< Numbers 5 >
1 Yahweh said to Moses/me,
BWANA alinena na Musa. Akasema,
2 “Tell this to the Israeli people: ‘You must send away from your (camp/area where you have your tents) any man or woman who has leprosy and anyone who has a discharge [of some fluid from his body], and anyone who has become unacceptable to God because of [having touched] a corpse.
“Waamuru wana wa Israel wawatoe watu wote wenye magonjwa ya ngozi yanayoambukiza, na kila mwenye mwenye vidonda vinavyotoa harufu, na ambaye amenajisika kwa kugusa maiti.
3 Send them away from there in order that they will not [touch people in the camp area] where I live among you and cause them to become unacceptable to me.’”
Awe mme au mke, umtoa kambini. Ili wasije wakaitia unajisi kambi, kwa sababu Mimi huishi ndani yake,”
4 So [Moses/I told that to the Israeli people, and] the Israeli people obeyed what Yahweh commanded Moses/me.
Watu wa Israeli walifanya hivyo. Waliwatoa kambini, Kama BWANA alivyomwagiza Musa. Watu wa Israeli walimtii BWANA.
5 Yahweh also told Moses/me,
Tena BWANA akanena na Musa. Akasema,
6 “Tell this to the Israeli people: ‘If someone (commits a crime against/does something wrong to) another person, [I consider that] that person has done wrong to me.
“Nena na wana wa Israeli. mtu mume na mtu mke akifanya dhambi yeyote ambayo watu hufanyiana wao kwa wao, na mtu huyo akamwasi BWANA, mtu huyo atakuwa na hatia.
7 That person must confess that he or she is guilty, and he or she must pay to the person to whom wrong was done [what others consider to be a suitable/proper payment] for what he has done, and he must pay an extra 20 percent.
Ndipo huyo mtu ataungama hiyo dhambi aliyoifanya. Mtu huyo atarudisha malipo ya hatia yake na kuongeza kwenye malipo hayo sehemu ya tano zaidi. Atamlipa huyo aliyemtendea makosa
8 If the person against whom the wrong was done [has died and] there is no relative to whom the money can be paid, then the money belongs to me, and it must be paid to the priest. In addition, the one who did the wrong must give a male sheep to the priest [to sacrifice] in order that (that person’s sin may be forgiven/I can forgive that person for his sin).
Lakini kama huyo mtu huyu aliyetendewa kosa hana ndugu wa kupokea hayo malipo, basi atalipa hayo malipo ya hatia kwangu kupitia kuhani pamoja na kondoo dume kwa ajili ya sadaka yake mwenyewe.
9 All the sacred offerings that the Israelis bring to the priest belong to the priest.
Kila sadaka ya wana wa Israeli, vitu ambavyo vimetengwa na vikaletwa kwa kuhani na watu wa Israeli, vitakuwa vyake.
10 The priest can keep those gifts.’”
Sadaka ya kila mtu itakuwa ya kuhani; kama mtu yeyote atatoa kitu chochote kwa kuhani, kitakuwa chake.”
11 Yahweh also said this to Moses/me:
Tena BWANA akanena na Musa. Akasema,
12 “Tell this to the Israeli people: ‘Suppose a man thinks that his wife has slept with another man,
“Nena na wana wa Israel. Uwaambie, 'kama mke wa mtu ataasi na kufanya dhambi dhidi ya mume wake.
13 but neither he nor anyone else knows if it is true or not, because no one saw her doing that.
Halafu mtu mwingine akalala naye. Kwa sababu, hiyo atakuwa amenajisika. Na hata kama mume wake hakuona na hajui, hata kama hakuna mtu aliyemkamta akiwa katika tendo na hakuna mtu wa kushuhudia dhidi yake; hata hivyo ile roho ya wivu itaendele kumjulisha yule mume kuwa mke wake amenajisika.
14 But if the woman’s husband is jealous, and if he suspects that she has committed adultery, and he wants to know whether that is true or not,
Ingawa, roho ya wivu inaweza kumdanganya yule mwanamume wakati mke wake hajanajisika.
15 he should take his wife to the priest. He must take along as an offering two quarts/liters of barley flour. The priest must not pour [olive] oil or incense on it, because this is an offering that the man has brought because he (is jealous/wants his wife to sleep only with him). It is an offering to find out if she is guilty or not. [Neither olive oil nor incense should be used because are associated with joy and this is not a time for joy.]
Kwa mazingira hayo, yule mwanamume anapaswa kumpeleka mke wake kwa kuhani. Yule mwanamume anapaswa kutoa sadaka ya divai kwa ajili yake. Atapaswa kuleta sehemu ya kumi ya efa ya unga wa shayiri. Asitie mafuta juu yake wala asitie ubani juu yake maana ni sadaka ya unga ya wivu, ni sadaka ya unga ya ukumbusho wa uovu.
16 The priest must tell the woman to stand [in front of the altar] in my presence.
Ndipo kuhani atasogeza karibu na kumweka mbele ya BWANA.
17 He must put some sacred water in a clay jar, and then he must put some dirt from the floor of the Sacred Tent into the water.
Kuhani atachukua kikombe cha maji matakatifu na atachukua mavumbi ya kwenye masikani. Ataweka yale mavumbi kwenye maji.
18 He must untie/unfasten the woman’s hair. Then he must put in her hands the grain that her jealous husband is offering to determine whether she has committed adultery or not. The priest must hold [the bowl that contains] bitter water that will cause (the woman to be cursed/bad things to happen to the woman) [if she is guilty].
Kisha kuhani atamweka huyo mwanamke mbele za BWANA na atazifungua nywele kichwani kwa huyo mwanamke. Atamwekea mikononi mwake hiyo sadaka ya unga kwa ajili ya ukumbusho, ambayo ni sadaka ya unga kwa ajili ya wivu.
19 The priest must require her to solemnly declare [that she will tell the truth]. Then he must say to her, “Has another man had sex [EUP] with you? Have you faithfully [slept only with your husband] or not? If you have not slept with another man, nothing bad will happen to you if you drink the water.
Kuhani atashikilia mikononi mwake maji machungu yanayoweza kuleta laana. Kuhani atamweka huyo mwanamke chini ya kiapo na kumwambia. 'Kama haujafanya uzinzi na mwanaume mwingine, na kama hajakengeuka na kufanya uovu, basi utakuwa huru na maji haya yanayoweza kuleta laana.
20 But if you have had sex with another man, [Yahweh will curse you].
Lakini kama wewe, mwanamke uliye chini ya mume wako, umekengeuka, na kama umenajisika, na kama mwanamume mwingina amelala nawe,
21 Your womb will shrivel up and your stomach will swell up. You will never be able to give birth to children, and as a result, everyone will curse you and avoid you. If you have committed adultery, [when you drink] this water, that is what will happen to you.” Then the woman must answer, “[If I am guilty], I will not object if that happens.”
ndipo, (kuhani atamtaka huyo mwanamke aape kiapo kinachoweza kuleta laana kwake, na kwamba ataendelea kumwambia yule mwanamke) 'BWANA atakufanya wewe kuwa laana itakayooneshwa kuwa hivyo kwa watu wako. Hii itatokea pale BWANA atakapoyafanya mapaja yako kuoza na tumbo lako kuvimba.
Haya maji ambayo huleta laana yataingia tumboni mwako na kulifanya tumbo lako kuvimba na mapaja yako kuoza,' mwanamke alitakiwa kujibu, 'Ndiyo, hayo yanipate kama mimi ni mwenye hatia.'
23 ‘Then the priest must write [with ink] on a small scroll these (curses/bad things that will happen to her if she is guilty) [and then wash the ink off into the bitter water].
Naye kuhani ataziandika laana hizi kwenye kitabu, na kisha kuzifuta laana zilizoandikwa kwa maji ya uchungu.
24 The priest must take from her the offering of barley flour [that she is holding], and lift it up to dedicate it to me. Then he must put it on the altar
Naye kuhani atamwelekeza yule mwanamke kunywa yale maji machungu yaletayo laana. Yale maji yaletayo laana yataingia na kuwa machungu.
Kuhani ataitwaa ile sadaka ya unga ya wivu mikononi mwa yule mwanamke. Atailekeza ile sadaka ya unga mbele ya BWANA na kuileta madhabahuni.
26 and burn part of it as a sacrifice. Then the woman must drink the bitter water.
Kuhani atachukua konzi ya sadaka ya unga mkononi mwake kama sadaka ya kuwakilisha, na kuiteketeza madhabahuni. Ndipo atakapompatia mwanamke yale maji machungu ili ayanywe.
27 If the woman has committed adultery, the water will cause her to suffer greatly. Her stomach will swell up and her womb will shrink, [and she will be unable to give birth to children]. And then her (relatives/fellow Israelis) will curse her.
Wakati wa kumpa yale maji ili anywe, kama amenajisika kwa sababu alifanya uovu dhidi ya mume wake, ndipo yale maji yaletayo laana yatamwingia na kuwa machungu. Tumbo lake litavimba na paja lake litaoza. Yule mwanamke atalaaniwa kati ya watu wake.
28 But if she (is innocent/has not committed adultery), her body will not be harmed, and she will still be able to give birth to children.
Lakini kama yule mwanake hajanajisika na kama ni msafi, basi atakuwa huru. Tena ataweza kubeba uja uzito.
29 ‘That is the ritual that must be performed when a woman who is married has been unfaithful to her husband,
Hii ndiyo sheria ya wivu. Ni sheria ya mwanamke anayekengeuka kwa mumewe na kunajisika.
30 or when a man is jealous and suspects that his wife [has had sex with another man]. The priest must tell that woman to stand [at the altar] in my presence and obey these instructions.
Ni sheria ya mwanamume mwenye roho ya wivu kwa mkewe. Atamleta mwanamke mbele ya BWANA, na kuhani atamfanyia huyo mwanamke kila kitu ambacho sheria ya wivu inamtaka kufanya.
31 Even if the woman has not done what the husband suspected, he will not be punished [MTY] for doing something wrong [by bringing his wife to the priest]. But if his wife is guilty, she will suffer as a result.’”
Yule mwanamume atakuwa hana hatia kwa kumleta mke wake kwa kuhani. Na yule mwanmke atauchukua uovu wake.”