< Matthew 2 >
1 Jesus was born in Bethlehem [town] in Judea [province] during the time [MTY] that King Herod [the Great ruled there. Some time] after Jesus was born, some men who studied the stars and who lived in a [country] east [of Judea] came to Jerusalem.
Baada ya Yesu kuzaliwa katika mji wa Bethlehemu huko Uyahudi, wakati wa utawala wa Mfalme Herode, wataalamu wa mambo ya nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu
2 They asked [people], “Where is the one who has been born [in order that he might be] the king of [you] Jews? [We believe that your new king] has been born, because we have seen the star [that we believe indicated that] he has been [born]. [We saw it while we were in our country] east [of here]. So we have come to worship him.”
wakiuliza, “Yuko wapi huyo aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tumeona nyota yake ikitokea mashariki, nasi tumekuja kumwabudu.”
3 When King Herod heard [what those men were asking], he became worried [that someone else might be proclaimed] {[people might proclaim someone else]} [king of the Jews to replace him]. Many [of the people] of Jerusalem [MTY, HYP] [also] became worried [because they were afraid of what King Herod might do].
Mfalme Herode aliposikia jambo hili aliingiwa na hofu sana pamoja na watu wote wa Yerusalemu.
4 Then Herod gathered together all the ruling priests and men who taught the people the [Jewish] laws and he asked them where [the prophets had predicted that] the Messiah was to be born.
Herode akawaita pamoja viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, akawauliza ni mahali gani ambapo Kristo angezaliwa.
5 They said to him, “[He will be born] in Bethlehem, [here] in Judea [province], because it was written by the prophet [Micah] {the prophet [Micah] wrote} [long ago what God said]:
Nao wakamwambia, “Katika Bethlehemu ya Uyahudi, kwa maana hivyo ndivyo ilivyoandikwa na nabii:
6 ‘You [who live in] Bethlehem [APO], in Judea [province], your town is certainly very important [LIT], because a man from your [town] will become a ruler. He will guide my people [who live in] Israel.’”
“‘Nawe, Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, wewe si mdogo miongoni mwa watawala wa Yuda; kwa maana kutoka kwako atakuja mtawala atakayekuwa mchungaji wa watu wangu Israeli.’”
7 Then [King] Herod secretly summoned those men who studied the stars. He asked them exactly when the star [first] appeared. [By what they told him, he was able to know the approximate age of the baby].
Ndipo Herode akawaita wale wataalamu wa nyota kwa siri na kutaka kujua kutoka kwao uhakika kamili wa wakati ile nyota ilionekana.
8 Then he [concealed what he really planned to do and] said to them, “Go to Bethlehem and inquire thoroughly [where] the infant is. When you have found him, [come back and] report to me so that I, myself, can go [there and] worship him, too.”
Kisha akawatuma waende Bethlehemu akiwaambia, “Nendeni mkamtafute kwa bidii huyo mtoto. Nanyi mara mtakapomwona, mniletee habari ili na mimi niweze kwenda kumwabudu.”
9 After the men heard what the king [told them], they went [toward Bethlehem]. To their surprise, the star that they had seen while they were in the eastern [country] went ahead of them [again] until it stood above [the house] where the child was.
Baada ya kumsikia mfalme, wale wataalamu wa nyota wakaenda zao, nayo ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, nao wakaifuata mpaka iliposimama mahali pale alipokuwa mtoto.
10 When they saw the star, they rejoiced greatly [and followed it].
Walipoiona ile nyota wakajawa na furaha kubwa mno.
11 They [found] the house and entered it and saw the child and his mother, Mary. They bowed down and worshipped him. Then they opened their treasure [boxes] [MTY] and they gave gold, [costly] frankincense, and myrrh to him.
Walipoingia ndani ya ile nyumba, wakamwona mtoto pamoja na Maria mama yake, wakamsujudu na kumwabudu yule mtoto Yesu. Ndipo wakafungua hazina zao, wakamtolea zawadi za dhahabu, uvumba na manemane.
12 [Because] God [knew that King Herod planned to kill Jesus], in a dream the men who studied the stars were warned {he warned the men who studied the stars} that they should not return to [King] Herod. So they returned to their country, [but instead of traveling back on the same road, they] went on a different road.
Nao wakiisha kuonywa katika ndoto wasirudi kwa Herode, wakarudi kwenda katika nchi yao kwa njia nyingine.
13 After the men who studied the stars left [Bethlehem], an angel [from] the Lord appeared to Joseph in a dream. He said, “Get up, take the child and his mother, and flee to Egypt. Stay there until I tell you [(sg) that you should leave], because [King] Herod is about [to send soldiers] to look for the child so that they can kill him.”
Walipokwisha kwenda zao, malaika wa Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto akamwambia, “Ondoka, mchukue mtoto na mama yake mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka nitakapowaambia, kwa maana Herode anataka kumtafuta huyu mtoto ili amuue.”
14 So Joseph got up, he took the child and his mother [that] night, and they fled to Egypt.
Kisha Yosefu akaondoka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake wakati wa usiku, nao wakaenda Misri
15 They stayed there until [King] Herod died, [and then they left Egypt]. By doing that, it was {they} fulfilled what the prophet [Hosea] wrote, which had been said by the Lord {which the Lord had said}, I have told my son to come out of Egypt.
ambako walikaa mpaka Herode alipofariki. Hili lilifanyika ili litimie lile lililonenwa na Bwana kwa kinywa cha nabii kusema: “Nilimwita mwanangu kutoka Misri.”
16 [While King] Herod [was still living], because he realized that he had been tricked by the men who studied the stars {the men who studied the stars had tricked him}, he became furious. Then, [assuming that Jesus was still in Bethlehem or the surrounding regions], Herod sent [soldiers there] to kill all the boy babies two years old and younger. [Herod calculated how old the baby was], according to what the men who studied the stars told him [about when the star first appeared].
Herode alipongʼamua kwamba wale wataalamu wa nyota wamemshinda kwa akili, alikasirika sana, naye akatoa amri ya kuwaua watoto wote wa kiume wenye umri wa miaka miwili kurudi chini katika mji wa Bethlehemu na sehemu zote za jirani, kufuatana na ule muda alioambiwa na wale wataalamu wa nyota.
17 [Because Bethlehem and Ramah towns were in the area where the descendants of Jacob’s wife Rachel lived, when soldiers killed the infant boys], they fulfilled what Jeremiah the prophet wrote,
Ndipo lilipotimia neno lililonenwa na nabii Yeremia.
18 [Women] in Ramah were weeping and wailing loudly. [Women who were the descendants] of Rachel, [the ancestor of the women there] [SYN], were grieving for [what happened to] their children. [Even though people tried to comfort them], they would not be comforted {stop mourning}, because their children were dead.
“Sauti ilisikika huko Rama, maombolezo na kilio kikubwa, Raheli akilia kwa ajili ya wanawe, akikataa kufarijiwa, kwa sababu hawako tena.”
19 After Herod died [and while Joseph and his family were still in Egypt], an angel that the Lord [had sent] appeared to Joseph in Egypt in a dream.
Baada ya Herode kufa, malaika wa Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto huko Misri
20 He said to Joseph, “Take the child and his mother and go back to Israel [to live], because the people who were looking for the child [in order to kill him] have died.”
na kusema, “Ondoka, mchukue mtoto na mama yake mwende, mrudi katika nchi ya Israeli kwa sababu wale waliokuwa wanatafuta uhai wa mtoto wamekufa.”
21 So Joseph took the child and his mother, and they went back to Israel.
Basi Yosefu, akaondoka akamchukua mtoto na mama yake wakaenda mpaka nchi ya Israeli.
22 When Joseph heard that Archaelaus now ruled in Judea [district] instead of his father, [King] Herod [the Great], he was afraid to go there. Because he was warned {[God] warned Joseph} in a dream [that it was still dangerous for them to live in Judea], he [and Mary and Jesus] went to Galilee [District]
Lakini aliposikia kwamba Arkelao alikuwa anatawala huko Uyahudi mahali pa Herode baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye akiisha kuonywa katika ndoto, akaenda zake sehemu za Galilaya,
23 to Nazareth [to live there]. The result was that what had been said by the ancient prophets {what the ancient prophets had said} [about the Messiah], that he would be called {people would call him} a Nazareth-man, was fulfilled {came true}.
akaenda akaishi katika mji ulioitwa Nazareti. Hivyo likawa limetimia neno lililonenwa na manabii, “Ataitwa Mnazarayo.”