< Proverbs 10 >

1 These [are more] proverbs/wise sayings from Solomon: If children are wise, they cause their parents to be happy; but if children are foolish, they cause their parents to be very sad.
Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
2 Money that you get by doing dishonest/wicked things will really not benefit you; but by living righteously you will live for (a long time/many years).
Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
3 Yahweh does not allow righteous [people] to starve, but he will prevent wicked [people] from getting what they want.
Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
4 Lazy people [soon] become poor; it is those who work hard who become rich.
Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
5 Those who are wise, harvest the crops when they are ripe; it is shameful/disgraceful to sleep [and not work] during harvest time.
Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
6 Righteous [people will] be blessed [by God]; [the nice things] that wicked [people] say [MTY] [sometimes] conceal the fact that they [are planning to] act violently.
Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
7 After righteous [people die], other people are blessed as they remember [what those people did before they died]; but we will soon forget wicked people [MTY] after they die.
Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
8 Wise people heed good instruction/advice, but people who talk foolishly will ruin themselves.
Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
9 Honest people will be safe, but [others] (OR, God) will find out those who are dishonest.
Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
10 Those who signal with their eyes [that they are about to do something that is wrong] cause trouble, but those who rebuke others truthfully cause them to be peaceful.
Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
11 What righteous [people] say [MTY] is [like] a fountain that (gives life/enables people to live many years) [MET], but what wicked [people] say [MTY] hides [the fact] that they intend to act violently.
Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
12 When we hate others, it causes quarrels, but if we love others, we forgive them [for the wrong things that they do].
Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
13 Those who have good sense say [MTY] what is wise, but people who do not have good sense must be punished.
Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
14 Wise people continue to learn all that they can, but when foolish people speak, they soon cause trouble.
Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
15 The wealth that rich people have [protects them like a city is protected by a] strong wall around it [MET], but people who are poor suffer much [because they have no one to help them].
Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
16 If you are righteous, your reward will be a good life, [but] all that sinful people gain is to sin more.
Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
17 Those who pay attention when others try to (correct them/teach them what they are doing that is wrong) will live (happily/for many years); but those who reject being rebuked will not find the road to life (OR, cause others to go astray).
Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
18 Those who will not admit that they hate [others] are liars, and those who slander [others] are foolish.
Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
19 When people talk a lot, that will lead them to sin a lot [by what they say]; if you are wise, you will refuse to say very much.
Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
20 What righteous/good [people] say [MTY] is [as valuable as] pure silver [MET]; what wicked [people] think is worthless.
Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
21 What righteous [people] say [MTY] benefits many [people], but foolish people die because of the stupid [things that they do].
Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
22 Yahweh blesses [some people] by enabling them to become rich, and working hard will not make them to become richer (OR, and he will not also cause them to become sad).
Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
23 Foolish people (have fun/enjoy) doing what is wrong, but wise/sensible people enjoy doing what is wise.
Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
24 Righteous [people] will get the good things that they want/desire, but what wicked [people] are afraid of is what will happen to them.
Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
25 When storms come, the wicked will (be blown away/never be safe), but righteous [people will] be safe forever.
Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
26 We do not like a lazy person who refuses to do the job that he is given to do, [just] like we do not like vinegar in our mouths or smoke in our eyes.
Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 If you revere Yahweh, you will live for a long time; but wicked [people] die before they become old.
Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
28 Righteous [people] confidently expect [that good things will happen to them], and that causes them to be happy/joyful; but when wicked [people] confidently expect something good to happen, it does not happen.
Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
29 Yahweh protects [MET] those who live righteously, but he destroys those who do what is evil.
Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
30 Righteous [people] will always be secure [LIT], but wicked people will be removed from their land (OR, from this earth).
Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
31 Righteous people [MTY] say things that are wise, but [God] will shut the mouths of people [MTY] who say what is not true.
Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
32 Righteous people [MTY] know what to say that is acceptable, but wicked [people] [MTY] are [constantly] saying things that are not true.
Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.

< Proverbs 10 >