< Nehemiah 13 >

1 On that day, when someone read to the people parts of the laws [that God gave] to Moses, they read where it was written that no one from the Ammon people-group or the Moab people-group was ever to be allowed to be with God’s people while they were gathered together [to worship].
Siku hiyo, Kitabu cha Mose kilisomwa kwa sauti kuu, na watu wote wakasikia. Humo ilionekana imeandikwa kwamba hakuna Mwamoni wala Mmoabu atakayeruhusiwa katika kusanyiko la watu wa Mungu,
2 The reason for that was that the people of Ammon and the people of Moab did not give/sell any food or water to the Israelis [while the Israelis were going through their areas after they left Egypt]. Instead, the people of Ammon and Moab paid money to Balaam in order that he would curse the Israelis. But God commanded Balaam to bless the people, not to curse them.
kwa sababu hawakuwalaki Waisraeli kwa chakula na maji. Badala yake walimwajiri Balaamu kuwalaani (lakini hata hivyo Mungu wetu aligeuza laana kuwa baraka).
3 So when the people heard these laws [being read to them], they sent away all the people whose ancestors had come from other countries.
Watu waliposikia sheria hii, waliwatenga watu wote wasio Waisraeli waliokuwa wa uzao wa kigeni.
4 Previously, Eliashib the priest had been appointed to be in charge of the storerooms in the temple. He was a relative of [our enemy] Tobiah.
Kabla ya hili, kuhani Eliashibu alikuwa amewekwa kuwa msimamizi wa vyumba vya ghala ya nyumba ya Mungu wetu. Alikuwa na uhusiano wa karibu na Tobia,
5 He allowed Tobiah to use a large room in which they had previously stored the grain offerings and the incense, the equipment that is used in the temple, the offerings [that the people had brought] for the priests, and the tithes of grain and wine and [olive] oil that [God] had commanded the people to bring to the [other] descendants of Levi, and to the temple musicians, and to the temple guards.
naye alikuwa amempa Tobia chumba kikubwa ambacho mwanzo kilikuwa kikitumika kuweka sadaka za nafaka, uvumba na vyombo vya Hekalu, pamoja na zaka za nafaka, divai mpya na mafuta waliyoagizwa Waisraeli kwa ajili ya Walawi, waimbaji na mabawabu wa lango, pamoja na matoleo kwa makuhani.
6 While [Tobias was using that room], I was not in Jerusalem, because in the 32nd year that Artaxerxes was the king of Babylonia, I went back there to report to him. After a while I requested the king to allow me to return to Jerusalem, [and he allowed me to go].
Lakini wakati haya yote yalipokuwa yakitendeka, sikuwa Yerusalemu, kwa kuwa katika mwaka wa thelathini na mbili wa utawala wa Artashasta mfalme wa Babeli nilikuwa nimerudi kwa mfalme. Baadaye nilimwomba ruhusa,
7 When I arrived in Jerusalem, I found out that Eliashib had done an evil thing by allowing Tobiah to use a room in God’s temple.
nikarudi Yerusalemu. Hapo niligundua jambo la uovu alilofanya Eliashibu kwa kumpa Tobia chumba katika nyua za nyumba ya Mungu.
8 I became very angry, and I threw out of that room everything that belonged to Tobiah.
Nilikasirika sana na nikavitupa nje vyombo vyote vya Tobia.
9 Then I commanded [that they perform a ritual] to make the rooms (pure/acceptable to God) again. And I also ordered that all the equipment used in the temple and all the grain offerings and incense should be put in that room again.
Nilitoa amri kutakasa vyumba, kisha nikavirudisha vifaa vya nyumba ya Mungu, pamoja na sadaka za nafaka na uvumba.
10 I also found out that the temple musicians and [other] descendants of Levi had left Jerusalem and returned to their fields/farms, because the Israeli people had not been bringing to them the food [that they needed].
Pia niligundua kuwa mafungu yaliyopangwa kupewa Walawi hawakuwa wamepewa, nao Walawi wote na waimbaji waliowajibika kwa huduma walikuwa wamerudi katika mashamba yao.
11 So I rebuked the officials, saying to them, “(Why have you not taken care of the work in the temple?/It is disgraceful that you have not taken care of the work in the temple.)” [RHQ] So I brought the descendants of Levi and the musicians back to the temple, and told them to do their work there again.
Basi niliwakemea maafisa na kuwauliza, “Kwa nini nyumba ya Mungu imepuuzwa?” Kisha niliwaita pamoja na kuwaweka kwenye nafasi zao.
12 Then all the people of Judah again started to bring to the temple storerooms their tithes of grain, wine, and [olive] oil.
Yuda wote walileta zaka za nafaka, divai mpya na mafuta kwenye ghala.
13 I appointed these men to be in charge of the storerooms: Shelemiah, who was a priest; Zadok, who knew the Jewish laws very well; and Pedaiah, a descendant of Levi. I appointed Hanan, who is the son of Zaccur and grandson of Mattaniah, to assist them. I knew that I could trust these men while they distributed those offerings to their fellow workers.
Nikamweka kuhani Shelemia, mwandishi Sadoki, na Mlawi aliyeitwa Pedaya kuwa wasimamizi wa ghala, na kumfanya Hanani mwana wa Zakuri, mwana wa Matania kuwa msaidizi wao, kwa sababu watu hawa walionekana kuwa waaminifu. Walipewa wajibu wa kugawa mahitaji kwa ndugu zao.
14 My God, do not forget all these good things that I have faithfully done for your temple and for the work that is done there!
Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa hili, wala usifute kile nilichokifanya kwa uaminifu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu na kwa ajili ya huduma yake.
15 During that time, I saw some people in Judea [who were working] on the Sabbath day. [Some were] pressing grapes [to make wine]. Others were putting grain, [bags of] wine, [baskets of] grapes, figs, and many [HYP] other things, on their donkeys and taking them into Jerusalem. I warned them that they should not sell things to the people of Judea on Sabbath days.
Siku hizo nikaona watu katika Yuda wakikanyaga mashinikizo ya divai siku ya Sabato na kuleta nafaka wakiwapakiza punda, pamoja na divai, zabibu, tini na aina nyingine za mizigo. Nao walikuwa wakileta haya yote Yerusalemu siku ya Sabato. Kwa hiyo niliwaonya dhidi ya kuuza vyakula siku hiyo.
16 I also saw some people from Tyre [city] who were living there in Jerusalem who were bringing fish and other things [into Jerusalem] to sell to the people of Judea on the Sabbath day.
Watu kutoka Tiro waliokuwa wakiishi Yerusalemu walileta samaki na aina nyingi za bidhaa na kuziuza Yerusalemu siku ya Sabato kwa watu wa Yuda.
17 So I rebuked the Jewish leaders and told them, “This is [RHQ] a very evil thing that you are doing! You are causing the Sabbath days to be unholy.
Niliwakemea wakuu wa Yuda na kuwaambia, “Ni uovu gani huu mnaofanya wa kuinajisi siku ya Sabato?
18 Your ancestors did [RHQ] things like that, so God punished them, and as a result, this city was destroyed! And now by causing the Sabbath day to be unholy, you are going to cause God to be angry with us Israeli people [and punish us] more!”
Je, baba zenu hawakufanya mambo kama haya, hata wakamsababisha Mungu wetu kuleta maafa haya yote juu yetu na juu ya mji huu? Sasa bado mnazidi kuchochea ghadhabu yake dhidi ya Israeli kwa kuinajisi Sabato.”
19 So I ordered that at (the beginning of every Sabbath day/every Friday evening) they should shut the gates of the city before it became dark. I also ordered that they should not open the gates until (the Sabbath day was ended [the next day]/Saturday evening). Then [each Sabbath day] I put some of my men at the gates, so they would make sure that nothing to sell was brought into the city on that day.
Wakati vivuli vya jioni vilipoangukia juu ya malango ya Yerusalemu kabla ya Sabato, niliamuru milango ifungwe, wala isifunguliwe mpaka Sabato iishe. Nikawaweka baadhi ya watu wangu mwenyewe kwenye malango ili pasiwepo mzigo utakaoingizwa ndani siku ya Sabato.
20 One or two times merchants [DOU] stayed outside of the city on (Friday night/[the night before the Sabbath day]).
Mara moja au mbili wachuuzi na wauzaji wa bidhaa za aina zote walilala usiku nje ya mji wa Yerusalemu.
21 I warned them, “It is useless [RHQ] for you to stay here outside the walls [on Friday night]! If you do this again, I will tell my men to arrest you!” So after that, they did not come on Sabbath days.
Lakini niliwaonya na kuwaambia, “Kwa nini mnalala karibu na ukuta? Kama mkifanya hivi tena, nitawaadhibu.” Kuanzia wakati ule hawakuja tena siku ya Sabato.
22 I also commanded the descendants of Levi to [perform the ritual to] purify themselves and to guard the city gates, to make sure that the Sabbath was kept holy [by not allowing merchants to enter it on Sabbath days]. My God, do not forget this also that I [have done for you]! And because of your faithfully loving me, allow me to continue to live [many more years]!
Kisha nikawaamuru Walawi kujitakasa na kwenda kulinda malango ili kutunza Sabato iwe takatifu. Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa ajili ya hili pia, nawe unionyeshe wema wako sawasawa na upendo wako mkuu.
23 During that time, I also found out that many of the Jewish men had married women from Ashdod [city], and from [the] Ammon and Moab [people-groups].
Zaidi ya hayo, niliona Wayahudi waliokuwa wameoa wanawake kutoka Ashdodi, Amoni na Moabu.
24 The result was that half of their children spoke the language that people in Ashdod speak or some other language, and they didn’t know how to speak our language.
Nusu ya watoto wao walizungumza lugha ya Kiashidodi au lugha ya watu wengine, bali hawakuweza kuzungumza Kiyahudi.
25 So I rebuked those men, and I [asked God to] curse them, and I beat them and pulled out [some of] their hair. Then I forced them to solemnly promise, knowing that God [MTY] was [listening], that they would never again marry foreigners, and never allow their children to marry foreigners.
Niliwakemea na kuwalaani. Niliwapiga baadhi ya watu na kungʼoa nywele zao. Niliwaapisha kwa jina la Mungu na kusema: “Msiwaoze binti zenu kwa wana wao, wala binti zao wasiolewe na wana wenu wala ninyi wenyewe.
26 [I said to them], “Solomon, the king of Israel, sinned [RHQ] as a result of [marrying] foreign women. He was greater than any of the kings of other nations. God loved him, and caused him to become the king of all the Israeli people, but his foreign wives caused even him to sin.
Je, Solomoni hakutenda dhambi kwa sababu ya wanawake wa namna hiyo? Miongoni mwa mataifa mengi hapakuwepo mfalme kama yeye. Alipendwa na Mungu wake. Naye Mungu alimweka kuwa mfalme juu ya Israeli yote, lakini hata yeye, wanawake wa mataifa mengine walimfanya atende dhambi.
27 [Do you think that] we should do what you have done, and disobey our God by marrying foreign women [who worship idols]? [RHQ]”
Je, tulazimike sasa kusikia kwamba ninyi pia mmefanya uovu huu mkubwa na kutokuwa waaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni?”
28 One of the sons of Jehoiada, the son of Eliashib the Supreme Priest, had married the daughter of [our enemy] Sanballat, from Beth-Horon [town]. So I forced Jehoiada’s son to leave Jerusalem.
Mmoja wa wana wa Yoyada mwana wa Eliashibu kuhani mkuu alikuwa mkwewe Sanbalati Mhoroni. Nami nilimfukuza mbele yangu.
29 My God, do not forget that those people [who have married foreign women] have caused it to be a shame/disgrace to be a priest, and have caused people to despise the agreement that you made with the priests and with the [other] descendants of Levi [who help the priests])!
Ee Mungu wangu, uwakumbuke, kwa sababu wamenajisi ukuhani, na agano la kikuhani na la Walawi.
30 I did all that to make sure that there were no more foreign people among the [Israeli] people [who would encourage them to worship idols]. I also established regulations for the priests and [other] descendants of Levi, in order that they would know what work they should do.
Kwa hiyo niliwatakasa makuhani na Walawi kutokana na chochote kilichokuwa cha kigeni, na kuwapa wajibu, kila mmoja katika kazi yake.
31 I also arranged for people to bring the firewood [that was needed to burn on the altar, as Moses had declared] that we should [do]. I also arranged for the people to bring the first part of what they harvested [each year]. My God, do not forget [that] I [have done all these things], and bless me [for doing them]!
Pia nilihakikisha kwamba matoleo ya kuni yaliletwa kwa wakati unaopaswa, na malimbuko kwa wakati wake. Ee Mungu wangu, unikumbuke, unitendee mema.

< Nehemiah 13 >