< Proverbs 20 >
1 Drinking a lot of wine or [other] strong drinks causes people to start fighting; it is foolish to become drunk/intoxicated.
Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
2 Being afraid of a king when he is angry is like [SIM] being afraid of a lion when it growls/roars; if you cause the king to become angry, he may execute you.
Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
3 [People] respect those who stay away from disputes/arguments; foolish people [love to] quarrel.
Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
4 [If] a lazy man does not plow [his fields at the right/proper time], he will look for [crops] at harvest [time], but there will be nothing there.
Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
5 [Just] as it is difficult to bring up water from a deep well, it is difficult to know what people are thinking, but someone who has good sense/insight will be able to find out what people are thinking.
Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
6 Many people proclaim that they can be trusted [to do what they say that they will do], but it is very difficult to find [RHQ] someone who can really be trusted.
Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
7 If parents conduct their lives as they should, [God] blesses their children (OR, their children are very happy/fortunate).
Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
8 A king who sits on his throne to judge people can [easily] [MTY] find out what things that people have done are good and what things are evil.
Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
9 There is no one [RHQ] who can truthfully say, “I do not know of any wrong things that I have done; I have (gotten rid of all my sinful behavior/quit doing what is sinful).”
Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
10 Yahweh detests people who use weights that are not right and measures that are not correct.
Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
11 Even children show by what they do whether they are good or not; they show whether (what they do/their behavior) is honest and right [or not].
Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
12 Two of the things that Yahweh has created [for us] are ears to hear things and eyes to see things.
Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
13 If you want to sleep [all the time], you will become poor; if you stay awake [and work], you will have plenty of food.
Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
14 People [look at things that they are about] to buy, [and in order to get it for a lower price sometimes they] say, “(It is no good/It is poor quality),” but [after they buy it], they go and boast [about having bought it for a cheap price].
“Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
15 Gold and precious stones are [valuable], but wise words [MTY] are more valuable.
Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
16 If you foolishly promise to a stranger that you will pay what he owes if he is unable to pay it [DOU], [you deserve to] have someone take your coat from you.
Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
17 People [may] think that food that they acquire by doing what is dishonest will taste very good, but later [they will not enjoy what they have done any more than they would enjoy] eating gravel/sand.
Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
18 When people give you good advice, [if you do what they suggest], your plans will succeed; so be sure to get good advice from wise people before you start fighting a war.
Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
19 Those who go around telling gossip are [always] telling secrets to [others]; so stay away from people who foolishly talk [too much].
Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
20 If someone curses his father or his mother, his life will be ended, [just] like a lamp is extinguished.
Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
21 If you very quickly take the property that your parents promise will be yours after they die, you will not receive any good/blessing from it.
Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
22 Do not say, “I will do evil to those who do evil to me;” wait for Yahweh [to do something about it], and he will (help you/[do what is right]).
Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
23 Yahweh detests [those who use] dishonest scales and weights that are not accurate/correct.
Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
24 Yahweh is the one who has decided what will happen to us, so (how can we (understand/know) what will happen before it happens?/we humans certainly cannot (understand/know) what will happen before it happens.) [RHQ]
Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
25 You should think carefully before you solemnly promise to dedicate something to God, because later you might be sorry you have promised to do it.
Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
26 Wise kings find out [MET] which people have done what is wrong, and they punish them very severely [IDM].
Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
27 Our consciences are [like] lamps that Yahweh [has given to us to enable us to know what we are thinking] [MET]; they reveal what is hidden deep in our (minds/inner beings).
Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
28 Kings will continue to rule as long as they faithfully love their people and are loyal to them and as long as they rule righteously/fairly.
Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
29 We honor/admire young people because they are strong, but we respect [MTY] old people more because they are wise.
Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
30 When we are beaten or whipped, it [can] cause us to quit doing what is evil in our lives; when someone wounds us [by punishing us], it [can] cause our behavior to become good.
Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.