< Numbers 27 >

1 One day the five daughters of Zelophehad came [to Moses/me]. They were Mahlah, Noah, Hoglah, Milcah, and Tirzah.
Binti za Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, walikuwa wa koo za Manase mwana wa Yosefu. Majina ya hao binti yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa. Walikaribia
2 They came to the entrance of the Sacred Tent and stood in front of Eleazar, Moses/me, the tribal leaders, and many [EUP] other Israeli people.
ingilio la Hema la Kukutania na kusimama mbele ya Mose, kuhani Eleazari, viongozi na kusanyiko lote, wakasema,
3 They said, “Our father died [during the time that we were] in the desert, and he did not have any sons. But he was not among those who supported Korah, who rebelled against Yahweh. He died just because he was a sinner [like everyone else].
“Baba yetu alikufa jangwani. Hakuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora, ambao walifungamana pamoja dhidi ya Bwana, lakini alikufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe na hakuacha wana.
4 (Why should the name of his clan disappear [with the result that we do not receive any land] only because our father had no sons?/It is not right that the name of his clan disappear [with the result that we do not receive any land] only because our father had no sons.) [RHQ] So give us some land like our relatives will be getting!”
Kwa nini jina la baba yetu lifutike kutoka ukoo wake kwa sababu hakuwa na mwana? Tupatie milki miongoni mwa ndugu za baba yetu.”
5 So Moses/I asked Yahweh [what to do about] their request.
Kwa hiyo Mose akalileta shauri lao mbele za Bwana,
6 And Yahweh replied,
naye Bwana akamwambia Mose,
7 “What the daughters of Zelophehad are requesting is right. You must give them some land, just as you are giving to their father’s relatives. Give to each of them some of the land that would have been given to their brothers [if they had any].
“Wanachosema binti za Selofehadi ni sawa. Ni lazima kwa hakika uwape milki kama urithi miongoni mwa ndugu za baba yao, na kubadili urithi wa baba yao uwe wao.
8 “Also tell this to the Israeli people: ‘If a man who has no sons dies, give the things that his sons would have inherited to his daughters.
“Waambie Waisraeli, ‘Ikiwa mtu atakufa naye hakuacha mwana, utampa binti yake urithi wake.
9 If the man has no sons or daughters, give to his brothers the things that his sons and daughters would have inherited.
Ikiwa hana binti, wape ndugu zake wa kiume urithi wake.
10 If the man had no brothers, give to his father’s brothers the things that his sons or daughters or brothers would have inherited.
Ikiwa hana ndugu wa kiume toa urithi wake kwa ndugu za baba yake.
11 If the man’s father has no brothers, give to his closest relative the things that the others would have inherited.’ That will be a rule for the Israeli people, because I am giving this as a command to you, Moses, [to tell them].”
Ikiwa baba yake hakuwa na ndugu wa kiume, toa urithi wake kwa ndugu wa karibu katika ukoo wake, ili aumiliki. Hili litakuwa dai la sheria kwa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru Mose.’”
12 One day, Yahweh said to Moses/me, “Climb to the top of the Abarim Mountains [east of the Jordan River]. Then look out over the land that I am giving to the Israeli people.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Panda juu ya mlima huu katika kilele cha Abarimu uione nchi ambayo nimewapa Waisraeli.
13 After you have seen it, you will die [EUP] just like your [older] brother Aaron did.
Baada ya kuiona, wewe pia utakusanywa pamoja na watu wako kama ndugu yako Aroni alivyokusanywa,
14 The reason [that you will die and not enter that land] is that you both disobeyed my instructions/commands in the Zin Desert. When the Israeli people rebelled against me there at Meribah, near Kadesh, [I told you to speak to the rock to cause] water to flow out of it. [But because you struck the rock instead of speaking to it], you did not show the people my holy power.”
kwa kuwa jumuiya ilipoasi amri yangu kwenye maji katika Jangwa la Sini, wakati jumuiya ilipogombana nami, nyote wawili mliacha kuitii amri yangu ya kuniheshimu kama mtakatifu mbele ya macho yao.” (Haya yalikuwa maji ya Meriba huko Kadeshi, katika Jangwa la Sini.)
15 Then Moses/I said this to Yahweh:
Mose akamwambia Bwana,
16 “Yahweh, you are the God who directs the spirits of all people. So please appoint a new leader for the Israeli people.
“Bwana, Mungu wa roho zote za wanadamu, na amteue mtu juu ya jumuiya hii
17 Appoint someone who will lead your people when they go to fight a battle, so that they will not [just wander around] like sheep that do not have a shepherd.” [SIM]
ili atoke na kuingia mbele yao, atakayewaongoza katika kutoka kwao na kuingia kwao, ili watu wa Bwana wasiwe kama kondoo wasio na mchungaji.”
18 Yahweh replied, “Get Joshua, the son of Nun, who has my Spirit within him. Lay your hands on him [to appoint him].
Kwa hiyo Bwana akamwambia Mose, “Mchukue Yoshua mwana wa Nuni, mtu ambaye Roho yuko ndani yake, uweke mkono juu yake.
19 Cause him to stand in front of Eleazar the priest, as all the people are watching, and commission/appoint him to be the new leader of the Israeli people.
Msimamishe mbele ya kuhani Eleazari pamoja na kusanyiko lote, umpe maagizo mbele yao.
20 Give to him some of the authority that you now have, in order that all the Israeli people will [know that they must] obey him.
Mpe sehemu ya mamlaka yako ili jumuiya yote ya Waisraeli ipate kumtii.
21 When you all need me to guide you, Joshua will stand in front of Eleazar. Then by (casting lots/throwing marked stones on the ground) Eleazar will find out what they should do.”
Atasimama mbele ya kuhani Eleazari, ambaye atapokea maamuzi kwa ajili yake, kwa kuuliza mbele za Bwana kwa ile Urimu. Kwa amri yake, yeye na jumuiya yote ya Waisraeli watatoka, na kwa amri yake, wataingia.”
22 So Moses/I did what Yahweh commanded. He/I presented Joshua to Eleazar and to all the Israeli people.
Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza. Akamtwaa Yoshua na kumsimamisha mbele ya kuhani Eleazari na kusanyiko lote.
23 Moses/I laid his/my hands on him and commissioned/appointed him to do the work that Yahweh told Moses/me to tell him to do.
Kisha akaweka mikono yake juu ya kichwa cha Yoshua na kumpa maagizo, kama vile Bwana alivyoelekeza kupitia kwa Mose.

< Numbers 27 >