< Numbers 31 >

1 Yahweh spoke to Moses/me and said,
Bwana akamwambia Mose,
2 “Before you die, [tell the] Israeli people that they should (pay back/get revenge on) the Midian people-group for what they did to you.”
“Uwalipize kisasi Wamidiani kwa ajili ya Waisraeli. Halafu baada ya hayo, utakufa.”
3 So Moses/I said to the people, “Get some men prepared for battle. Yahweh will enable them to (pay back/get revenge on) the Midian people-group [for what they did to us].
Kwa hiyo Mose akawaambia watu, “Waandaeni baadhi ya wanaume wenu waende vitani kupigana na Wamidiani ili wawalipize kisasi cha Bwana.
4 Select 1,000 men from each tribe to fight.”
Peleka wanaume 1,000 vitani kutoka kila kabila la Israeli.”
5 So 12,000 men prepared for fighting in the battle, 1,000 from each tribe.
Kwa hiyo waliandaliwa wanaume 12,000 kwa vita, wanaume 1,000 kutoka kila kabila, walitolewa kutoka koo za Israeli.
6 When Moses/I sent them to the battle, Phinehas, the son of Eleazar the priest, went with them. He took with him some of the things from the Sacred Tent and the trumpets that would be blown to give the signal [to start the battle].
Mose aliwatuma vitani, watu 1,000 kutoka kila kabila, pamoja na Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, ambaye alichukua vyombo vya mahali patakatifu na tarumbeta za kuashiria.
7 The Israeli men fought the soldiers from the Midian people-group, as Yahweh had told Moses/me to tell them to do, and they killed every man from the Midian people-group.
Walipigana dhidi ya Wamidiani, kama Bwana alivyomwagiza Mose, nao waliua kila mwanaume.
8 Among those whom they killed were the five kings of the Midian people-group—Evi, Rekem, Zur, Hur, and Reba. They also killed with a sword Balaam, the son of Beor.
Miongoni mwa watu waliouawa walikuwepo wafalme watano wa Midiani, nao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba. Vilevile walimuua Balaamu mwana wa Beori kwa upanga.
9 They captured all the women and children of the Midian people-group and took away their cattle, their flocks of sheep, and herds of goats, and all their other possessions.
Waisraeli waliwateka wanawake wa Kimidiani pamoja na watoto wao na walichukua makundi ya ngʼombe, kondoo na mali zao kama nyara.
10 Then they burned down all the houses in the towns and villages where the people of the Midian people-group lived,
Walichoma moto miji yote ambayo Wamidiani walikuwa wanaishi, pamoja na kambi zao zote.
11 but they took home with them all the women and children and animals and possessions.
Walichukua nyara zote na mateka, pamoja na watu na wanyama,
12 They brought all these to Eliezer and Moses/me, and to the rest of the Israeli people who were at their/our camp on the plains where the Moab people-group lived, near the Jordan River, across from Jericho.
nao waliwaleta wafungwa mateka na nyara kwa Mose na kwa kuhani Eleazari, nao Waisraeli walikusanyika kwenye kambi zao katika tambarare za nchi ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
13 Eleazar and all the leaders of the people and Moses/I went outside the camp to greet/meet with them.
Mose, kuhani Eleazari na viongozi wote wa jumuiya wakatoka kuwalaki nje ya kambi.
14 But Moses/I was angry with some of the men who had returned from the battle. He/I was angry with the army officers and the men who were commanders of 1,000 men and those who were commanders of 100 men.
Mose aliwakasirikia maafisa wa jeshi, yaani hao wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, ambao walirudi kutoka vitani.
15 He/I asked them, “Why did you allow the women to live [RHQ]?
Mose akawauliza, “Je, mmewaacha wanawake wote hai?”
16 They are the ones who did what Balaam suggested and urged/persuaded our people to worship Baal [instead of Yahweh]. As a result, Yahweh caused a plague to strike his people while they were at Peor.
“Wanawake hao ndio waliofuata ushauri wa Balaamu, nao ndio waliowasababisha Waisraeli wamwasi Bwana kwa kile kilichotokea kule Peori, na kwa hiyo pigo liliwapata watu wa Bwana.
17 So, now you must kill all the boys of the Midian people-group, and also kill all the women who have had sex [EUP] with any man.
Sasa waue wavulana wote. Pia muue kila mwanamke ambaye alikwisha fanya tendo la ndoa,
18 Spare only the girls who are virgins [EUP]. You can keep them to be your [wives or your slaves].
lakini mwacheni hai kwa ajili yenu kila msichana ambaye kamwe hajawahi kuzini na mwanaume.
19 All of you who have killed someone or touched the corpse of someone who was killed [in the battle] must stay outside the camp for seven days. On the third day and on the seventh day, you must [perform the ritual to] cause you and those whom you have captured to become acceptable to God again.
“Ninyi nyote ambao mmeua mtu yeyote au kumgusa mtu yeyote ambaye ameuawa, lazima mkae nje ya kambi kwa muda wa siku saba. Katika siku ya tatu na ya saba lazima mjitakase wenyewe pamoja na wafungwa wenu.
20 You must also wash your clothes and anything [that you took to the battle] that is made of leather or goat’s hair or wood.”
Takaseni kila vazi pamoja na kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi, kwa singa za mbuzi au kwa mti.”
21 Then Eleazar said to the soldiers who had returned from the battle, “This is what Yahweh has instructed Moses:
Kisha kuhani Eleazari aliwaambia askari waliokuwa wamekwenda vitani, “Haya ndiyo matakwa ya sheria ambayo Bwana alimpa Mose:
22 You must put into a fire any gold or silver or bronze or iron or tin or lead things [that you brought back from the battle].
Dhahabu, fedha, shaba, chuma, bati, risasi,
23 Put everything that will not burn into the fire, and then they will be acceptable for you to use. But also sprinkle those things with the water that causes things and people to become acceptable to God. The things that would burn [if you put them] in a fire, sprinkle them with that water.
na kitu kingine chochote ambacho kinaweza kuhimili moto lazima mkipitishe kwenye moto, kisha kitakuwa safi. Lakini ni lazima pia kitakaswe kwa maji ya utakaso. Kitu chochote kisichoweza kuhimili moto lazima kipitishwe kwenye yale maji ya utakaso.
24 On the seventh day, wash your clothes, and then you will become acceptable to God again. After you do that, you may return to the camp.”
Katika siku ya saba fueni nguo zenu, nanyi mtakuwa safi. Kisha mtaweza kuingia kambini.”
25 Yahweh also said to Moses/me,
Bwana akamwambia Mose,
26 “Tell Eleazar and the leaders of the family groups that they must write down a list of all the goods, the women, and the animals that were captured [in the battle].
“Wewe na kuhani Eleazari pamoja na viongozi wa jamaa ya jumuiya mtahesabu watu wote na wanyama ambao walitekwa.
27 Then they must divide all those things, half given to the men who fought in the battle and the other half given to the rest of the people.
Gawanyeni hizo nyara kati ya askari ambao walishiriki katika vita na kwa jumuiya.
28 From the men who fought in the battle, take one from every 500 people and from every 500 cattle and donkeys and sheep, to be a tax for me.
Kutoka fungu la wale waliokwenda kupigana vitani, tenga kama ushuru kwa ajili ya Bwana kitu kimoja kati ya kila mia tano, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo au mbuzi.
29 Take these things to Eleazar to (be my share/belong to me).
Chukua ushuru huu kutoka fungu lao, umpe kuhani Eleazari kama sehemu ya Bwana.
30 And from the half that belongs to the ordinary people, take one item from every 50. That includes people, cattle, donkeys, sheep, goats, and other animals. Give those things to the descendants of Levi who take care of my Sacred Tent.”
Kutoka fungu la Waisraeli, chukua kitu kimoja kati ya kila hamsini, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo, mbuzi au wanyama wengine. Hivyo uwape Walawi, ambao wanawajibika kutunza Maskani ya Bwana.”
31 So Eleazar and Moses/I did what Yahweh commanded.
Kwa hiyo Mose na kuhani Eleazari wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Mose.
32 There were 675,000 sheep, 72,000 cattle, 61,000 donkeys, and 32,000 virgins that they had captured from the Midian people-group.
Nyara zilizobaki kutoka mateka ambayo askari walichukua ni kondoo 675,000,
ngʼombe 72,000,
punda 61,000,
na wanawake 32,000 ambao hawakumjua mume kwa kufanya tendo la ndoa.
36 The men who fought in the battle took 337,000 sheep [from the battle],
Nusu ya fungu la wale waliokwenda kupigana vitani lilikuwa: Kondoo 337,500
37 and they gave 675 of them to Yahweh.
ambayo ushuru kwa ajili ya Bwana ilikuwa kondoo 675;
38 They took 36,000 cattle and gave 72 of them to Yahweh.
ngʼombe 36,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa ngʼombe 72;
39 They took 30,500 donkeys, and they gave 61 of them to Yahweh.
punda 30,500 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa punda 61;
40 They took 16,000 virgins, and they dedicated 32 of them to Yahweh.
Watu 16,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa watu 32.
41 Moses/I gave to Eleazar all [the animals] that had been given to Yahweh, as Yahweh had commanded.
Mose alimpa kuhani Eleazari ushuru kama sehemu ya Bwana, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
42 Moses/I separated what those who had fought in the battle received from what the other people received. The people had taken 337,500 sheep, 36,000 cattle, 30,500 donkeys, and 16,000 virgins,
Ile nusu iliyokuwa ya Waisraeli, ambayo Mose aliitenga kutoka kwa ile ya watu waliokwenda vitani,
nusu iliyokuwa ya jumuiya, ilikuwa kondoo 337,500,
ngʼombe 36,000,
punda 30,500,
na wanadamu 16,000.
47 From what the people received, Moses/I took one from every 50 items and dedicated them to Yahweh. That included animals and people. As Yahweh commanded, he/I gave them all to the descendants of Levi who took care of the Sacred Tent.
Kutoka hiyo nusu iliyokuwa ya Waisraeli, Mose alichagua moja kati ya kila hamsini ya wanadamu na wanyama, kama Bwana alivyomwagiza, naye aliwapa Walawi, ambao waliwajibika kutunza Maskani ya Bwana.
48 Then the army officers and those who commanded 1,000 men and those who commanded 100 men came to Moses/me.
Kisha maafisa waliokuwa juu ya vikosi vya jeshi, wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, walimwendea Mose
49 They said, “We, who are your servants, have counted the soldiers whom we command, and [we found that] none of them (is missing/has been killed).
na kumwambia, “Watumishi wako wamehesabu askari walio chini ya amri yetu na hakuna hata mmoja aliyekosekana.
50 So [to thank Yahweh for that], we have brought to him a gift of the gold items that we found [after the battle]: Gold arm bands and bracelets and rings and earrings and necklaces. This will enable us to be forgiven for our sins.”
Kwa hiyo tumeleta kama sadaka kwa Bwana vyombo vya dhahabu kila mmoja wetu alivyopata, yaani vikuku, bangili, pete za muhuri, vipuli na mikufu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yetu mbele za Bwana.”
51 So Eleazar and Moses/I accepted the gold items that they brought.
Mose na kuhani Eleazari wakapokea kutoka kwao dhahabu, yaani vyombo vyote vilivyonakshiwa.
52 The total of it weighed about (420 pounds/190 kg.).
Dhahabu yote kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia ambavyo Mose na kuhani Eleazari walimletea Bwana kama zawadi ilikuwa shekeli 16,750
53 Each soldier had taken these things for himself.
Kila askari alikuwa amejichukulia nyara zake binafsi.
54 Eleazar and Moses/I accepted these gold items from these commanders and put them in the Sacred Tent to remind the Israeli people about how Yahweh [had helped them defeat the Midian people-group].
Mose na kuhani Eleazari walipokea dhahabu kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, wakazileta katika Hema la Kukutania kama ukumbusho kwa Waisraeli mbele za Bwana.

< Numbers 31 >