< Numbers 9 >

1 One year after the Israelis left Egypt, during the month of March, while they were in the Sinai Desert, Yahweh said to Moses/me,
Bwana akasema na Mose katika Jangwa la Sinai katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka Misri. Akasema,
2 “Tell the Israeli people that they must celebrate the Passover [Festival again].
“Waamuru Waisraeli waadhimishe Pasaka katika wakati ulioamriwa.
3 They must do it on the fourteenth day of this month, early in the evening, and they must obey all the instructions about it [that I gave you previously].”
Adhimisheni wakati ulioamriwa, yaani wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi huu, kufuatana na desturi zake zote na masharti yake.”
4 So Moses/I told the people what Yahweh had said about celebrating the Passover.
Hivyo Mose akawaambia Waisraeli waiadhimishe Pasaka,
5 The people celebrated it, there in the Sinai Desert, in the evening of the fourteenth day of the month, just as Yahweh had commanded Moses/me.
nao wakafanya hivyo kwenye Jangwa la Sinai wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza. Waisraeli wakafanya kila kitu kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
6 But some of the Israeli people had touched a corpse, and as a result they had become unfit to celebrate the Passover. So they asked Aaron and Moses/me,
Lakini baadhi yao hawakuweza kuadhimisha Pasaka siku ile kwa sababu walikuwa najisi kwa taratibu za kiibada kwa ajili ya kugusa maiti. Kwa hiyo wakamwendea Mose na Aroni siku ile ile,
7 “It is true that we have touched a corpse. But why should that prevent us from celebrating the Passover Festival and offering sacrifices to Yahweh like everyone else [RHQ]?”
wakamwambia Mose, “Tumekuwa najisi kwa sababu tumegusa maiti, lakini kwa nini tuzuiliwe kumtolea Bwana sadaka yake pamoja na Waisraeli wengine katika wakati ulioamriwa?”
8 Moses/I replied, “Wait here until I go into the Sacred Tent and find out what Yahweh says about it.”
Mose akawajibu, “Ngojeni mpaka nitafute kile Bwana anachoagiza kuwahusu ninyi.”
9 [So Moses/I went into the tent and asked Yahweh what he/I should tell the people], and this is what Yahweh said:
Ndipo Bwana akamwambia Mose,
10 “Tell this to the Israeli people: If any of you or your descendants touch a corpse and as a result become unacceptable to me, or if you are away from home on a long trip [at the time to celebrate the Passover], you will still be permitted to celebrate it.
“Waambie Waisraeli: ‘Wakati mmoja wenu au wazao wenu wanapokuwa najisi kwa sababu ya maiti au wakiwa safarini, hata hivyo wanaweza kuadhimisha Pasaka ya Bwana.
11 But you must celebrate it exactly one month later, early in the evening of the fourteenth day of that month. Eat the meat of the lamb for the Passover Festival with bread that is baked without yeast and eat bitter herbs.
Wataiadhimisha wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Watamla mwana-kondoo, pamoja na mkate usiotiwa chachu, na mboga chungu.
12 Do not leave any of it until the next morning. And do not break any of the lamb’s bones. Obey all the regulations about celebrating the Passover.
Wasibakize chochote hadi asubuhi wala wasivunje mifupa ya mwana-kondoo. Wakati wanapoadhimisha Pasaka, hawana budi kufuata masharti yote.
13 But if any of you has not done anything that would make you unfit to celebrate the Passover Festival, and you are not away from home on a long trip, and you do not sacrifice to me at the proper time, you will no longer be allowed to associate with my people. (You will be punished/I will punish you).
Lakini kama mtu ni safi kwa taratibu za kiibada naye hayuko safarini, asipoadhimisha Pasaka, mtu huyo hana budi kukatiliwa mbali na watu wake kwa sababu hakutoa sadaka ya Bwana kwa wakati ulioamriwa. Mtu huyo atawajibika kubeba matokeo ya dhambi yake.
14 Foreigners who live among you may also celebrate the Passover Festival, if they obey all my commands concerning it.”
“‘Mgeni anayeishi miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana, lazima afanye hivyo kwa kufuata desturi na masharti. Lazima masharti yawe sawasawa kwa mgeni na mzawa.’”
15 On the day that the Sacred Tent was set up, a cloud covered it. From the time that the sun set until the time that the sun rose [the next day], the cloud resembled a [huge] fire. And that is what happened every day [that we/the Israelis were in the desert].
Katika siku hiyo ambayo Maskani, Hema la Ushuhuda, iliposimamishwa, wingu liliifunika. Kuanzia jioni mpaka asubuhi wingu lililokuwa juu ya Maskani lilionekana kama moto.
Hivyo ndivyo lilivyoendelea kuwa; wingu liliifunika wakati wa mchana, na usiku lilionekana kama moto.
17 When the cloud rose up and started to move [to a new location], we/they followed it. When the cloud stopped, we/the Israelis stopped there and set up their tents.
Wakati wowote wingu lilipoinuka kutoka juu ya Hema, nao Waisraeli waliondoka; mahali popote wingu liliposimama, Waisraeli walipiga kambi.
18 We/They traveled when Yahweh, [by causing the cloud to move or stop], signaled to us/them when to move and when to stop. When the cloud stayed over the Sacred Tent, we/the Israelis stayed at that place.
Kwa amri ya Bwana Waisraeli waliondoka, na kwa amri yake walipiga kambi. Kwa muda wote wingu liliposimama juu ya Maskani, Waisraeli walibaki wamepiga kambi.
19 Sometimes the cloud stayed over the tent for a long time, so when that happened, we/they did not travel.
Wakati wingu lilipobaki juu ya Maskani kwa muda mrefu, Waisraeli walitii amri ya Bwana nao hawakuondoka.
20 Sometimes the cloud remained over the tent for only a few days. We/The people stopped and set up our/their tents as Yahweh commanded us/them, and we/they traveled [to a new location] when Yahweh commanded us/them to do that.
Wakati mwingine wingu lilikuwa juu ya Maskani kwa siku chache tu; kwa amri ya Bwana wangelipiga kambi na kisha kwa amri yake wangeliondoka.
21 Sometimes the cloud stayed in one place for only one day. When that happened, when the cloud rose up [into the sky] the next morning, then we/they traveled. Whenever the cloud moved, during the day or during the night, we/they traveled.
Wakati mwingine wingu lilikuwepo kuanzia jioni mpaka asubuhi tu, na lilipoinuka asubuhi, nao waliondoka. Ikiwa ni mchana au usiku, wakati wowote wingu lilipoinuka, waliondoka.
22 If the cloud stayed over the Sacred Tent for two days, or for a month, or for a year, during that time we/they stayed where we/they were. But when the cloud rose up [into the sky], we/they started to travel.
Ikiwa wingu lilikaa juu ya Maskani kwa siku mbili au mwezi au mwaka, Waisraeli wangebaki wamepiga kambi na hawakuondoka; lakini lilipoinuka, wangeondoka.
23 When Yahweh commanded us/them to [stop and] set up our/their tents, we/they did that. When he told us/them to move, we/they moved. We/They did whatever Yahweh told Moses/me that we/they should do.
Kwa amri ya Bwana walipiga kambi, na kwa amri ya Bwana waliondoka. Walitii amri ya Bwana, kufuatana na agizo lake kupitia Mose.

< Numbers 9 >