< Leviticus 9 >
1 Eight days later, Moses/I summoned the elders of Israel.
Katika siku ya nane, Musa akawaita Aroni na wanawe pamoja na wazee wa Israeli.
2 Then he/I said to Aaron, “Take a young bull for the offering to enable you leaders to be forgiven for the sins you have committed, and a ram to be completely burned [on the altar], both of them without any defects, and offer them to Yahweh.
Akamwambia Aroni, “Twaa ndama dume kutoka kundini kwa ajili ya sadaka ya dhambi zako, na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, wote wawili wasiwe na dosari, na uwatoe mbele za Yahweh.
3 Then say to the Israeli people, ‘Take one male goat for the offering to enable you all to be forgiven for the sins you have committed. Also take a calf and a lamb that have no defects, to be an offering completely burned [on the altar].
Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Twaeni beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi na ndama na mwana-kondoo, hawa wawili wawe na umri wa mwaka mmoja na bila dosari, ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
4 Also take an ox and a ram to be an offering to maintain fellowship [with Yahweh], along with an offering of flour mixed with olive oil. Do this because today Yahweh is going to appear to you.’”
pia twaeni fahali na kondoo dume kwa sadaka za amani ili kuwatoa mbele za Yahweh, na sadaka za nafaka iliyochanganywa na mafuta, kwa sababu leo Yahweh atajidhihirisha kwenu.
5 [After Moses/I told this to the Israeli people, some of them] took the things that Moses/I had commanded them to take, and went to the courtyard in front of the Sacred Tent. Then all the people came near and stood in front of Yahweh.
Kwa hiyo wakaleta kwenye hema la kukutania vyote ambavyo Musa aliagiza, nalo kusanyiko lote la Israeli likakaribia na kusimama mbele za Yahweh.
6 Then Moses/I said, “This is what Yahweh has commanded you to do, in order that his glory will appear to you.”
Kisha Musa akasema, “Hivi ndivyo Yahweh amewaamru nyinyi mfanye, ili kwamba utukufu wake uweze kuonekana kwenu.
7 Then Moses/I said to Aaron, “Come to the altar and sacrifice the animal that is your offering to enable you to be forgiven for the sins you have committed, and the animal that will be completely burned there. Because of those offerings, God will forgive you and the people for the sins that you have committed [DOU]. Do those things that Yahweh has commanded.”
“Musa akamwambia Aroni, “Njoo karibu na Madhabahu na uteo sadaka yako ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa, na kufanya upatanisho kwa ajili ya watu ili kufanya upatanisho kwa ajili yao kama vile ambavyo Yahweh amekwishaamru.”
8 So Aaron came close to the altar and slaughtered the calf to be an offering for his sins.
Kwa hiyo Aroni akaikaribia madhabahu na akamchinja yule ndama kwa ajili ya sadaka ya dhambi, ambayo ilikuwa kwa ajili yake mwenyewe.
9 His sons brought its blood to him [in a bowl]. He dipped his finger into the blood and put some of it on the projections at the corners of the altar. He poured out the rest of the blood at the base of the altar.
Nao wana wa Aroni wakamletea hiyo damu, naye akakichofya kidole chake kwenye damu na kuiweka kwenye pembe za madhabahu, kisha akaimwaga damu chini ya kitako cha madhabahu.
10 He/I burned the fat, including that which covered the kidneys and the liver, as Yahweh had commanded him/me.
Hata hivyo, aliyateketeza hayo mafuta, figo, na mafuta yanafunika ini juu ya madhabahu kuwa sadaka ya dhambi, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamru Musa.
11 Then Aaron burned [the rest of] the meat and the hide/skin outside the camp.
Na akaiteketeza hiyo nyama pamoja na ngozi nje ya kambi
12 Then Aaron slaughtered the animal that would be completely burned [on the altar]. His sons handed him [the bowl containing] its blood, and he sprinkled the blood on all sides of the altar.
Aroni akaichinja sadaka ya kuteketezwa, nao wanawe wakampa hiyo damu, ambayo aliinyunza pande zote za madhabahu.
13 Then they handed him the head and the pieces of the animal that would be burned, and he burned them on the altar.
Kisha wakampa ile sadaka ya kuteketezwa, kipande kwa kipande, pamoja na kichwa, naye akaviteketeza juu ya madhabahu.
14 He washed the inner parts and the legs of the animal, and burned them on the altar, on top of the other pieces of the animal.
Akaziosha sehemu za ndani pamoja na miguu na kuziteketeza juu ya dhabihu ya kuteketezwa juu ya Madhabahu.
15 Then Aaron brought the animals that would be sacrifices for the Israeli people. He took the goat and slaughtered it to be an offering to enable them to be forgiven for the sins they had committed, like he had done with the goat for his own offering.
Aroni akaleta dhabihu ya watu— mbuzi, kisha akamtoa kuwa dhabihu kwa ajili ya dhambi yao naye akamchinja, akaitoa dhabihu kwa ajili ya dhambi, kama alivyofanya kwa yule mbuzi wa kwanza.
16 Then he brought the animal for the offering to be completely burned. He slaughtered it and offered it in the way that Yahweh had commanded him to do.
Akaileta sadaka ya kuteketezwa na kuitoa kama Yahweh alivyokuwa ameamru.
17 He also brought the offering of grain. He took a handful of it and burned it on the altar, like he had done for the animal that he had slaughtered and completely burned [on the altar] in the morning.
Akaileta sadaka ya nafaka; akakijaza kiganja chake nafaka na kuiteketeza juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa.
18 Then he slaughtered the ox and the ram, to be an offering for the Israeli people to maintain fellowship with Yahweh. His sons handed him [the bowl containing] the blood, and he sprinkled the blood against all sides of the altar.
Pia akamchinja fahali na yule kondoo dume, dhabihu kwa ajili ya sadaka ya amani, ambayo ilikuwa kwa ajili ya watu. Nao wana wa Aronni wakampa damu, ambayo aliinyunyiza kila upande wa mdhabahu.
19 But he took the fat from the ox and the ram, including their fat tails that were cut close to the backbone, and all the fat that covered the livers and the kidneys.
Hata hivyo, waliyakata mafuta ya fahali na ya yule kondoo dume, mafuta ya kwenye mkia, mafuta yafunikayo sehemu za ndani, figo, na yale mafuta yaliyofunika mapafu.
20 He put them on top of the breasts of those animals and carried them to the altar to be burned.
Wakazichukua hizi sehemu zilizokatwa wakaziweka juu ya vidari, na kisha Aroni akateketeza mafuta juu ya madhabahu.
21 Then, doing what Moses/I had commanded, he lifted up in front of Yahweh the breast and the right thigh of those animals, to signify that those two animals completely belonged to Yahweh.
Naye Aroni akavitikisa vidari na paja la kulia kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh, kama vile Musa alivyokuwa ameamru,
22 Then Aaron lifted his arms toward the people and [asked Yahweh to] bless them. Then having finished making all those offerings, he stepped down [from the place where the altar was].
Kisha Aroni akainua juu mikono yake mbele ya watu na kuwabariki, kisha akashuka chini kutoka mahali alipokuwa akitoa hiyo sadaka ya dhambi, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya amani.
23 Then Aaron and Moses/I entered the Sacred Tent. When they/we later came out, they/we [asked Yahweh to] bless the people. And suddenly the glory/brightness of Yahweh appeared to all the people.
Musa na Aroni wakaingia ndani ya hema la kukutania, kisha wakatoka nje tena na kuwabariki watu, na utukufu wa Yahweh ukaonekana kwa watu wote.
24 A fire from Yahweh appeared and burned up the offering that was to be completely burned and the fat that was on the altar. And when all the people saw that, they shouted joyfully and prostrated themselves on the ground [to worship Yahweh].
Moto ukashuka kutoka kwa Yahweh na ukairamba sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wlipoona jambo hili, wakapiga kelele na kulala chini.