< Luke 24 >
1 Before dawn on Sunday those women went to the tomb. They took with them the spices that they had prepared [to put on Jesus’ body].
Mnamo siku ya kwanza ya juma, alfajiri na mapema, wale wanawake walichukua yale manukato waliyokuwa wameyaandaa, wakaenda kaburini.
2 They discovered that the stone had been rolled away from [the entrance to] the tomb.
Wakakuta lile jiwe limevingirishwa kutoka kwenye kaburi,
3 They went in the tomb, but the body of the Lord Jesus was not there!
lakini walipoingia ndani, hawakuuona mwili wa Bwana Yesu.
4 They did not know what to think about that. Then suddenly two men wearing bright shining clothes stood by them!
Walipokuwa wanashangaa juu ya jambo hili, ghafula watu wawili waliokuwa wamevaa mavazi yanayongʼaa kama umeme wakasimama karibu nao.
5 The [women] were frightened. As they prostrated themselves on the ground, the two men said to them, “(You should not be seeking someone who is alive in [a place where they bury] dead people!/Why are you seeking in [a place where they bury] dead people someone who is alive?) [RHQ]
Wale wanawake, wakiwa na hofu, wakainamisha nyuso zao mpaka chini. Lakini wale watu wakawaambia, “Kwa nini mnamtafuta aliye hai miongoni mwa wafu?
6 He is not here; he has (become alive again/risen from the dead)! Remember that while he was still with you in Galilee [district] he said to you,
Hayuko hapa; amefufuka! Kumbukeni alivyowaambia alipokuwa bado yuko pamoja nanyi huko Galilaya kwamba:
7 ‘[Even though I] am the one who came from heaven, [someone] will enable sinful men to seize [MTY] me. They will [kill me by] nailing me to a cross. But on the third day [after that], I will become alive [again].’”
‘Ilikuwa lazima Mwana wa Adamu atiwe mikononi mwa watu wenye dhambi na waovu ili asulubiwe, na siku ya tatu afufuke.’”
8 The [women] remembered that he had said that.
Ndipo wakayakumbuka maneno ya Yesu.
9 So they left the tomb and went to the eleven [apostles] and his other [disciples] and told them those things.
Waliporudi kutoka huko kaburini, wakawaeleza wale wanafunzi kumi na mmoja pamoja na wengine wote mambo haya yote.
10 The ones who kept telling those things to the apostles were Mary from Magdala [village], Joanna, Mary who was the mother of James, and the other women [who were] with them.
Basi Maria Magdalene, Yoana, na Maria mama yake Yakobo, pamoja na wanawake wengine waliofuatana nao ndio waliwaelezea mitume habari hizi.
11 But the apostles thought that what the women [said] was nonsense. They did not believe what the women said.
Lakini hawakuwasadiki hao wanawake, kwa sababu maneno yao yalionekana kama upuzi.
12 But Peter got up and ran to the tomb [anyway]. He stooped down [and looked inside]. He saw the linen cloths [in which Jesus’ body had been wrapped]. [The cloths were] by themselves (OR, [He did not see] anything else). So, wondering what had happened, he went home.
Hata hivyo, Petro akainuka na kukimbia kwenda kule kaburini. Alipoinama kuchungulia, akaona vile vitambaa vya kitani, ila hakuona kitu kingine. Naye akaenda zake akijiuliza nini kilichotokea.
13 That same day two of [Jesus’ disciples] were walking to a village named Emmaus. It was about (seven miles/eleven kilometers) from Jerusalem.
Ikawa siku iyo hiyo, wanafunzi wawili wa Yesu walikuwa njiani wakienda kijiji kilichoitwa Emau, yapata maili saba kutoka Yerusalemu.
14 They were talking with each other about all the things that had happened [to Jesus].
Walikuwa wakizungumza wao kwa wao kuhusu mambo yote yaliyotukia.
15 While they were discussing those things, Jesus himself approached them and started walking with them.
Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akaja akatembea pamoja nao,
16 But they were prevented {[something] prevented them} from recognizing [MTY] him.
lakini macho yao yakazuiliwa ili wasimtambue.
17 [Jesus] said to them, “What have you two been talking about while you were walking?” They stopped, and their faces looked very sad.
Akawauliza, “Ni mambo gani haya mnayozungumza wakati mnatembea?” Wakasimama, nyuso zao zikionyesha huzuni.
18 One of them, whose name was Cleopas, said, “(You [(sg)] must be the only person who is visiting Jerusalem [for the Passover festival] who does not know the events that have happened there in recent days!/Are you the only person who is visiting Jerusalem [for the Passover festival] who does not know the events that have happened there in recent days?) [RHQ]”
Mmoja wao, aliyeitwa Kleopa, akamuuliza, “Je, wewe ndiye peke yako mgeni huku Yerusalemu ambaye hufahamu mambo yaliyotukia humo siku hizi?”
19 He said to them, “What events?” They replied, “[The things that happened] to Jesus, [the man] from Nazareth, who was a prophet. Many people saw him [perform] great miracles, and God [enabled him] to teach wonderful [messages]!
Akawauliza, “Mambo gani?” Wakamjibu, “Mambo ya Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii, mwenye uwezo mkuu katika maneno yake na matendo yake, mbele za Mungu na mbele ya wanadamu wote.
20 But our chief priests and leaders handed him over [to the Roman authorities. The authorities] sentenced him to die, and they killed him by nailing him to a cross.
Viongozi wa makuhani na viongozi wetu walimtoa ahukumiwe kufa, nao wakamsulubisha.
21 We [(exc)] were hoping that he was the one who would free [us] Israelites [from our enemies] But [this does not seem possible now, because] three days have [already] passed since that happened.
Lakini tulikuwa tumetegemea kwamba yeye ndiye angelikomboa Israeli. Zaidi ya hayo, leo ni siku ya tatu tangu mambo haya yatokee.
22 On the other hand, some women from our group amazed us. Early this morning they went to the tomb,
Isitoshe, baadhi ya wanawake katika kundi letu wametushtusha. Walikwenda kaburini leo alfajiri,
23 but Jesus’ body was not there! They came [back] and said that they had seen some angels in a vision. The angels said that he was alive!
lakini hawakuukuta mwili wake. Walirudi wakasema wameona maono ya malaika ambao waliwaambia kwamba Yesu yu hai.
24 Then some of those who were with us went to the tomb. They saw that things were exactly as the women had reported. But they did not see [Jesus].”
Kisha baadhi ya wenzetu walikwenda kaburini wakalikuta kama vile wale wanawake walivyokuwa wamesema, lakini yeye hawakumwona.”
25 He said to them, “[You two] foolish [men! You are so] slow to believe all that the prophets have written [about the Messiah]!
Yesu akawaambia, “Ninyi ni wajinga kiasi gani, nanyi ni wazito mioyoni mwenu kuamini mambo yote yaliyonenwa na manabii!
26 ([You should certainly have known that] it was necessary that the Messiah should suffer all those things [and die], and then enter his glorious [home in heaven]!/Was it not necessary that the Messiah should suffer all those things [and die], and then enter his glorious [home in heaven]?) [RHQ]”
Je, haikumpasa Kristokuteswa kwa njia hiyo na kisha aingie katika utukufu wake?”
27 Then he explained to them all the things that [the prophets] had written in the Scriptures about himself. He started with what Moses [MTY] [wrote] and then explained to them what all the [other] prophets [wrote].
Naye akianzia na Sheria ya Mose na Manabii wote, akawafafanulia jinsi Maandiko yalivyosema kumhusu yeye.
28 They came near to the village to [which the two men] were going. Jesus indicated that he would go further,
Nao walipokaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, Yesu akawa kama anaendelea mbele.
29 but they urged him [to not do that]. They said, “Stay with us [tonight], because it is late in the afternoon and it will soon be dark.” So he went in [the house] to stay with them.
Lakini wao wakamsihi sana akae nao, wakisema, “Kaa hapa nasi, kwa maana sasa ni jioni na usiku unaingia.” Basi akaingia ndani kukaa nao.
30 When they sat down to eat, he took some bread and [asked God to] bless it. He broke it and gave [some pieces] to them.
Alipokuwa mezani pamoja nao, akachukua mkate, akashukuru, akaumega, akaanza kuwagawia.
31 And just then [God] enabled them to recognize [MTY] him. But [immediately] he disappeared!
Ndipo macho yao yakafumbuliwa, nao wakamtambua, naye akatoweka machoni pao. Hawakumwona tena.
32 The two men said to each other, “[While we were walking] along the road and he talked with us and [enabled] us [(inc)] to understand the Scriptures, we [became so excited that it was as though] [MET] a fire was burning within us [RHQ]! [We should not stay here; we should go tell the others what happened]!”
Wakaulizana wao kwa wao, “Je, mioyo yetu haikuwakawaka kwa furaha ndani yetu alipokuwa anazungumza nasi njiani na kutufafanulia Maandiko?”
33 So they left immediately and returned to Jerusalem. There they found the eleven [apostles] and others who had gathered together with them
Wakaondoka mara, wakarudi Yerusalemu. Wakawakuta wale wanafunzi kumi na mmoja na wale waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika
34 who told [those two men], “It is true that the Lord has become alive again, and he has appeared to Peter!”
wakisema, “Ni kweli! Bwana amefufuka, naye amemtokea Simoni.”
35 Then those two [men] told [the others] what had happened [as they were walking] along the road. They also [told them how] they both recognized Jesus as he broke some bread [for them].
Kisha wale wanafunzi wawili wakaeleza yaliyotukia njiani na jinsi walivyomtambua Yesu alipoumega mkate.
36 As they were saying that, Jesus himself [suddenly] appeared among them. He said to them, “[May God give] you [inner] peace!”
Walipokuwa bado wanazungumza hayo, Yesu mwenyewe akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”
37 They were startled and afraid, [because] they thought that they were seeing a ghost!
Wakashtuka na kuogopa wakidhani kwamba wameona mzuka.
38 He said to them, “(You should not be alarmed!/Why are you alarmed?) [RHQ] And (you should not be doubting [that I am alive]/Jesus!/why are you doubting [that I am alive]/Jesus?) [RHQ]
Lakini Yesu akawauliza, “Kwa nini mnaogopa? Kwa nini mna shaka mioyoni mwenu?
39 Look at [the wounds in] my hands and my feet! You can touch me and see [my body]. Then you can see that it is really I myself. [You can tell that I am really alive] because ghosts do not have bodies, as you see that I have!”
Tazameni mikono yangu na miguu yangu, mwone kuwa ni mimi hasa. Niguseni mwone; kwa maana mzuka hauna nyama na mifupa, kama mnionavyo kuwa navyo.”
40 After he said that, he showed them [the wounds in] his hands and his feet.
Aliposema haya, akawaonyesha mikono na miguu yake.
41 They were joyful and amazed, [but] they still did not believe [that he was really alive] (OR, [that Jesus was the one that they were seeing]). [So] he said to them, “Do you have anything here to eat?”
Wakashindwa kuamini kwa ajili ya furaha na mshangao waliokuwa nao. Akawauliza, “Mna chakula chochote hapa?”
42 [So] they gave him a piece of broiled fish.
Wakampa kipande cha samaki aliyeokwa,
43 While they were watching, he took it and ate it.
naye akakichukua na kukila mbele yao.
44 Then he said to them, “[I will repeat] what I told you while I was still with you: Everything that was written about me by Moses and the [other] prophets [MTY] and in the Psalms must be fulfilled!”
Akawaambia, “Haya ndiyo yale niliyowaambia nilipokuwa bado niko pamoja nanyi, kwamba yote yaliyoandikwa kunihusu mimi katika Sheria ya Mose, Manabii na Zaburi hayana budi kutimizwa.”
45 Then he enabled them to understand [the things that had been written about him in] the Scriptures.
Ndipo akafungua fahamu zao ili waweze kuyaelewa Maandiko.
46 He said to them, “This is what they wrote: That the Messiah would suffer [and die], but on the third day after that he would become alive again.
Akawaambia, “Haya ndiyo yaliyoandikwa: Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka kwa wafu.
47 [They] also [wrote that the message] must be preached {[that his disciples] must preach [the message]} [everywhere that people] must turn from their sinful ways for [God] to forgive their sins. [They wrote that his followers should preach that message, claiming] his authority [MTY]. They wrote that they should start [preaching] it in Jerusalem, and then [go and] preach it to all ethnic groups.
Toba na msamaha wa dhambi zitatangaziwa mataifa yote kupitia jina lake kuanzia Yerusalemu.
48 You [apostles] must tell people that you know that those things [that happened to me] are true.
Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.
49 And I want you to know that I will send the [Holy Spirit] [MTY] to you, as my Father promised that [he would do]. But you must stay in this city until God fills you with the power [of his Spirit].”
“Tazama nitawatumia ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini hadi mtakapovikwa uwezo utokao juu.”
50 Then [Jesus] led them outside [the city] until they came near Bethany [village]. There he lifted up his hands and blessed them.
Akiisha kuwaongoza mpaka kwenye viunga vya Bethania, akainua mikono yake juu na kuwabariki.
51 As he was doing that, he left them [and went up to heaven].
Alipokuwa anawabariki, akawaacha, akachukuliwa mbinguni.
52 They worshipped him. And then they returned to Jerusalem very joyfully.
Kisha wakamwabudu na kurudi Yerusalemu wakiwa wamejawa na furaha kuu.
53 Each day [SYN] they went into the Temple [courtyard], and spent a lot of time praising God.
Nao wakadumu ndani ya Hekalu wakimtukuza Mungu. Amen.