< Micah 3 >

1 Then I said, “You Israeli [MTY] leaders, listen [to what I say]! You should certainly [RHQ] know what things are right [to do] [and what things are wrong],
Kisha nikasema, “Sikilizeni enyi viongozi wa Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli. Je, hampaswi kujua hukumu,
2 but you hate what is good and you love what is evil. [You act like butchers]: [it is as though] you strip the skin off my people and [tear] the flesh from their bones.
ninyi mnaochukia mema na kupenda maovu; ninyi mnaowachuna watu wangu ngozi na kuondoa nyama kwenye mifupa yao;
3 [It is as though] you chop them into pieces like [SIM] meat [to be cooked] in a pot.
ninyi mnaokula nyama ya watu wangu, mnaowachuna ngozi na kuvunja mifupa yao vipande vipande; mnaowakatakata kama nyama ya kuwekwa kwenye sufuria na kama nyama ya kuwekwa kwenye chungu?”
4 Then, [when you have troubles], you plead to Yahweh [to help you], but he will not answer you. At that time, he will turn away from you because of the evil things that you have done.”
Kisha watamlilia Bwana, lakini hatawajibu. Wakati huo atawaficha uso wake kwa sababu ya uovu waliotenda.
5 This is what Yahweh says about your [false] prophets who are deceiving the people: “If someone gives them food, those prophets say that things will go well for him. But they declare war against anyone who does not give them food.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kuhusu manabii wanaowapotosha watu wangu, mtu akiwalisha, wanatangaza ‘amani’; kama hakufanya hivyo, wanaandaa kupigana vita dhidi yake.
6 So [now it is as though] [MET] night will descend on you prophets; you will not receive any [more] visions. [It is as though] [MET] the sun will set for you; the time [when you are greatly honored] will end.
Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono, na giza, msiweze kubashiri. Jua litawachwea manabii hao, nao mchana utakuwa giza kwao.
7 [Then] you (seers/people who predict what will happen in the future) [DOU] will be disgraced; you will cover your faces [because you will be ashamed], because when you ask me [what will happen], there will be no answer from me.”
Waonaji wataaibika na waaguzi watafedheheka. Wote watafunika nyuso zao kwa sababu hakuna jibu litokalo kwa Mungu.”
8 But as for me, I am full of [God’s] power, [power] from the Spirit of Yahweh. I am courageous and strong to declare to the Israeli people [MTY, DOU] that they have sinned and rebelled [against Yahweh].
Lakini kuhusu mimi, nimejazwa nguvu, nimejazwa Roho wa Bwana, haki na uweza, kumtangazia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
9 You leaders of the people [MTY] of Israel, listen to this! You hate [it when people do] what is just; and [when people say] what is true, you distort it, [saying it is false].
Sikieni hili, enyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli, mnaodharau haki na kupotosha kila lililo sawa;
10 [It is as though] you are building [houses in] Jerusalem on foundations that consist of murdering people and doing what is corrupt.
mnaojenga Sayuni kwa kumwaga damu na Yerusalemu kwa uovu.
11 Your leaders make [favorable] decisions [only if they receive] bribes. Your priests teach people only if [those people] pay them [well]. Your [false] prophets require people to pay them to tell people what will happen [to them] in the future. Those prophets say, “Yahweh is telling us [what we should say], and [we say that] we will not experience any disasters.”
Viongozi wake wanahukumu kwa rushwa, na makuhani wake wanafundisha kwa malipo, nao manabii wake wanatabiri kwa fedha. Hata hivyo wanamwegemea Bwana na kusema, “Je, Bwana si yumo miongoni mwetu? Hakuna maafa yatakayotupata.”
12 Because of what you [leaders do], Zion [Hill] will be plowed like a field; it will become a heap of ruins/rubble; the top of the hill, where the temple is [now], will be covered with bushes.
Kwa hiyo kwa sababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto, na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu kilichofunikwa na vichaka.

< Micah 3 >