< Nahum 1 >

1 [I am] Nahum, from Elkosh [village]. [This is] a message about Nineveh [city, the capital of Assyria that was given] to me in a vision [by Yahweh].
Neno alilosema Mungu kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono cha Nahumu, Mwelkoshi.
2 Yahweh our God (is jealous/does not want people to worship any other god). He is very angry [with those who worship other gods], and he gets revenge [DOU] [on all] those who oppose him [DOU].
Bwana ni mwenye wivu na Mungu mlipiza kisasi; Bwana hulipiza kisasi na amejaa ghadhabu. Bwana hulipiza kisasi juu ya watesi wake, naye anadumisha ghadhabu yake dhidi ya adui zake.
3 Yahweh does not quickly become angry; but he is very powerful, and he will certainly punish [LIT] those who have done evil things [MTY]. He shows his power by sending whirlwinds and storms, and clouds are [like] [MET] the dust [stirred up by] his feet.
Bwana si mwepesi wa hasira naye ni mwenye nguvu, Bwana hataacha kuadhibu wenye hatia. Njia yake ipo katika kisulisuli na tufani, na mawingu ni vumbi la miguu yake.
4 When he commands oceans and rivers to become dry, they dry up. [He causes the grass in the fields in] the Bashan [region] and [on the slopes of] Carmel [Mountain] to wither, [and causes] the flowers in Lebanon to fade.
Anakemea bahari na kuikausha, anafanya mito yote kukauka. Bashani na Karmeli zinanyauka na maua ya Lebanoni hukauka.
5 When he appears, [it is as though] the mountains shake and the hills melt; the earth quakes and [the people on] the earth tremble.
Milima hutikisika mbele yake na vilima huyeyuka. Nchi hutetemeka mbele yake, dunia na wote waishio ndani yake.
6 There is no one [RHQ] who can resist him when he becomes extremely angry; there is no one [RHQ] who can survive when his anger is very hot. When he is very angry, [it is as though] his anger is like [SIM] a blazing fire, and [it is as though] mountains are shattered into pieces.
Ni nani awezaye kuzuia hasira yake yenye uchungu? Nani awezaye kuvumilia hasira yake kali? Ghadhabu yake imemiminwa kama moto, na miamba inapasuka mbele zake.
7 But he is good; he protects [us his people] when we experience troubles. He takes care of those who trust in him.
Bwana ni Mwema, kimbilio wakati wa taabu. Huwatunza wale wanaomtegemea,
8 But he will get rid of his enemies; he will be to them [like] [MET] a flood that destroys everything. He will chase his enemies into the darkness [of the place where the dead are].
lakini kwa mafuriko makubwa, ataangamiza Ninawi; atafuatilia adui zake hadi gizani.
9 [So], it is useless [RHQ] for you [people of Nineveh] to plot against Yahweh. He will not [need to] strike you two times to destroy you; he will destroy you [by striking you only once].
Shauri baya lolote wapangalo dhidi ya Bwana yeye atalikomesha; taabu haitatokea mara ya pili.
10 [It will be as though his enemies] are tangled in thorns, and they will stagger like people who have drunk a lot of wine. They will be burned up like [SIM] a fire completely burns up stubble/straw.
Watasongwa katikati ya miiba na kulewa kwa mvinyo wao. Watateketezwa kama mabua makavu.
11 In Nineveh [city] there was a man who advised people to do very wicked things to Yahweh.
Ee Ninawi, kutoka kwako amejitokeza mmoja, ambaye anapanga shauri baya dhidi ya Bwana na kushauri uovu.
12 But this is what Yahweh says [about you Israeli people]: “Although the people of Assyria have very many people and their army is very powerful, they will be destroyed and will disappear. [I say to my people in Judah, ] ‘have [already] punished you, but I will not punish you again.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Ingawa wana muungano nao ni wengi sana, watakatiliwa mbali na kuangamia. Ingawa nimekutesa wewe, ee Yuda, sitakutesa tena.
13 Now I will cause the [people of Assyria] to no longer control/oppress you [MET]; [it will be as though] I will tear off the shackles/chains on your [hands and feet].”
Sasa nitavunja nira zao kutoka shingo yako, nami nitazivunjilia mbali pingu zako.”
14 [And this is what] Yahweh also declares about you people of Nineveh: “You will not have any descendants who will continue to have your family names. And I will destroy all the statues of your gods that were carved or formed in molds. I will cause you [to be killed and] sent to your graves, because you are vile/despicable!”
Hii ndiyo amri Bwana aliyoitoa kukuhusu wewe, Ninawi: “Hutakuwa na wazao watakaoendeleza jina lako. Nitaharibu sanamu za kuchonga na sanamu za kuyeyusha ambazo zipo katika hekalu la miungu yenu. Nitaandaa kaburi lako, kwa maana wewe ni mwovu kabisa.”
15 [You people of Judah, ] look! A messenger will be coming across the mountains, and he [SYN] will be bringing good news [to you]. He will be declaring [that you will now have] peace [because Assyria will have been conquered]. [So, ] celebrate your festivals, and do what you solemnly promised to do [when your enemies were threatening to attack you], because your wicked [enemies] will not invade your country again, [because] they will be completely destroyed.
Tazama, huko juu milimani, miguu ya huyo mmoja aletaye habari njema, ambaye anatangaza amani! Ee Yuda, sherehekea sikukuu zako, nawe utimize nadhiri zako. Waovu hawatakuvamia tena; wataangamizwa kabisa.

< Nahum 1 >