< Nehemiah 7 >

1 After the wall had been finished and we had put the gates in their places, we assigned to the temple guards and to the members of the [sacred] choir and the other descendants of Levi the work that they were to do.
Baada ya ukuta kukamilika kujengwa upya na nikaweka milango, mabawabu wa lango, waimbaji, na Walawi waliteuliwa.
2 I appointed two men to [help me to] govern Jerusalem, my brother Hanani and Hananiah who was the commander of the fortress [in Jerusalem]. Hananiah always did his work reliably, and he revered God more than most other people do.
Nikamweka Hanani ndugu yangu kuwa kiongozi wa Yerusalemu, pamoja na Hanania jemadari wa ngome, kwa kuwa alikuwa mtu mwadilifu na mwenye kumcha Mungu kuliko watu wengine.
3 I said to them, “Do not open the gates of Jerusalem until late each morning. And close the gates and put the bars across the doors [(late in each afternoon/before sunset)] while the gatekeepers are still guarding the gates.” I also told them to appoint some people who lived in Jerusalem to be guards [on the wall], and to assign some of them to be guards at certain other places and to assign others to guard the area close to their own houses.
Nikawaambia, “Malango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka jua litakapokuwa limepanda. Walinzi wa malango wakiwa bado kwenye zamu, waamuru wafunge milango na waweke makomeo. Pia wateueni wenyeji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja kwenye lindo lake, na wengine karibu na nyumba zao wenyewe.”
4 The city [of Jerusalem] covered a large area, but [at that time] not many people lived in the city, and they had not built many new houses yet [HYP].
Mji ulikuwa mkubwa, tena wenye nafasi nyingi, lakini walikuwepo watu wachache ndani yake, nazo nyumba zilikuwa bado ni magofu.
5 [To defend the city, we needed more people there.] Then God gave me the idea to summon the leaders and officials and [other] people, and to look in the books [in which were written the names] of all the people and their clans. So I found the records of the people who had first returned from Babylonia. This is what I found written in those records:
Hivyo Mungu wangu akaweka moyoni mwangu kuwakusanya wakuu, maafisa na watu wa kawaida kwa ajili ya kuorodheshwa kulingana na jamaa zao. Nilikuta orodha ya vizazi ya wale waliokuwa wa kwanza kurudi toka utumwani. Haya ndiyo niliyokuta yameandikwa humo:
6 (This is a list/Here are the names) of the people who returned to Jerusalem and to other places in Judea. They had been living in Babylonia since King Nebuchadnezzar’s army had captured their relatives/ancestors and took them to Babylonia. But they had returned to Judea and were living in the towns [where their ancestors had lived].
Hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
7 Their leaders were Zerubbabel, Joshua, Azariah, Raamiah, Nahamani, Mordecai, Bilshan, Mispereth, Bigvai, Nehum, Baanah, and me. This is a list of the number of men in each clan who returned:
wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigwai, Nehumu na Baana): Orodha ya wanaume wa Israeli ilikuwa:
8 2,172 men from the clan of Parosh;
wazao wa Paroshi 2,172
9 372 men from the clan of Shephatiah;
wazao wa Shefatia 372
10 652 men from the clan of Arah;
wazao wa Ara 652
11 2,818 men from the clan of Pahath-Moab, who are descendants of Jeshua and Joab;
wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,818
12 1,254 men from the clan of Elam;
wazao wa Elamu 1,254
13 845 men from the clan of Zattu;
wazao wa Zatu 845
14 760 men from the clan of Zaccai;
wazao wa Zakai 760
15 648 men from the clan of Bani (OR, Binnui);
wazao wa Binui 648
16 628 men from the clan of Bebai;
wazao wa Bebai 628
17 2,322 men from the clan of Azgad;
wazao wa Azgadi 2,322
18 667 men from the clan of Adonikam;
wazao wa Adonikamu 667
19 2,067 men from the clan of Bigvai;
wazao wa Bigwai 2,067
20 655 men from the clan of Adin;
wazao wa Adini 655
21 98 men from the clan of Ater, whose other name is Hezekiah;
wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
22 328 men from the clan of Hashum;
wazao wa Hashumu 328
23 324 men from the clan of Bezai;
wazao wa Besai 324
24 112 men from the clan of Hariph, [whose other name is Jorah];
wazao wa Harifu 112
25 95 men from the clan of Gibeon, [whose other name is Gibbar].
wazao wa Gibeoni 95
26 Men whose ancestors had lived in these towns also returned: 188 men from Bethlehem and Netophah
watu wa Bethlehemu na Netofa 188
27 128 men from Anathoth;
watu wa Anathothi 128
28 42 men from Beth-Azmaveth
watu wa Beth-Azmawethi 42
29 743 men from Kiriath-Jearim, Kephirah and Beeroth;
watu wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
30 621 men from Ramah and Geba;
watu wa Rama na Geba 621
31 122 men from Micmash;
watu wa Mikmashi 122
32 123 men from Bethel and Ai;
watu wa Betheli na Ai 123
33 52 men from Nebo;
watu wa Nebo 52
34 1,254 from Elam;
wazao wa Elamu 1,254
35 320 from Harim;
wazao wa Harimu 320
36 345 from Jericho;
wazao wa Yeriko 345
37 721 from Lod, Hadid, and Ono;
wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 721
38 3,930 from Senaah. The following priests also returned:
wazao wa Senaa 3,930
39 973 from the clan of Jedaiah who are descendants of Jeshua;
Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
40 1,052 from the clan of Immer;
wazao wa Imeri 1,052
41 1,247 from the clan of Pashhur;
wazao wa Pashuri 1,247
42 1,017 from the clan of Harim.
wazao wa Harimu 1,017
43 [Other] descendants of Levi who returned were: 74 from the clan of Jeshua and Kadmiel, who are descendants of Hodevah [who is also known as Hodaviah];
Walawi: wazao wa Yeshua (kupitia Kadmieli kupitia jamaa ya Hodavia) 74
44 148 singers who are descendants of Asaph.
Waimbaji: wazao wa Asafu 148
45 Also 138 temple gatekeepers from the clans of Shallum, Ater, Talmon, Akkub, Hatita, and Shobai returned.
Mabawabu wa malango: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 138
46 Temple workers who returned were descendants of these men: Ziha, Hasupha, Tabbaoth,
Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
47 Keros, Sia [who is also known as Siaha], Padon,
wazao wa Kerosi, Sia, Padoni,
48 Lebanah, Hagabah, Shalmai,
wazao wa Lebana, Hagaba, Shalmai,
49 Hanan, Giddel, Gahar,
wazao wa Hanani, Gideli, Gahari,
50 Reaiah, Rezin, Nekoda,
wazao wa Reaya, Resini, Nekoda,
51 Gazzam, Uzza, Paseah,
wazao wa Gazamu, Uza, Pasea,
52 Besai, Meunim, Ephusesim [who is also called Nephusim],
wazao wa Besai, Meunimu, Nefusimu,
53 Bakbuk, Hakupha, Harhur,
wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
54 Bazlith [who is also called Bazluth], Mehida, Harsha,
wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
55 Barkos, Sisera, Temah,
wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
56 Neziah, and Hatipha.
wazao wa Nesia na Hatifa.
57 Descendants of the servants of King Solomon who returned were: Sotai, Sophereth [who is also called Hassophereth], Perida [who is also known as Peruda],
Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Soferethi, Perida,
58 Jaalah, Darkon, Giddel,
wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
59 Shephatiah, Hattil, Pokereth-hazzebaim, and Amon.
wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Amoni.
60 Altogether, there were 392 temple workers and descendants of Solomon’s servants who returned.
Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
61 Another group of 642 people from the clans of Delaiah, Tobiah, and Nekoda also returned. They came from the towns of Tel-Melah, Tel-Harsha, Kerub, Addan ([which is also known as Addon]), and Immer [in Babylonia]. But they could not prove that they were descendants of Israelis.
Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 642
63 Priests from the clans of Hobaiah, Hakkoz, and Barzillai also returned. Barzillai had married a woman who is a descendant of [a man named] Barzillai from [the] Gilead [region], and he had taken his wife’s family name.
Na kutoka miongoni mwa makuhani: wazao wa Hobaya, Hakosi na Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
64 They searched in the records that contained the names of people’s ancestors, but they could not find the names of those clans, so they were not allowed to have the rights and duties that priests have right away.
Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani, kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
65 The governor told them that before they could eat the food offered as sacrifices, a priest should use the marked stones [to find out what God said about their being priests].
Kwa hiyo, mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
66 Altogether, there were 42,360 people who returned to Judea.
Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
67 There were also 7,337 of their servants, and 245 singers, which included men and women.
tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 245.
68 The Israelis also brought back [from Babylonia] 736 horses, 245 mules,
Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245
69 435 camels, and 6,720 donkeys.
ngamia 435 na punda 6,720.
70 Some of the leaders of the clans gave gifts for the work [of rebuilding the temple]. I, being the governor, gave (17 pounds/8.6 kg.) of gold, 50 bowls [to be used in the temple], and 530 robes for the priests.
Baadhi ya viongozi wa jamaa walichangia kazi ya ujenzi. Mtawala alikabidhi kwenye hazina darkoni 1,000 za dhahabu, mabakuli 50, na mavazi 530 kwa ajili ya makuhani.
71 Some of the leaders of the clans gave a total of (337 pounds/153 kg.) of gold, and (3,215 pounds/1,460 kg.) of silver.
Baadhi ya viongozi wa jamaa walikabidhi kwenye hazina darkoni 20,000 za dhahabu, na mane 2,200 za fedha kwa ajili ya kazi hiyo.
72 The rest of the people gave a total of (337 pounds/153 kg.) of gold, (2,923 pounds/1,330 kg.) of silver, and 67 robes for the priests.
Jumla ya matoleo ya watu wengine yalikuwa ni darkoni 20,000 za dhahabu, mane 2,000 za fedha, na mavazi sitini na saba ya makuhani.
73 So the priests, the [other] descendants of Levi [who helped the priests], the temple guards, the musicians, the temple workers, and many ordinary people, who were all Israelis, started to live in the towns and cities of Judea [where their ancestors had lived].
Makuhani, Walawi, mabawabu, waimbaji na watumishi wa Hekalu, pamoja na baadhi ya watu wengine na Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao wenyewe. Ilipotimia miezi saba, nao Waisraeli wakiwa tayari wanaishi katika miji yao,

< Nehemiah 7 >