< Numbers 22 >
1 Then the Israelis traveled west to the area of Moab that was in the valley of the Jordan [River], across the river from Jericho [city].
Kisha Waisraeli wakasafiri katika tambarare za Moabu na kupiga kambi kando ya Mto Yordani, ngʼambo ya Yeriko.
2 But King Balak, the son of Zippor, who ruled Moab, found out what the Israelis had done to the Amor people-group.
Basi Balaki mwana wa Sipori, aliona mambo yale yote ambayo Israeli aliwatendea Waamori,
3 [When he saw that] the Israelis were very numerous, he and his people became terrified.
Moabu aliogopa, kwa kuwa walikuwepo watu wengi sana. Hakika, Moabu alijawa na hofu kubwa kwa sababu ya Waisraeli.
4 So the king of Moab [went to] the leaders of the Midian people-group and said to them, “This huge group [of Israelis] will (wipe out/destroy) everything around them, like an ox devours grass!” Balak was the king of Moab.
Wamoabu wakawaambia wazee wa Midiani, “Umati huu wa watu unakwenda kuramba kila kitu kinachotuzunguka, kama maksai arambavyo majani ya shambani.” Kwa hiyo Balaki mwana wa Sipori, ambaye alikuwa mfalme wa Moabu wakati huo,
5 He sent messengers to [a prophet named] Balaam, who was living in his own area, in Pethor [town], near the [Euphrates] River. He sent this message to request that Balaam would come [to help him]: “A huge group of people has arrived here from Egypt. [It looks like] they are covering the entire land! And they have begun to live close to us.
akatuma wajumbe kwenda kumwita Balaamu mwana wa Beori, ambaye alikuwa huko Pethori, karibu na Mto Frati, katika nchi yake ya kuzaliwa. Balaki akasema: “Taifa limekuja kutoka Misri, nao wamefunika uso wa nchi, nao wametua karibu nami.
6 Because they are very powerful/numerous, [we are afraid of them. So] please come and curse them for me. Then my army may be able to defeat them and expel them from the land [where they are now living]. I know that good things will happen to the people whom you bless, and disasters will happen to the people whom you curse.”
Sasa uje kuwalaani watu hawa, kwa kuwa wana nguvu sana kuniliko. Kisha huenda nikaweza kuwashinda na kuwatoa nje ya nchi. Kwa kuwa ninajua kwamba, wale unaowabariki wanabarikiwa na wale unaowalaani wanalaaniwa.”
7 [Balak’s messengers, who were] leaders of both the Moab and Midian people-groups, took money with them to pay Balaam in order that he would [come and] curse the Israelis. They went to Balaam and told him what Balak had said.
Wazee wa Moabu na wa Midiani wakaondoka, wakiwa wamechukua ada ya uaguzi. Walipokwenda kwa Balaamu, wakamweleza kile Balaki alikuwa amesema.
8 Balaam said, “Stay here tonight. [Tomorrow morning] I will tell you whatever Yahweh tells me that I should say to you.” So the leaders from Moab stayed there that night.
Balaamu akawaambia, “Mlale hapa usiku huu, nami nitawaletea jibu lile Bwana atakalonipa.” Kwa hiyo wakuu wa Moabu wakakaa naye.
9 During the night, God appeared to Balaam and asked him, “(Who are/Tell me about) these men who are staying with you.”
Mungu akamjia Balaamu na kumuuliza, “Watu gani hawa walio pamoja nawe?”
10 Balaam replied, “Balak, the king of Moab, sent these men to tell me this:
Balaamu akamwambia Mungu, “Balaki mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu, alinipelekea ujumbe huu:
11 ‘A huge group of people has come from Egypt, and they have spread all over this area. Please come immediately to curse them. Then I may be able to defeat them and expel them [from this area].’”
‘Taifa ambalo limekuja kutoka Misri limefunika uso wa nchi. Sasa uje unilaanie hao watu. Kisha huenda nitaweza kupigana nao na kuwafukuza.’”
12 God replied to Balaam, “Do not go with them! I have blessed those people, so you must not curse them!”
Lakini Bwana akamwambia Balaamu, “Usiende pamoja nao. Hupaswi kulaani watu hao, kwa kuwa wamebarikiwa.”
13 The next morning, Balaam got up and told Balak’s men, “Go back home. [But go by yourselves, because] Yahweh is not allowing me to go with you.”
Asubuhi iliyofuata Balaamu akaamka, akawaambia wakuu wa Balaki, “Rudini katika nchi yenu, kwa kuwa Bwana amenikataza nisiende pamoja nanyi.”
14 So the men from Moab returned to King Balak and they reported to him, “Balaam refused to come with us.”
Kwa hiyo wakuu wa Moabu wakarudi kwa Balaki na kumwambia, “Balaamu amekataa kuja pamoja nasi.”
15 But Balak sent another [group of] leaders to Balaam. It was a group that was larger and they were more important [than the men in the first group].
Kisha Balaki akatuma wakuu wengine, wengi zaidi na wanaoheshimiwa zaidi kuliko wale wa kwanza.
16 They went to Balaam and told him this: “This is what King Balak says: ‘Please do not allow anything to hinder you from coming here.
Wakafika kwa Balaamu na kumwambia: “Balaki mwana wa Sipori amesema hivi: Usiruhusu kitu chochote kikuzuie kuja kwangu,
17 I will pay you (a lot of money/very well) [if you come], and I will do anything that you ask me to do. Just come and curse these [Israeli] people for me!’”
kwa sababu nitakulipa vizuri sana na kufanya lolote usemalo. Njoo unilaanie watu hawa.”
18 But Balaam answered them, “Even if Balak would give me a palace filled with silver and gold, I would not do anything to disobey Yahweh, (my God/the God whom I [worship]).
Lakini Balaamu akawajibu, “Hata kama Balaki angenipa jumba lake la kifalme likiwa limejazwa fedha na dhahabu, singeweza kufanya kitu chochote kikubwa au kidogo ili kutenda kitu nje ya agizo la Bwana Mungu wangu.
19 But stay here one more night, like the other messengers did, and I will find out if Yahweh has anything more to say to me.”
Mlale hapa usiku huu kama wale wengine walivyofanya, nami nitatafuta ni nini kingine Bwana atakachoniambia.”
20 That night God appeared to Balaam again and said to him, “These men have come to request that you go back with them, so you may go with them, but do only what I tell you [to do]!”
Usiku ule Bwana akamjia Balaamu na kumwambia, “Kwa kuwa watu hawa wamekuja kukuita wewe, nenda nao, lakini ufanye tu lile nitakalokuambia.”
21 So the next morning, Balaam put a saddle on his donkey and he departed [with two of his servants] along with the men from Moab.
Balaamu akaamka asubuhi, akatandika punda wake akaenda pamoja na wakuu wa Moabu.
22 [Even though God had given Balaam permission to go, he was still angry]. So he sent one of his angels to Balaam. This angel stood in the road to block Balaam’s path. As Balaam and the two servants were riding on their donkeys,
Lakini Mungu alikasirika sana alipokwenda, naye malaika wa Bwana akasimama barabarani kumpinga. Balaamu alikuwa amepanda punda wake, na watumishi wake wawili walikuwa pamoja naye.
23 Balaam’s donkey saw the angel. The angel was standing in the road and was holding a sword in his hand, [but Balaam did not see him]. Balaam’s donkey turned off the road into a field. So Balaam struck the donkey and forced it to go back onto the road.
Wakati punda alipomwona malaika wa Bwana akiwa amesimama barabarani akiwa na upanga uliofutwa mkononi mwake, punda akageukia upande kuelekea shambani. Balaamu akampiga ili amrudishe barabarani.
24 Then the angel stood in a place where the road was very narrow, between two vineyards, with walls on each side of the road.
Ndipo malaika wa Bwana akasimama katika njia nyembamba iliyo kati ya mashamba mawili ya mizabibu, yakiwa na kuta pande zote mbili.
25 When the donkey saw the angel standing there, it walked very close to the wall [to try to get past the angel]. As a result, it bashed Balaam’s foot against the wall. So Balaam struck the donkey again.
Punda alipomwona malaika wa Bwana, alijisukumiza karibu na ukuta, na kugandamiza mguu wa Balaamu ukutani. Ndipo Balaamu akampiga tena punda.
26 Then the angel went further along the road and stood at a place that was extremely narrow, with the result that the donkey could not get past at all.
Kisha malaika wa Bwana akaendelea mbele na kusimama mahali pembamba ambapo hapakuwepo nafasi ya kugeuka, upande wa kulia wala wa kushoto.
27 This time, when the donkey saw the angel, it lay down [on the ground] with Balaam sitting on top of it. Balaam became extremely angry, and he struck the donkey again with his walking stick.
Punda alipomwona malaika wa Bwana, alilala chini Balaamu angali amempanda, naye Balaamu akakasirika na kumpiga kwa fimbo yake.
28 Then Yahweh enabled the donkey to speak! It said to Balaam, “What bad thing have I done to you that caused you to strike me three times?”
Kisha Bwana akakifungua kinywa cha punda, akamwambia Balaamu, “Nimekutendea nini kinachokufanya unipige mara hizi tatu?”
29 Balaam shouted, “I struck you because you have caused me to appear to be foolish! If I had a sword with me, I would kill you!”
Balaamu akamjibu punda, “Umenifanya mjinga! Kama ningelikuwa na upanga mkononi mwangu, ningelikuua sasa hivi.”
30 But the donkey answered, “I am your own donkey [RHQ], the one that you have always ridden! Have I ever done anything like this previously?” Balaam said, “No.”
Punda akamwambia Balaamu, “Je, mimi si punda wako mwenyewe, ambaye umenipanda siku zote, hadi leo? Je, nimekuwa na tabia ya kufanya hivi kwako?” Akajibu, “Hapana.”
31 Then Yahweh enabled Balaam to see the angel standing on the road, holding a sword in his hand. Balaam [realized that it was an angel and] prostrated himself on the ground in front of the angel.
Kisha Bwana akafungua macho ya Balaamu, naye akamwona malaika wa Bwana amesimama barabarani akiwa ameufuta upanga wake. Balaamu akainama, akaanguka kifudifudi.
32 The angel asked him, ‘(Why did you strike your donkey three times?/ You should certainly not have struck the donkey three times! [RHQ] I have come to block your path because what you are planning to do is wrong.
Malaika wa Bwana akamuuliza Balaamu, “Kwa nini umempiga punda wako mara tatu hizi? Nimekuja kukuzuia kwa sababu njia yako imepotoka mbele yangu.
33 Three times your donkey saw me and turned away from me. If it had not done that, I would certainly have killed you already, but I would have allowed the donkey to live.”
Punda aliniona na kunikwepa mara hizi tatu. Kama punda hangenikwepa, hakika ningekuwa nimeshakuua sasa, lakini ningemwacha punda hai.”
34 Then Balaam said to the angel, “I have sinned. But I did not realize that you were standing there, trying to block my path. So if you do not want me to continue going, I will return home.”
Balaamu akamwambia malaika wa Bwana, “Nimetenda dhambi. Sikutambua kuwa umesimama barabarani kunizuia. Basi kama haikupendezi, nitarudi.”
35 But the angel replied, “I will allow you to go with these men, but you must say only what I tell you to say!” So Balaam went on with the leaders whom Balak [had sent].
Malaika wa Bwana akamwambia Balaamu, “Uende na watu hao, lakini useme tu lile nikuambialo.” Kwa hiyo Balaamu akaenda na wale wakuu wa Balaki.
36 When King Balak heard that Balaam was coming, he went to meet him at a Moab town alongside the Arnon [River] that was at the border of his own land.
Balaki aliposikia kuwa Balaamu anakuja, akatoka kumlaki katika mji wa Moabu, katika mpaka wa Arnoni, ukingoni mwa nchi yake.
37 [When he arrived where] Balaam was, he said to him, “I sent you [RHQ] a message saying that you should come immediately [RHQ]! Why did you not come immediately? [Did you think that] I was not able to pay you a lot of money for coming?”
Balaki akamwambia Balaamu, “Je, sikukupelekea jumbe za haraka? Kwa nini hukuja kwangu? Hivi kweli mimi siwezi kukulipa?”
38 Balaam replied, “I have come here now, but I am not able to say anything [that I want to]. I will say only the words that God tells me to say [MTY].”
Balaamu akajibu, “Vema, sasa nimekuja kwako. Lakini kwani nina uwezo wa kusema tu chochote? Ni lazima niseme tu kile ambacho Mungu ataweka kinywani mwangu.”
39 Then Balaam went with Balak to Kiriath-Huzoth [town].
Kisha Balaamu alikwenda na Balaki mpaka Kiriath-Husothi.
40 There Balak killed some cattle and sheep as sacrifices, and offered [parts of the meat] to Balaam and the leaders who were with him.
Balaki akatoa dhabihu ya ngʼombe na kondoo; baadhi yake akampa Balaamu na wakuu waliokuwa pamoja naye.
41 [They slept there], and the next morning Balak took Balaam part way up [the mountain] to Bamoth-Baal [village]. From there, they could see some of the Israeli people who were down below.
Asubuhi iliyofuata Balaki akamchukua Balaamu mpaka Bamoth-Baali, na kutoka huko Balaamu akawaona baadhi ya watu.