups, and they started to do the evil things that those people did.
bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
36 Our ancestors worshiped the idols of those people, which resulted in their being destroyed/exiled/taken to another country [MET].
nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
37 [Some of] the Israelis sacrificed their sons and daughters to the demons [that those idols represented].
Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
38 They killed [MTY] their own children, who (were innocent/had not done things that were wrong), and offered them as sacrifices to the idols in Canaan. [As a result], Canaan land was polluted by those murders [MTY].
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
39 So by their deeds they caused themselves to become unacceptable to God; [because they did not faithfully worship only God], [they became like] women who sleep with other men [instead of sleeping only with their husbands] [MET].
Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
40 So Yahweh became very angry with his people; he was completely disgusted with them.
Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
41 [As a result] he allowed people-groups [who did not believe in him] to conquer them, so those who hated our ancestors started to rule over them.
Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
42 Their enemies (oppressed them/treated them cruelly) and completely controlled them [MET].
Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
43 Many times Yahweh rescued them, but they continued to rebel against him, and they were finally destroyed because of the sins that they committed.
Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
44 However, Yahweh [always] heard them when they cried out to him; he listened to them when they were distressed.
Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
45 For their sake, he thought about the agreement/promise that he had made [to bless] them, and because he never stopped loving them very much, he changed his mind [about punishing them more].
Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
46 He caused all those who had taken the Israelis [to Babylonia] to (feel sorry for/pity) them.
Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
47 Yahweh our God, rescue/save us and bring us back [to Israel] from among those people-groups in order that we may thank you [MTY] and joyfully praise you.
Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
48 Praise Yahweh, the God whom [we] Israelis [worship], praise him now and forever! And I want everyone to say, “Amen/May it be so!” Praise Yahweh!
Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.

< Psalms 106 >